Kilimanjaro moja
Member
- Nov 30, 2012
- 67
- 33
MBUNGE wa Musoma Mjini, Vicent Nyerere (CHADEMA), ameanza ziara ya kuimarisha chama chake mkoani Geita, huku akimpiga kijembe Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kuwa anawachosha bure mawaziri kwa kuwalazimisha kufanya ziara mikoani kuzungumza na wananchi.
Nyerere ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, alisema kuwa mkakati huo hauwezi kuinusuru CCM kwani mawaziri na sekretariati nzima ya CCM hawana majibu ya maswali ya kero za wananchi.
Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara jana mjini Kasamwa, Nyerere alitamba kuwa kichwa chake kimoja ni sawa na sekretarieti nzima ya CCM na mawaziri waliopita katika baadhi ya mikoa kusafisha hali ya hewa ili chama chao kisife.
Nyerere alifafanua kuwa, mkakati huo wa CCM ni sawa na kulamba matapishi yao, kwani mawaziri hao hao ndio wameshindwa kutekeleza vema shughuli za maendeleo kwa Watanzania, badala yake wamegeuka kunyonya rasilimali za taifa.
"Wanapobandua CCM na mawaziri wao, mimi nabandika hapo, watu hawahitaji ziara za akina Abdulrahman Kinana, Nape Nnauye na mawaziri, wao wanataka majibu kwa serikali kwamba kwanini baada ya kuwaondoa mawaziri wabovu madarakani wameshindwa kuwashtaki.
"Hawa walioenguliwa ndio walizembea wakati twiga wetu wanasafirishwa nje ya nchi, kashfa ya rada imetokea kwao na madudu mengine mengi, sasa leo wanapokuja kwa wananchi hawana majibu ya hatua gani zilichukuliwa, ziara hizo ni bure tu za kuwachosha," alisema.
Nyerere ambaye alikuwa meneja kampeni wa Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (CHADEMA) kwenye uchaguzi mdogo na kutoana jasho na Rais mstaafu Benjamin Mkapa, alisema kitendo cha CCM kuwalazimisha mawaziri kutembea nao kwenye mikutano ya hadhara, kamwe hakiwezi kubadili mawazo, mtazamo na mwelekeo wa Watanzania.
Alisema ni lazima wataiweka madarakani CHADEMA ifikapo mwaka 2015, kwani wamechoshwa na ahadi hewa za Serikali ya CCM chini ya Rais Kikwete.
"Kwa CCM hawana jipya tena. Huo mkakati wao wa kutembea na mawaziri majukwaani hauwezi kukinusuru chama hiki tawala kufa. Ni Mtanzania yupi ambaye hadi leo hajui kwamba ugumu wa maisha hivi sasa unatokana na utendaji mbovu wa serikali hiyo wakiwemo mawaziri wake hao?" alihoji.
Alisema wananchi sasa wanataka CCM na Rais Kikwete wawaeleze ni kwanini wameshindwa kuwachukulia hatua za kisheria mawaziri waliozembea na kuisababishia hasara kubwa serikali kwa kununua ndege na rada mbovu, kupeleka wanyama nje na kusaini mikataba mibovu.
Katika ziara hiyo, Nyerere aliyeongozana na viongozi mbalimbali wa CHADEMA, akiwemo aliyekuwa mwenyekiti wa CCM wilayani Geita, ambaye mwishoni mwa wiki alijiengua huko, Daud Ntinonu, alihoji pia sababu za CCM kupangua makatibu wakuu kila mara.
"Hata wabadili viongozi mara ngapi, kamwe hawawezi tena kuungwa mkono na Watanzania, wananchi wa leo wanahitaji mabadiliko ya kweli ya kimaendeleo, ambayo yatakwenda kutekelezwa na CHADEMA mwaka 2015," alisema.
Katika kile alichodai ni hali ngumu, Nyerere alidai kuwa kama baba mdogo wake hayati Mwalimu Julius Nyerere, angefufuka na kuiona hali hii sasa, asingeweza kukaa hata dakika moja bila kufa tena.
Huku akishangiliwa na umati mkubwa wa wananchi, Nyerere aliwahakikishia Watanzania kwamba, baada ya Mwalimu Nyerere kufariki mwaka 1999, CCM imetelekeza rasmi mawazo na sera za kiongozi huyo aliyekuwa adui namba moja wa rushwa na uchu wa madaraka.
Nyerere ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, alisema kuwa mkakati huo hauwezi kuinusuru CCM kwani mawaziri na sekretariati nzima ya CCM hawana majibu ya maswali ya kero za wananchi.
Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara jana mjini Kasamwa, Nyerere alitamba kuwa kichwa chake kimoja ni sawa na sekretarieti nzima ya CCM na mawaziri waliopita katika baadhi ya mikoa kusafisha hali ya hewa ili chama chao kisife.
Nyerere alifafanua kuwa, mkakati huo wa CCM ni sawa na kulamba matapishi yao, kwani mawaziri hao hao ndio wameshindwa kutekeleza vema shughuli za maendeleo kwa Watanzania, badala yake wamegeuka kunyonya rasilimali za taifa.
"Wanapobandua CCM na mawaziri wao, mimi nabandika hapo, watu hawahitaji ziara za akina Abdulrahman Kinana, Nape Nnauye na mawaziri, wao wanataka majibu kwa serikali kwamba kwanini baada ya kuwaondoa mawaziri wabovu madarakani wameshindwa kuwashtaki.
"Hawa walioenguliwa ndio walizembea wakati twiga wetu wanasafirishwa nje ya nchi, kashfa ya rada imetokea kwao na madudu mengine mengi, sasa leo wanapokuja kwa wananchi hawana majibu ya hatua gani zilichukuliwa, ziara hizo ni bure tu za kuwachosha," alisema.
Nyerere ambaye alikuwa meneja kampeni wa Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari (CHADEMA) kwenye uchaguzi mdogo na kutoana jasho na Rais mstaafu Benjamin Mkapa, alisema kitendo cha CCM kuwalazimisha mawaziri kutembea nao kwenye mikutano ya hadhara, kamwe hakiwezi kubadili mawazo, mtazamo na mwelekeo wa Watanzania.
Alisema ni lazima wataiweka madarakani CHADEMA ifikapo mwaka 2015, kwani wamechoshwa na ahadi hewa za Serikali ya CCM chini ya Rais Kikwete.
"Kwa CCM hawana jipya tena. Huo mkakati wao wa kutembea na mawaziri majukwaani hauwezi kukinusuru chama hiki tawala kufa. Ni Mtanzania yupi ambaye hadi leo hajui kwamba ugumu wa maisha hivi sasa unatokana na utendaji mbovu wa serikali hiyo wakiwemo mawaziri wake hao?" alihoji.
Alisema wananchi sasa wanataka CCM na Rais Kikwete wawaeleze ni kwanini wameshindwa kuwachukulia hatua za kisheria mawaziri waliozembea na kuisababishia hasara kubwa serikali kwa kununua ndege na rada mbovu, kupeleka wanyama nje na kusaini mikataba mibovu.
Katika ziara hiyo, Nyerere aliyeongozana na viongozi mbalimbali wa CHADEMA, akiwemo aliyekuwa mwenyekiti wa CCM wilayani Geita, ambaye mwishoni mwa wiki alijiengua huko, Daud Ntinonu, alihoji pia sababu za CCM kupangua makatibu wakuu kila mara.
"Hata wabadili viongozi mara ngapi, kamwe hawawezi tena kuungwa mkono na Watanzania, wananchi wa leo wanahitaji mabadiliko ya kweli ya kimaendeleo, ambayo yatakwenda kutekelezwa na CHADEMA mwaka 2015," alisema.
Katika kile alichodai ni hali ngumu, Nyerere alidai kuwa kama baba mdogo wake hayati Mwalimu Julius Nyerere, angefufuka na kuiona hali hii sasa, asingeweza kukaa hata dakika moja bila kufa tena.
Huku akishangiliwa na umati mkubwa wa wananchi, Nyerere aliwahakikishia Watanzania kwamba, baada ya Mwalimu Nyerere kufariki mwaka 1999, CCM imetelekeza rasmi mawazo na sera za kiongozi huyo aliyekuwa adui namba moja wa rushwa na uchu wa madaraka.