VIDEO: Kero ya Mbwa Nairobi, Kenya yasababisha kutungwa kwa hii sheria

Mwendo Kasii

JF-Expert Member
Sep 10, 2016
203
212
upload_2016-9-16_16-4-57.jpeg

Jiji la Nairobi limeingia tena kwenye headlines mpya baada ya kupitisha sheria itakayowabana wafugaji wa Mbwa. Ripoti zinasema iwapo Mbwa wako atabweka kwa dakika 6 mfululizo ndani ya saa moja au dakika tatu mfululizo ndani ya dakika 30 utatozwa faini ya Shilingi elfu tano za Kenya ambazo ni sawa na Shilingi laki moja na elfu saba mia sita za Tanzania au utatumikia kifungo cha miezi miwili jela.

Wataalamu wa mifugo wanasema pamoja na kupitishwa kwa sheria hiyo, kuna muda ukifika inakua vigumu sana kumfundisha Mbwa kubweka na kunyamaza.

Kituo cha TV cha K24 wameripoti kuhusu kero ya kelele za Mbwa kubweka kiholela imesababisha kutungwa kwa sheria ya kudhibiti ubwekaji wa aina hiyo.


source: Millard Ayo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom