Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,567
Wanabodi,
Siku Wabunge wa Bunge hili walipokuwa wanaapishwa mjini Dodoma, nilikuwepo, na nilipandisha uzi Huu ambapo kuhusu wabunge wa viti maalum, nilisema hivi!.
Kwa muda wote wa uhai wa bunge hili, lazima tukubali, tukatae, baadhi ya waheshimiwa wabunge wetu wa viti maalum, hawajaweza ku deliver anything worthwhile of substance Kipindi chao chote cha kuwa bungeni, hivyo naweza kuwa right, niliposema, baadhi yao, wako pale kwa kutimiza tuu huduma za kijamii za kibinaadamu!.
Miongoni mwa wabunge hawa wa viti maalum, ambao mimi niliwahesabu kama wapo wapo bungeni kutimiza mahitaji ya huduma za kijamii za kibinaadamu, ni Mhe. Vicky Kamata, kwa jinsi ilivyo Mrembo vile na Mungu amempendelea na kujaaliwa, nilimdhania mchango wake mkubwa mule bungeni ni pambo la bunge kwa kuvaa vizuri, na kupendezea kwa sana vikiwemo vikuku vya miguu yote miwili kuashiria anacheza kote kote kiasi kwanza uwepo wake, unasaidia kupunguza stress za wabunge kwa kiwango kikubwa na kwa wale wazee wasinziaji, kuwa hamasisha wasisinzie!, lakini kiukweli leo ndio nimemsikia na kumfahamu vuzuri kuliko nilivyomdhania!.
Kikubwa alichokifanya leo, ni kusimama kidete, kumvaa Zungu, uso kwa uso kumpinga kuliendesha bunge, kibabe, kwa ubaguzi, kwa uonevu na kwa double standards za hali ya juu, na kuamua kuliko kunyanyaswa, ni bora ajikalie kimya kuliko kuburuzwa!.
Hali ilikuwa hivi.
Jana Mhe. Kamata, alipeleka jina lake kuwa ni miongoni mwa wabunge, watakaochangia leo.
Leo akaangalia majina yaliyopitishwa kuchangia akajikuta yupo, muda wa kawaida kuchangia kwa mujibu wa kanuni ni dakika 10 kila mbunge. Mwenyekiti wa Bunge kikao cha leo, ni Mhe. Iddi Azan.
Uliopofika muda wake wa kuchangia, akashanga kujikuta jina lake limerukwa, na badala yake akaitwa Mhe. Hamad Rashid, ambaye jina lake kwenye walioomba kuchangia leo, halikuwepo, hivyo Mhe. Zungu, amemchomekea tuu.
Baada ya Hamad Rashid kumaliza, ndipo Vicky akaitwa na kupewa muda wa dakika 5 tuu, kuchangia!, hapa sasa ndipo nikapata fursa ya kumjua Vicky Kamata wa ukweli!, alimgomea Zungu kuwa iweje yeye, ambaye ni mchangiaji halali aliyepeleka jina toka jana, apewe dakika 5, wakati wachangiaji ambao majina yao hayapo, wamefanya kuchomekewa tuu, wapewe dakika kumi?!, Vicky akaomba apewe dakika zeke 10!. Zungu akamgomea kuwa muda umeisha, hizo dakika tano alizompa ni kumhurumia tuu ili angalau achangie, vinginevyo asubiri kuchangia kikao kijacho!. Vicky akamgomea, Zungu akamuamuru akae chini, na kumuita mchangiaji anayefuata ambaye ni Mhe. Magret Mkanga, kabla Mkanga hajaanza kuchangia, Vicky akawasha kipaza sauti na kuuliza kwa sauti ya ukali na very authoritative, Mkanga anachangia kwa dakika ngapi?!. Zungu akamjibu anyamaze, ndipo Vicky akasimama na kuwasha kipaza sauti kuongea, Zungu nae akasimama, kikanuni, Mwenyekiti akisimama, mbunge husika anapaswa kukaa chini, Viky akagoma kukaa!, ndipo Zungu akamuamuru akae chini, Vicky akamjibu kwa ukali kuwa sikai chini, sikubali, huu ni uonevu, kwa nini uchomekee wengine wachangie dakika 10, sisi wengine ndio tupewe dakika 5, na ulipomuita Mkango hukusema umempa dakika ngapi, huu ni uonevu, haiwezekani!.
Ndipo Zungu akamuamuru tena kukaa chini, na kumuamuru kama ana malalamiko yoyote, amuandikie spika malalamiko yake!, yeye anaendesha bunge kwa mujibu wa kanuni, na wote aliowaita, ameletewa majina. Ndipo Vicky akaa na kikae kikaendelea kwa waliobaki kuchangia kwa dakika tano tano!.
My Take.
Nchi yetu tumefikishwa hapa tulipo kwa sababu ya kukubali kuburuzwa, na kukosekana moyo wa udhubutu kusema hapana!, hata wakati mambo yanakwenda ndivyo sivyo, sisi na viongozi wetu, na wabunge wetu kazi yatu ni kusema tuu yes!, hewala!. Kitendo cha Vicky Kamata kusema no, alipoona mambo yanakwenda ndivyo sivyo, huu ndio ndio uthubutu, unaotakiwa sasa kulikomboa taifa hili na sio kupelekwa pelekwa tuu kama ling'ombe!.
Hongera Sana Vicky Kamata!.
Big Up!.
Pia Hongera kubarikiwa!.
Thanks.
Paskali