Vibaraka wa Nyalandu waliopindua maamuzi ya serikali kukata rufaa

hugochavez

JF-Expert Member
Mar 1, 2013
1,907
1,009
Taarifa za uhakika zilizopatikana kutoka ndani ya kambi haramu ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Singida ya kupindisha maamuzi yaliyofanyika miaka mingi iliyopita kuwa makao makuu yajengwe katika kijiji cha Ilongero wao wakayapeleka kwenye hifadhi ya msitu wa Sagarumba, hatimaye jana mkuu wa mkoa wa singida eng.Mtigumwe kubatilisha maamuzi hayo ya kijuha na kuyarudisha Ilongero.....

Mwenyekiti huyo ambaye elimu yake ni darasa la saba hivi sasa anahaha kutaka kupinga maamuzi ya mkoa eti akate rufaa kwa rais kuwa amedharauliwa..anasahau kuwa yeye alipindua maamuzi halali ya mwaka 2006 na kilichokuwa kinasubiriwa ni kuhamia tu.

nyuma ya mwenyekiti huyo ambaye hana elimu wapo wapambe wake mwenyekiti wa CCM wa wilaya Narumba Hanje, mhandisi Ikungu nk ambao wamehodhi maeneo makubwa jirani na eneo la sagarumba hivyo wanajiona wamepokwa tonge mdomoni.

mkuu wa mkoa wananchi tupo nyuma yako, usitetereke. hao ni waganga njaa.
 
Mbona kwenye bandiko sioni ukibaraka wa huyo jamaa na Nyalandu?.
huyu ELIA DIGHA ni msaidizi wa mbunge nyalandu kwa miongo miwili sasa. kituko ni kwamba, nyalandu alivyoona joto limefika shingoni akawaruka vibaraka wake akaungana na wananchi, akaungana na mkuu wa mkoa na chama mkoa, sasa huyu elia digha ndio anaruka ruka kama kuku aliyekatwa shingo.
 
Ilongera ndio center,yafaa kuwa makao makuu
Lakini kwa kuwa umeshindwa kuonesha ukibaraka wa Nyalandu,tuambie wewe ni kibaraka wa nani?
 
Fafanua Nyalandu anaingiaje mkuu?
anaingia kama mbunge wa jimbo la singida kaskazini aliyesimamia ubakaji wa demokrasia na haki ya wanasingida, alipoona kimenuka akastuka gafla, akajirudi.
 
Ilongera ndio center,yafaa kuwa makao makuu
Lakini kwa kuwa umeshindwa kuonesha ukibaraka wa Nyalandu,tuambie wewe ni kibaraka wa nani?
nimeonyesha hapo chini mkuu, hatan hivyo mimi ni kibaraka wa wananchi
 
Lazaro Nyalandu.. Mtuhumiwa wa ufadhili wa ujangili wa wanyama pori katika hifadhi za Taifa za wanyama pori.
 
Chadema wanatakiwa wajiangalie vizuri sera zao lasivyo wanatuchangaya wananchi
 
Back
Top Bottom