VIDEO - Mwigulu Nchemba - CHADEMA NI WAUWAJI

Benz Petrol

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
504
195
Ndugu wanajamvi,

Hebu tazameni siasa za maji taka za Mwigulu na magamba wenzake katika moja ya kampeni za udiwani Arusha: MWIGURU AKILI KUHUSIKA NA MKANDA WA LWAKATALE; ATUMIA SIASA ZA MAJITAKA KUOMBEA KURA ARUSHA - YouTube



  • Asema Chadema wanaua katika mikutano yao na kuwaambia wafadhili kwamba serikali inakadamiza upinzani
  • ANUKULIWA "CHADEMA NI CHAMA CHA WAUAJI MPAKA SASA WAMEUWA WATU ZAIDI YA WANANE"
  • Amkaribisha kwenye jukwa kijana Musa aliyemwagiwa tindikali Igunga na kuwaambia wananchi ni kazi ya Chadema
  • ABAINISHA KUWA YEYE NDIYO ALIYETOA VITENDEA KAZI KWENYE VIDEO INAYODAIWA YA UGAIDI YA LWAKATARE

My take: WaTanzania wa leo, sio wazamani. CCM mtaji wao ni umbumbubu wa wananchi ndiyo maana bado wanakuja na siasa chafu kama hizi. Basi kwa taarifa yenu magamba kwa siasa hizi 2015 bye bye!

Update: Ndugu Benson Kigaila akitoa majibu juu ya shtuma za Mwigulu Nchemba dhidi ya Chadema

 
Last edited by a moderator:
Inabidi CDM wamfungulie kesi huyu jamaa ili alete ushahidi maana amezoea uongo.
 
Tunawaomba wote wenye mapenzi mema na nchi hii waendelee kuomba kwa nguvu zote hawa watajitaja wenyewe kwa wenyewe. Tuleteeni story na uthibitisho kama huu wapendwa hawa jamaa ni wepesi kuliko mnavyodhani, wanaishi kwa nguvu za TISS na Polisi hata Mwenyekiti wao alisha thibitisha kwamba wasiendelee kutegemea polisi.

Ikumbukwe siku zao sasa zinahesabika, "HUWEZI KUWADANGANYA WATU WOTE KILA WAKATI"
 
Naamini huyu jamaa akili zimeanza kumruka. Mtu ukishafikia kiwango cha kujiaminisha uongo wako mwenyewe (kujidanganya), basi wewe ni mufilisi.

Hivi anadhani waTanganyika ni wajinga kiasi hicho? Kwamba mauaji ya Morogoro, Iringa, Singida yamefanywa na CHADEMA?

bahati mbaya hata hao waliopewa majukumu ya kulinda Usalama wa Raia huende wapo likizo. Vinginevyo Mwiguli alitakiwa afunguliwe mashitaka ya kutoa shutuma za uongo.
 
Jamaa ushahidi anao kama wakienda mahakamani atawashinda sana.

Mkuu mwingine upi mkuu tofauti na polisi walionao!! Story za kuwadanganya wananchi kwenye mikutano huwa tofauti mahakamani mkuu na ni tofauti na unavyofikiria!

LIle suala tu la ugaidi limeshakwama mahakamani!! Usiombe mahakama mkuu! na huko hakuna jaziba!

Huwezi kulipia uharifu kwa kupata video ya uharifu!!

Tusidanganyane kabisa!!
 
Ikiwa hivi ndiyo ilikuwa tusubiri mahakamani itakuwaje? Mh Mwiguru isingekuwa yema kuhusisha vyombo vya usalama mara bahada ya kupata tishio wao wakaifanya kwa weledi kuliko wewe kununua kamera na kumpa mtu akarekodi?
 
Mtu mzima unayefikiria kabisa kusaka tu huruma ya Kura huwezi sema uwongo uliopitiliza namna hiyo! Kwamba Mwangosi aliuwawa na CDM! dha inauma sana but Mungu yupo!! Kule Arusha mtu kakatwa shingoni na shoka nao wakawa CDM! Morogoro CDM wakawa wanafukuza wanachama wao kwa risasi!!??

Pls Mwigulu mgeukie japo Mungu uone anavyokuangalia!!
 
Ikiwa hivi ndiyo ilikuwa tusubiri mahakamani itakuwaje? Mh Mwiguru isingekuwa yema kuhusisha vyombo vya usalama mara bahada ya kupata tishio wao wakaifanya kwa weledi kuliko wewe kununua kamera na kumpa mtu akarekodi?


Mwigulu akawa Polisi na ndiye usalama wa Taifa kupata na kurekodi uharifu!! na akawa mlipaji wake! hii kali!
 
Mwigulu akawa Polisi na ndiye usalama wa Taifa kupata na kurekodi uharifu!! na akawa mlipaji wake! hii kali!
Ndiyo maana inanishangaza kwa nini PolisI na mwendesha mashitaka wa serkali bado wanaendelea nayo? Kwa maelezo yake hapa nina wasiwasi kama ushahidi huu utakubaliwa mahakamani!
 
Huyu jamaa kichwani hayuko sawa haki ya mungu tena najiapia.kuna mtu alisema kuwa mwigulu aliwahi kuugua uendawazimu utotoni kweli sasa nakubali kwasababu mtu mwenye akili timamu hawezi kusema au kufanya mambo anayofanya nchemba isipokuwa kwa mtu mwenye psychosism issues tu.huyu jamaa sio mzima kabisa,kwanini ccm wasimpeleke kwa watalaam wa magonjwa ya akili.iko siku atakuja kufanya kitu cha ajabu bungeni tukaishia kupata aibu kubwa.huyu jamaa hajapona vizuri,god help our speaker regain her wisdom to keep our parliamentarian house away from possible disgrace!
 
Jinsi ninavyomfahamu Kikwete, Juliana Shonza akizungusha kiuno na kuonyesha umahiri wake mtasikia ameteuliwa kuwa DC

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
CCM wanao uwezo mkubwa wa kumfanyia huyu Musa operation na uso ukarudi kama ulivyokuwa. Ila wamemuacha hivyo ili wamtumie kwenye kampeni. Na hii ni uthibitisho kuwa CCM walimwagia tindikali ili kuufanya uso wake katuni la kutishia watu wakati wa kampeni. india huko huko ndiko alikopelekwa Kubenea na akarudi uso umependeza,. Iweje kwa Musa. Ni lazima kuwa kulikuwa na maagizo ya Mwingulu kuwa madaktari wahakikishe kuwa huo uso unarudi ukiwa wa kutisha ili atakaposimamama kwenye kampeni watu haswa kina mama waogope.
 
Kwa hiyo Mwigulu anamtumia huyo kijana kutafuta sympathy ya wapiga kura? Mbinu hiyo inaweza kufanyakazi kule Iramba sio Arusha. Na sasa Chadema ndio inatumika kuwaomba kura wananchi na wala sio sera za chama? Halafu mwenyekiti wa CCM, katibu mkuu na makamu mwenyekiti wanajiona kwamba kweli wako kwenye siasa? Kwa mtindo huu CCM bye bye.

Tiba
 
Back
Top Bottom