Ulaya ndio kimbilio la waafrika wanaoteswa na waafrika wenzao Ili wamalizweLissu mtu mbinafsi kupita kiasi. Ingekua mandela amegeuza kufungwa kwake ndio ajenda kuu kwenye siasa zake sijui ingekuaje. Halafu unakuta mijinga inamlinganisha lissu na mandela. Mtu tangu ajeruhiwe na watu hawajulikani ndio imekua siasa zake. Anafikiria usalama wake binafsi na kulipiza kisasi tu. Mtu mbinafsi muoga kama kunguru anaweza kuongoza kitu gani zaidi ya kutafuta maslahi binafsi?
Thomas Sankara alisema tofauti ya mwanamapinduzi na mchumia tumbo ni namna mtu alivyo tayari kutoa uhai wake bila kujutia katika kupigania maslahi ya umma. Lissu ni mwanasiasa mchumia tumbo tu. Kwa hofu ya maisha yake yeye na familia yake amewakimbia wale anaodai kuwatetea kwenda kuishi brussels kwa fadhila ya mabeberu. Mji wa brussels ubeljiji ndio mahali wakoloni waliketi mwaka 1884 kugawana bara la afrika.