Uchaguzi 2020 Video: Mapokezi ya Tundu Lissu huko Igunga

Dah kipi kinafanya Magu akataliwe kwa kiwango hiki? Mbona akina Pascal walidai jamaa hana haja ya kufanya kampeni 2020..
Kila kitu kimesimama wanaofaidi ni wachache tu mfano ununuzi wa wapinzani wamelipwa pesa nyingi kusaliti wananchi waliowachagua, watu wameumia sana na lile zoezi CCM hawajui tu. Ubabe mfano mdogo dhuluma anayotendewa Lissu waziwazi ni kichaa pekee anaweza kuunga mkono. Maneno yanayotoka kwenye kinywa cha mkuu ndio usiseme ' Mkichagua wapinzani mtajuta!. Kifupi mambo ni mengi saana.
 
Lissu ni mpango wa .Mungu Mwenyezi Muumba wa mbingu na dunia. Huyu jamaa ni zawadi ya kipekee sana aliyotupa Mungu. Mwaka huu, liwake jua, inyeshe mvua lazima wananchi wa Tanzania kwa nguvu moja na sauti moja, tumsimike huyu mtu ikulu.

Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020-2025 ni Tundu Antiphas Lissu
 
Kile kipande cha kuzomea hakiko hapa ee?

Watu wamempokea vizuri badae akaanza kupiga umbea na mitusi bila kuwaambia utatuzi wa changamoto zao wakaona bure kabisa huyu wakazomea wee.
 
49 Reactions
Reply
Back
Top Bottom