mtaa umetulea
JF-Expert Member
- Nov 17, 2020
- 1,719
- 2,164
Ni uonevu tu
WEWE NI MACHINGA HUNA LOLOTE.Inahitaji jicho la tatu kuliona hili.
Kwanini nchi imejaa wamachinga wengi kuliko wanaofanya biashara rasmi madukani?!
Ukiishajibu hilo,twende kwenye conclusion,je Tanzania ni nchi yenye wamachinga zaidi au wafanyabiashara rasmi zaidi?
Je,tunataka nchi ya wamachinga au wafanyabiashara rasmi?
Tuna mikakati gani kutomuua au kutompoteza mmachinga na badala yake kumgeuza kuwa mfanyabiashara rasmi?!
Kiwango cha elimu,maarifa,mipango ya maendeleo ya jamii na uchumi katika taifa hili na utekelezaji wake kinatengeneza workforce ya aina gani,skilled au unskilled?!
Aina hiyo ya workforce ina mchango gani kutengeneza machinga au mfanyabiashara rasmi?!
Tuna workforce ya aina gani sasa(majority),tunataka workforce ya aina gani baadae na tunaipataje bila kuathiri uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja?!(smooth transition)?
Haya ni mambo ya kuzingatia.
Tusiingize migambo mitaani na kujifanya sisi ni wamarekani tuliosheheni mabilionea watakaoweza kuinvest,tukavunjavunja ALL THAT WE HAVE tukijivunia kuleta kitu ambacho ni priviledge kwa mhindi,mnaijeria,mkenya,mzungu etc na wale unawaona kero kumbe ndio workforce yako pekee uliyo nayo ambayo unapaswa kuilea kama yai.
Tukifukuza machinga,je,hawa machinga kuna siku tutawakuta wanamiliki maduka wao,au watanzania wenzao?!au tutakutana na wageni wakimiliki njia za uchumi za nchi?!
Suala la machinga ni pana na kiashiria cha tatizo kubwa la nchi kuliko tunavyowaza short sighted.
Tuweke siasa za magufuli-Samia,ccm-chadema kando,tusiwe blinded na ego.
Tuwaze kama watanzania,ni kama mzazi mwenye mtoto mtukutu nyumbani,jambo la kwanza unawaza kumbadili awe mwema,na sio kumtimua.
Tusizungumze kama tunaongelea aliens from another country,planet etc.
Tunazungumzia vijana wa kitanzania,wanaotumia nafasi finyu ya uwekezaji kujikwamua kiuchumi.
Tunazungumzia baba na mama wa wale watoto unaokutana nao kituoni wamevaa uniforms wanakwenda shule!
Angalia upande wa pili wa shilingi.Huko ndiko nchi iliko,ndiko vijana wenu wengi waliko,ni machinga barabarani,machinga maofisini.
Ubinafsi usikufanye uwe blind.
Nina biashara zangu rasmi nalipa kodi nyingi za serikali hapa mjini,na sijawahi kumchukia machinga asiye na duka kama mimi hata siku moja.It pains me kuona mnazungumzia mambo ya kutimua binadamu anayejitafutia riziki kirahisi tu!Yaani mnaona rahisi tu mambo haya ya uwekezaji na uchumi mtu kahangaika wee hadi kaweka banda lake,timua hao!You guys?!
I expect mtandao kama huu uwe na mawazo critical zaidi,yasiyopatikana kirahisi.
Wajengeeni maeneo yao,warasimisheni kazi zao,wapeni financial support,waelimisheni watanzania waweze kuwa competitive na mataifa mengine then watahama tu bila vurugu kuja mnakokutaka.
Wekeni na simamieni mipango miji kila mtu anayetaka kufanya lolote ajue anafanyia wapi na vipi,na taratibu zikoje,na ziwe condusive kwake,sio alimradi tu.
rejea enzi za kikweteKiukweli hili suala ni gumu sana na halitekelezeki, kamwe halitakaa lifanikiwe, so kwangu hili naliona kama tamko tu la kawaida la kupima upepo.
Naonga mkono hoja nilienda Posta one day nikakuta vibanda vibaya sura havina at central business centre, kwa kweli haikua sawa kabisa.Gari la tangazo linapita kutangaza ya kuwa ifikapo tarehe 18 mwezi huu hakitakiwi kibanda chochote kuonekana kando kando ya barabara katika jiji la Dar es Salaam.
I second you mkuu. Nishaongea Sana hili hapa Jukwaani tangu kitambo. Lakin SIJUI ni kwanini hawatengewi maeneoSwala la machinga waondoke tu mjini wanaua biashara watengewe maeneo yao Magufuli alibugi sana
Kwanza hawalipi kodi na wanaponunua bidhaa hawaombi risiti kwenye maduka makubwa so serikali inapata hasara ya kodi.
Vile vile wengi mjini ni wafanya biashara wakubwa wanafanya kutoa pesa kwenye mfuko wa suluali na kuweka kwenye mfuko wa shati.
Ndio maana ukwepaji kodi unaongezeka kwa sababu watu wenye address za kulipa kodi biashara zao wanachukua machinga.
Halafu machinga wenyewe wanauza sana halafu hawana leseni za biashara za kufanyia kazi wengine unakuta ndio wale waliofunga maduka kipindi cha Magufuli unakuta machinga ameweka bidhaa za milio 10 nje hii sio haki hata kidogo.
Watafutiwe maeneo maalumu kama Tandika tegeta, Ubungo mbagala wawe na shopping mail zao na walipe kodi ili tuone kama watauza tens bidhaa ovyo na kuhatarisha hata maisha ya wanunuzi.
Unakuta mtu anauza nyanya kariakoo katikati ya barabara seriously sehemu ambayo mnasema ni soko la kimataifa.?
Magufuli ni marehemu kwa sasa. Mimi na wewe ni marehemu watarajiwa. Punguza machungu ya nafsi yataishia kukuumiza na kukupatia maradhi.Magufuli ameiharibu nchii hii. Wamlaumu Magufuli kwa kuwaelekeza kuvunja Sheria. Wamguate huko wamkabe makofi
Pale kariakoo kuna majengo yanayotaka kuendana na unayoyasemea hapa,ila wanadai kule juu hamna biashara,wateja awapandi!,kikubwa serikali iandae maeneo ya machinga nje ya mji,soon pale mbezi kutakua kama kulivyokua mbagala mwisho na tandika,jamaa wangetafutiwa eneo mapema sanaHIVI MSAJILI HAWAWEZI KU SCARIFY MAGOROFA MATATU TU KARIAKOO YALIYOFUATANA IKATENGENEZWA MALL KUBWA KWELI YA GHOROFA 10 IKAJENGWA KWA UFUNDI NA RAMANI YA AINA YAKE IKABEBA MACHINGA 10,000 WALIOPO KARIAKOO SEREKALI IKAWA INAPATA KODI YAKE KWA WEPESI?,MAANA MACHINGA WAMEIKOMALIA SANA KARIAKOO NA KUWAFUKUZA WAKATI MWINGINE SIO HAKI,PIA KUWAHAMISHA INAKUWA NGUMU,KARUME PABAKIE,ILALA,PABAKIE,MACHINGA COMPLEX ISANIFIWE IBADILISHWE ILI YAWE MAKAZI NA FIDIA KWA MAJENGO MATATU WATAKAYOWAPA JIJI KATIKA UJENZI WA MALL.
*Ground zero ikawa Parkings
*1&2floor ikawa nguo za mitumba
*3&4floor ikawa wauza vyombo
*5&6floor electronics goods
*7&8floor ikawa viatu of varieties
*9 floor restaurants
*10floor mixtures small items.
Kuna mpumbavu kasema watahamishiwa chato.Hao wanaotolewa maeneo hayo wanatarajiwa kuhamishiwa wapi?. Mtihani mpya kwa wale waliochukua mikopo haswa kina mama wanaotegemea vikoba na pesa za aina hiyo.