Uchaguzi 2020 Viapo vya mawakala

Kesho ndio siku ya kuapishwa mawakala wa vyama katika uchaguzi mkuu.

Tukumbuke kuwa wakala anaapa halafu anaondoka bila utambulisho wowote, yaani anaondoka kama mimi na wewe!

Eti wakala anaenda mikono mitupu kituo cha kupigia kura eti kujitambulisha kwa msimamizi wa uchaguzi ndio apewe barua ya uwakala?

Msimamizi wa uchaguzi atamtambuaje kama huyu ndiye yule aliyeapishwa?

Kwanza msimamizi wa uchaguzi atamuomba kitambulisho cha uraia au leseni ya udereva au pasi ya kusafiria ili atambue kuwa ni yeye -
1) Holaa, hana! anamkataa, anasema nitajuaje kama ni wewe! Mzozo unaanza! Anatolewa

2) Kama anavyo vitambulisho vitamulikwa kwa darubini kuhakikisha havitofautiana hata kidogo mpangilio wa majina au spelling ya jina. Kama kuna tofauti yoyote msimamizi anamkataa. Mzozo unaanza! Afande anapapasa AK47, wakala anatolewa!

Lengo la haya yote ni kuwachelewesha mawakala kuingia vituoni.

Simu zitapigwa weeee, mawakala wakija kukubalika ni baada ya masaa, hapo ujue kura bandia kibao zitakuwa zimeisha penyezwa.

Yaani CCM ni shiiiidaaaa!
Natabiri mzozo mkubwa mwanzo kabisa mwa kupiga kura.

TAHADHARI:

1). HAKIKISHA MWAKALA WANA VITAMBULISHO

2. HAKIKISHA MAJINA YA MAWAKALA MNAYOPELE KWA TUME YANAFANANA KWA MPANGILIO NA SPELLING KAMA VITAMBULISHO WALIVYONAVYO.

3). MAWAKALA MSIJESAHAU VITAMBULISHO VYENU IWE LESENI, PASPOTI, VYA NIDA, AU CHA KUPIGIA KURA, vinginevyo utatupiliwa mbali

Huo ni mtazamo wangu! We unasemaje!
Madhara ya vyama kutojiandaa ndiyo haya

Ufafanuzi huu ni kwa mujibu wa kifungu cha 57 (1) na (2) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, na kifungu cha 58 (1) na (2) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292

Chama cha siasa kinaruhusiwa baada ya kupata ridhaa ya Mgombea au Wagombea kuteua na kuwasilisha kwa Msimamizi wa Uchaguzi orodha ya majina ya mawakala wa upigaji kura siku saba (7) kabla ya siku ya uchaguzi

Ni vema mawakala wapangiwe vituo vya kupigia kura ndani ya kata wanayoishi ili waweze kuwatambua wapiga kura.

Kila chama cha siasa kitakuwa na wakala mmoja tu kwa kituo ambaye atawakilisha wagombea wa chama hicho kwa uchaguzi wa Rais, Mbunge na Diwani katika kituo husika

Utambulisho wa Mawakala wa Vyama Vya Siasa

Kwa mujibu wa kanuni ya 50 (6) ya Kanuni Uchaguzi wa Rais na Wabunge za mwaka 2020 na kanuni ya 43 (6) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani) za mwaka 2020, barua ya utambulisho wa kila wakala itakayowasilishwa na chama iainishe kituo alichopangiwa na iambatishwe na picha mbili (passport size) zilizopigwa si zaidi ya miezi mitatu.

Aidha, kwa mujibu wa kifungu 57 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 chama kitaruhusiwa kuteua wakala mbadala endapo aliyeteuliwa awali amefariki au ameshindwa kutekeleza majukumu ya uwakala. Katika kurahisisha utekelezaji wa suala hili, sambamba na orodha ya mawakala wa vituoni, vyama viwasilishe majina mawili ya mawakala wa ziada kwa kila kata ambao watatumika kama mawakala mbadala iwapo itahitajika

Endapo wakala hana picha anaweza kuwasilisha nakala mbili za mojawapo ya vitambulisho vifuatavyo: -

(i) Kadi ya mpiga kura;

(ii) Kitambulisho cha Taifa;

(iii) Leseni ya udereva; au

(iv) Pasi ya kusafiria. Baada ya Msimamizi wa Uchaguzi kupokea utambulisho wa mawakala atafanya yafuatayo: -

(i) Ataandaa orodha ya mawakala kwa kila kituo.
(ii) Ataikabidhi orodha hiyo kwa Wasimamizi wa vituo pamoja na barua ya utambulisho yenye picha wakati wa kugawa vifaa. Kama barua haina picha iambatishwe na moja ya nakala za vitambulisho vilivyotajwa hapo juu.
(iii) Atawaelekeza Wasimamizi wa Vituo kubandika orodha ya mawakala watakayopatiwa nje ya kituo cha kupigia kura kabla ya kuanza kwa zoezi la upigaji kura.
(iv) Atawaelekeza Wasimamizi wa Vituo wasiombe utambulisho mwingine wowote kutoka kwa mawakala wa vyama. Tume inashauri uteuzi wa mawakala uzingatie uwiano wa kijinsi na makundi maalum kama vile vijana na watu walemavu.

Hata hivyo, vyama vya siasa vina mamlaka kamili juu ya uamuzi wa kuteua mawakala kwa kadri watakavyoona inafaa.
 
Kanuni 63(2) ya Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa JMT inatamka bayana kuwa mawakala wa vyama vya siasa watapewa form ya matokeo ya uchaguzi vituoni (form namba 20) ‘iwapo kutakuwepo nakala za kutosha’.

Umeona shida ilipo mkuu? Kwa nini waseme iwapo kutakuwepo nakala za kutosha? Ni kipi hakijulikani ? Kwamba idadi ya vyama + idadi ya mawakala wanaohitajika * idadi ya jumla ya vituo haijulikani ?
..yani ndio unajiuliza wakati hii hujuma inafanywa sheria wabunge walikua hawaoni??na hii ilitakiwa iwe issue ya kampeni..kwamba wabunge wa ccm ndio wamepitisha sheria hizi za hujma .....sasa nakala zipungueje wakati tume imepewa pesa nyingi na serikali kwasababu ya uchaguzi??...hamna namna ya kukubali huu upuuzi....nakala hata kama mawakala watakua milioni lazima zitoshe...hela si zilitolewa kwa ajili ya kuandaa uchaguzi!
 
Kesho ndio siku ya kuapishwa mawakala wa vyama katika uchaguzi mkuu.

Tukumbuke kuwa wakala anaapa halafu anaondoka bila utambulisho wowote, yaani anaondoka kama mimi na wewe!

Eti wakala anaenda mikono mitupu kituo cha kupigia kura eti kujitambulisha kwa msimamizi wa uchaguzi ndio apewe barua ya uwakala?

Msimamizi wa uchaguzi atamtambuaje kama huyu ndiye yule aliyeapishwa?

Kwanza msimamizi wa uchaguzi atamuomba kitambulisho cha uraia au leseni ya udereva au pasi ya kusafiria ili atambue kuwa ni yeye -
1) Holaa, hana! anamkataa, anasema nitajuaje kama ni wewe! Mzozo unaanza! Anatolewa

2) Kama anavyo vitambulisho vitamulikwa kwa darubini kuhakikisha havitofautiana hata kidogo mpangilio wa majina au spelling ya jina. Kama kuna tofauti yoyote msimamizi anamkataa. Mzozo unaanza! Afande anapapasa AK47, wakala anatolewa!

Lengo la haya yote ni kuwachelewesha mawakala kuingia vituoni.

Simu zitapigwa weeee, mawakala wakija kukubalika ni baada ya masaa, hapo ujue kura bandia kibao zitakuwa zimeisha penyezwa.

Yaani CCM ni shiiiidaaaa!
Natabiri mzozo mkubwa mwanzo kabisa mwa kupiga kura.

TAHADHARI:

1). HAKIKISHA MWAKALA WANA VITAMBULISHO

2. HAKIKISHA MAJINA YA MAWAKALA MNAYOPELE KWA TUME YANAFANANA KWA MPANGILIO NA SPELLING KAMA VITAMBULISHO WALIVYONAVYO.

3). MAWAKALA MSIJESAHAU VITAMBULISHO VYENU IWE LESENI, PASPOTI, VYA NIDA, AU CHA KUPIGIA KURA, vinginevyo utatupiliwa mbali

Huo ni mtazamo wangu! We unasemaje!

Mtazamo wako Ni sahihi kabisa Ndugu Mtanzania. Uchaguzi huu ni wa kufa au kupona. Hilo angalizo lako linatakiwa lifanyiwe kazi upesi.
CHADEMA na ACT Wazalendo tafuteni Mawakala WAAMINIFU wenye IDs(NIDA, MPIGA KURA, PASSPORT, LESENI) zinazosomeka majina kikamilifu otherwise NEC NA WASIMAMIZI toka CCM(Wakurugenzi) wanakwenda kutumia hiyo kama loophole ya kuwa disqualify Mawakala wenu!!!!
 
Back
Top Bottom