VIDEO: Eti huyu naye ni mheshimiwa, ana diplomatic passport

Sexer

JF-Expert Member
Oct 22, 2014
8,204
7,892

napiga picha jinsi congressmen pale US walivyo vs huyu MP wa hapa kwetu, ni aibu!!
 
Watu wa aina hii wanastahili kuwa bungeni kwa ajili ya burudani.

Mkuu;
Nadhani sijakuelewa, wawepo kwenye bunge la burudani au kwa ajili ya burudani. Kule Uingereza walikuwepo watu wa aina hii wakiitwa Clowns. Nilidhani picha ya photoshop kwa kweli.
Ndungai una kazi kubwa. Hawa wanaachwa kuichangia bajeti ya nchi, wenye mawazo wanafanyiwa fitna watoke wawapishe hao. Nchi yangu ina kazi
 
Huyu msukuma ni mbunge anawakilisha chama gani? Kuna taarifa nimepata kuwa ni mbunge wa ccm; kama ni hivyo basi JPM na chama chake wana kazi kubwa kuhakikisha kuwa nchi yetu inakuwa na wabunge wenye hadhi na uwezo, na hili kulifanikisha over the long term ni lazima ccm ianzie na uchaguzi wa wabunge watakaowakilisha nchi kwenye bunge la Afrika Mashariki. Safari hii ni lazima nchi kupitia vyama vya siasa vijaribu kuteua wawakilishi wenye hadhi na uwezo watakaoendana na heshima ya nchi badala ya kuchagua watu kwa kufuata urafiki na majina lakini hawala uwezo, matokeo yake ni kuitia nchi aibu kwa tabia chafu na michango katika mijadala iliyo duni!!!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom