Viatu vya mchuchumio vinavyowatesa wanawake…..!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,806
15,379
high+heel.jpg


Viatu vya kisigino kirefu au mchuchumio vimekuwa ni maarufu sana siku hizi, karibu kila mwanamke anavutiwa na aina hiyo ya viatu, awe ni mwembamba au mnene, mrefu au mfupi wote wanavutiwa na viatu hivyo. Lakini wale wanawake wafupi ndio zaidi, hupenda aina hiyo ya viatu ili kuonekana ni warefu, ufupi umekuwa kero kwao, ajabu eh…!

Lakini kwa bahati mbaya uvaaji wa viatu vya mchuchumio huwa unawasumbua sana wanawake wengi, sio tu kuwasumbua, bali hutokea kutembea vibaya kiasi cha kuwafanya kuwa kichekesho na hata ule uzuri walioutarajia unakuwa haupo. Kwa hiyo mwanamke anakuwa kituko badala ya kupendeza.

Tafiti mbalimbali zimebainisha kwamba, viatu hivi vimewahi kuwaumiza sana wavaaji na hata kuwauwa pia. Pamoja na kuumia au kufa, kuna kuingia katika aibu kwa kushindwa kutembea vizuri na kugeuka kituko.

Inashauriwa kwamba ni vyema wanawake wanaopenda kuvaa viatu hivyo wafanye mazoezi ndani kabla hawajaanza kuvaa viatu hivyo vya mchuchumio hadharani. Kwa kufanya mazoezi kutawaepusha na ajali au fedheha watakapokuwa wanatembea barabarani……….

Ujumbe huu uwafikie wafuatao:
cacico, gfsonwin, snowhite, lara 1, Lisa, Ciello, charminglady, nivea, FirstLady, sweetlady, AshaDii, King'asti, @FP, Preta, marejesho, Madame B, na wanyange wengine watumiao aina hiyo ya viatu..............

 
hayo uliyoyasema yapo sana na madhara yake ni makubwa mno, watu hawajui tu......
mimi huwa navaa viatu virefu kwenye hafla ambayo najua sitakuwa na mizunguko mingi. na kama kwenye sehemu ambayo nitakuwa na mizunguko sana na ni lazima nivae viatu virefu sababu ya nguo ambayo nimevaa basi nitavaa viatu ambavyo vipo comfortable sana, kiasi kwamba hata naweza kukimbia navyo......
pamoja na hayo madhara uliyoyasema, hivi viatu huwa vinaumiza sana migongo ya wamama hapo baadae
 
Huyu nime mtamani kweli ili anapatikana wapi? Ndio mambo ya fashion mzee wangu, ila tatizo watumiaji hawjijui aina ya vitu vya kuvaaa

Mimi wakati mwingine huw anacheka sana huko barabarani, ukiwaona dada zetu kwenye mitoko jinsi wanavyotembea utadhani bata...
Yaani mpaka unajiuliza, 'kavalishwa...!'

Najua ni mambo ya fasion, lakini fasion si kuvaa tu, bali pia na kumiliki kile unachokivaa sio kikumiliki wewe..........!
 
Mtambuzi,

Kiatu hufanya nguo uliyovaa ishuke thamani ama ionekane ya thamani zaidi. Na kiatu pia huchukuliwa kawaida na watu wengi but viatu iwe kwa mwanamke ama mwanaume huongea lugha yake ya kipekee kabisa. Huwezi vaa viatu virefu kila mahala, ila bana mahala ambapo kiatu kirefu kinatakiwa ni kujikaza kwenda mbele but unakufa navyo hadi huko unakoenda kieleweke. Hiyo picha umeweka hapo, pamoja na uzuri wote na figure iliyo Perfect, kiatu kimecheza nafasi ya yeye kuwa more hot..

Mahala kama mtoko mkubwa wa usiku, Mkutano hasa hii ya Co-operate world, na sherehe mbali mbali hasa hizi za Cocktail ni lazima utokelezee na kiatu kirefu. Umuhimu huu ndio hasa unaeleza why akina dada/mama siku hizi wanatembea na viatu pair mbili, flat (sandals) na heels, akitoka tu nje ya mahala husika anaweka mbadala. Kiatu kirefu makes akina dada aonekane sexy and extra hot pia hata kuwa upo sophisticated Siku moja nikipata nafasi nitatoa viatu vya kike na kiume vya aina mbali mbali hutoa ujumbe gani kuhsu mhusika... Lol.
 
Mimi na huu ungongoti nilionao nikivaa viatu virefu nakuwa kama jini..!

Viatu hivyo huwa navivaaa pale tuu inapobidi..!

Ila ni kweli huwa vinanikong'oli sana viatu vya mchuchumio..!!
 
Bora sisi wanaume hatuvai, maana akina sisi tuna matege, viatu soli zinalala 45 degree na daladala zetu kupata siti labda uwahi ya dereva. yaani Mtambuzi 'Mzee wa kalma' sipati picha ingekuaje? lol.
 
Ninaelewa mimi, mchuchumio humfanya mwanamke aonekane sexy na k-lady zaidi, hasa akitembea unless mtu hajazoea high heels.
 
Mtambuzi,

Kiatu hufanya nguo uliyovaa ishuke thamani ama ionekane ya thamani zaidi. Na kiatu pia huchukuliwa kawaida na watu wengi but viatu iwe kwa mwanamke ama mwanaume huongea lugha yake ya kipekee kabisa. Huwezi vaa viatu virefu kila mahala, ila bana mahala ambapo kiatu kirefu kinatakiwa ni kujikaza kwenda mbele but unakufa navyo hadi huko unakoenda kieleweke. Hiyo picha umeweka hapo, pamoja na uzuri wote na figure iliyo Perfect, kiatu kimecheza nafasi ya yeye kuwa more hot..

Mahala kama mtoko mkubwa wa usiku, Mkutano hasa hii ya Co-operate world, na sherehe mbali mbali hasa hizi za Cocktail ni lazima utokelezee na kiatu kirefu. Umuhimu huu ndio hasa unaeleza why akina dada/mama siku hizi wanatembea na viatu pair mbili, flat (sandals) na heels, akitoka tu nje ya mahala husika anaweka mbadala. Kiatu kirefu makes akina dada aonekane sexy and extra hot pia hata kuwa upo sophisticated Siku moja nikipata nafasi nitatoa viatu vya kike na kiume vya aina mbali mbali hutoa ujumbe gani kuhsu mhusika... Lol.

Heshima kwako Da AshaDii......

Ahsante kwa maoni yako mazuri, nadhani sasa ni wakati muafaka kwa Mods kuangalia uwezekano wa kuweka jukwaa la fashion ili members wapate kuelimishana humo kuhusu aina ya mavazi ya kuvaa na how to practice. jamani huko maofisini ninakopita, (msishangae mimi ni MACHINGA) nakutana na vituko kila uchao, hususan kwenye majengo marefu halafu ukute hakuna elevator siku hiyo utachoka jinsi wanyange wanavyoziparamia ngazi na hivyo viatu.........Ye uuuwi...!!!!!!!

Wengine mpaka wakifika juu, utawaonea huruma..................
 
Last edited by a moderator:
Halafu uwe na usafiri wa Tz 11 ikisaidiwa na treni ya mwakyembe mbona utakoma...ndio maan wanawake siku hizi tuna vigimbi
sasa rafiki mchuchumio kwenye treni unafanya nini tena? lol!
mimi huwa nashangaa wadada wanaosafiri na michuchumio, yaani natamani kuwaamkia, lol!
hivyo viatu vinapendeza sana ila sheshe lake nalo si mchezo
 

Similar Discussions

8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom