Video: Azam TV tunzeni heshima yenu, hivi ni vitasa feki

njaakalihatari

JF-Expert Member
Feb 12, 2019
4,084
8,663
Kwanza hongereni sana kwa kuleta revolution ya tv hapa bongo. Soka mmefanikiwa, bongo movies pia naona mnakomaa na ndondi pia mmeamua kutuletea.

Ila dah ndugu zangu kilichotokea Dodoma kwa Dulla Mbabe ni uhuni. Ni kama vile mnashirikiana na matapeli kuokota walevi mnawaleta hapa waje wapigane wachukue hela tu!

Yaani mwezi mzima mna-hype pambano bila hata kuangalia backgrounds za hao wapiganaji. Kweli Mwakinyo alikuwa sahihi alivyosema kuna watu wanapigana na walevi toka nje ya nchi.

Hebu angalia knockout ya Dullah Mbabe, ngumi ya bega moja tu mkenya chali keshachukua hela yake.

 
Azam kwenye ndondi wanatuibia tu
Hii ya leo imezidi hadi watangazaji wa azam wenyewe wameikataa hadi Dulla Mbabe anaona aibu anakazania kapiga ngumi nne mtangazaji anauliza hata ngumi umepigwa kweli?

Aiseeee kwa mwendo huu watu wataacha kwenda sasa bora kusubiria yanayoandaliwa na Kevin Twissa Jackson Group naona wana muelekeo
 
Jamani nipeni connection na mimi nikavute kilaini hela ya Azam
Nenda chama cha ngumi jiandikishe kama promota tafuta bondia kwa mfano mfaume mfaume vs wa nje so nenda kwa mfano malawi katafute msukuma mkokoteni njoo azam waambie una pambano, bOOOM PROMO YA KUTOSHA unavuta mkwanja wako ukiwa mjanja na sponsors unawaokota pia
 
nenda chama cha ngumi jiandikishe kama promota tafuta bondia kwa mfano mfaume mfaume vs wa nje so nenda kwa mfano malawi katafute msukuma mkokoteni njoo azam waambie una pambano,bOOOM PROMO YA KUTOSHA unavuta mkwanja wako ukiwa mjanja na sponsors unawaokota pia
Bonge la business idea.
Pia nadhani naweza kuanzisha ligi ya ngumi.😂🤣😅
 
Naona mnaongea kwa hisia lakini hamjui mchezo wa ngumi
Nakubaliana na wewe kabisa.

Nashangaa hata wale wachambuzi ambao nao ni maboksa kabisa wameshindwa kuona ngumi 2 za haraka mwanzo ambazo moja ya kulia ilimpata kwy kidevu, ya pili ilipiga juu kichwani.

Kwa kawaida kama bondia yuko vizuri, hizo punch 2 zinakata kabisa stim, sema mkenya ni mzoefu na mgumu ndio maana aliendelea kuguard....

Uzito wa ngumi ya 4 ambayo jamaa alidondoka ni sababu jamaa aliisha lewa...lakini pia angalia ilivyo mrusha japo aliiguard...mkenya yuko sahihi alipima ule uzito na hali yake ya kurecover akaona akirudi hata kuwa na guard ya kuhimili bora ajiokoe

Mie naona Dulla kashinda kwa uwezo wake mkubwa na Mkenya kama alivyosema kuna kesho hakuona sababu ya kwenda kwy matibabu makubwa endapo angeendelea maana angeweza kupigwa knockout kali sana
 
Kabla ya ile ya bega Mkenya alipokea za uzani mbili tatu za fasta ila yote kwa yote hakuwa bondia mzuri ,Kongole kwa Dula Mbabe .
 
Kwanza hongereni sana kwa kuleta revolution ya tv hapa bongo. Soka mmefanikiwa, bongo movies pia naona mnakomaa na ndondi pia mmeamua kutuletea.

Ila dah ndugu zangu kilichotokea Dodoma kwa Dulla Mbabe ni uhuni. Ni kama vile mnashirikiana na matapeli kuokota walevi mnawaleta hapa waje wapigane wachukue hela tu!

Yaani mwezi mzima mna-hype pambano bila hata kuangalia backgrounds za hao wapiganaji. Kweli Mwakinyo alikuwa sahihi alivyosema kuna watu wanapigana na walevi toka nje ya nchi.

Hebu angalia knockout ya Dullah Mbabe, ngumi ya bega moja tu mkenya chali keshachukua hela yake.

Ndio tabia za Wakenya kufanya utapeli au wizi. Kimsingi yule Mkenya hakuwa tayari kupigana. Alipohojiwa akawa anasema kuanzia asubuhi mwili wake haukuwa vizuri.
 
Hebu waende wakapigane nje kwanza tumechoka na maigizo yao yaani mchezo ukianza 100% unajua mbongo atashinda hivi huku mhindi hayupo tumpige hela kiurahisi?
 
Mim tangu niangalie lile pambano la twaha kiduku na yule Thailand (sijui) nikaona jamaa mweupe analeta ukatuni ulingoni sijakaa niangalie tena huu upumbavu
 
Toka nianze kufatilia Haya mapambano kwa tv ya azam,IBRA class ndo bondia pekee ambae alikuwa na mshindani wa kweli hao wengine sijui wakina Mwakinyo,kiduku huwa wanaletewa mabondia wakawaida sana
 
Back
Top Bottom