Uchaguzi 2020 Viapo vya mawakala

Asante. Nakumbusha pia suala la wasimamizi kuwapangia mawakala vituo. Chadema viongozi hakikisheni mawakala wanapangwa mapema (sio last minute), maana watafanya figisu ya kumpanga wakala kituo cha mbali ambapo au atachelews au kushindwa kabisa kufika.
Kuwapangia vituo ni kazi ya vyama vyenyewe. Ndiyo maana vyama vinepewa orodha ya vituo vyote. Na kwa haki ya kawaida inatakiwa kila wakala atoke eneo husika ili pia aweze kupiga kura zote!
 
Kuna na ile ya mawakala wa vyama kutopewa nakala ya matokeo. Tume inasema watapewa kama zitakuwepo. Kiufupi yametengenezwa mazingira ya kuhujumu huu uchaguzi.
Hili tumeshalitolea ufafanuzi ni hivi msimamizi wa uchaguzi Kama hatokuwa na form ya nakala ya matokeo sisi tutachukua ya kwake kwa nguvu yeye akatafute anakokujua.
 
Wasiwasi wangu pia uko hapa, Hivi upinzani watapeleka wakala kila kituo?
Kama jibu ni yes basi pia nihatua moja mbele.
 
Kesho ndio siku ya kuapishwa mawakala wa vyama katika uchaguzi mkuu.

Tukumbuke kuwa wakala anaapa halafu anaondoka bila utambulisho wowote, yaani anaondoka kama mimi na wewe!

Eti wakala anaenda mikono mitupu kituo cha kupigia kura eti kujitambulisha kwa msimamizi wa uchaguzi ndio apewe barua ya uwakala?

Msimamizi wa uchaguzi atamtambuaje kama huyu ndiye yule aliyeapishwa?

Kwanza msimamizi wa uchaguzi atamuomba kitambulisho cha uraia au leseni ya udereva au pasi ya kusafiria ili atambue kuwa ni yeye -
1) Holaa, hana! anamkataa, anasema nitajuaje kama ni wewe! Mzozo unaanza! Anatolewa

2) Kama anavyo vitambulisho vitamulikwa kwa darubini kuhakikisha havitofautiana hata kidogo mpangilio wa majina au spelling ya jina. Kama kuna tofauti yoyote msimamizi anamkataa. Mzozo unaanza! Afande anapapasa AK47, wakala anatolewa!

Lengo la haya yote ni kuwachelewesha mawakala kuingia vituoni.

Simu zitapigwa weeee, mawakala wakija kukubalika ni baada ya masaa, hapo ujue kura bandia kibao zitakuwa zimeisha penyezwa.

Yaani CCM ni shiiiidaaaa!
Natabiri mzozo mkubwa mwanzo kabisa mwa kupiga kura.

TAHADHARI:

1). HAKIKISHA MWAKALA WANA VITAMBULISHO

2. HAKIKISHA MAJINA YA MAWAKALA MNAYOPELE KWA TUME YANAFANANA KWA MPANGILIO NA SPELLING KAMA VITAMBULISHO WALIVYONAVYO.

3). MAWAKALA MSIJESAHAU VITAMBULISHO VYENU IWE LESENI, PASPOTI, VYA NIDA, AU CHA KUPIGIA KURA, vinginevyo utatupiliwa mbali

Huo ni mtazamo wangu! We unasemaje!
Bali mawakala wa ccm hawataguswa
 
Na this time vyama hasa upinzani wawe makini na mawakala wao ikiwezekana watu wenye msimamo mkali maana mikakati inapangwa mingi,wakala usije kubali kusaini karatasi bila kujua jaman vijijin kura zinaibiwa sana wakala simamia haki hao wasimamizi wanaoletwa hao kuwa makini nao mikakati n mikali
 
Nyingine ni
1) wakala kukuta kabadilishiwa kituo. Chama kimempangia kituo A, tume inampeleka D ambako hamjui mtu yeyote!
2) Nakala ya matokeo. Vyama vilivyokuwa 15, orodha inaonyesha wa kwanza kabisa ni mgombea urais wa CCM, wa mwisho ni CHADEMA. Hiyo siyo bahati mbaya, ni mpango maalum. Ili copy ya mwisho ionekane inatakiwa mwandishi akazie kalamu kwa nguvu ya ajabu. Na wakati wa kuzigawa ataanza kusoma mtu wa CCM na anayepata copy ya mwisho ni CHADEMA. Ninamashaka kama itakuwa na maandishi yanayoonekana. Ni shiiiidaaaa!
 
Kukaa kimya ni nafuu ya mjinga. Ficha ujinga kwa kukaa kimya.
Wewe ndiye ulipaswa kukaa kimya ili kuficha ujinga wako.

Kwanza hicho chama chako hakiwezi kuweka wakala kila kituo nchi nzima; kama walishindwa kuweka wagombea udiwani kata mia mbili nchi nzima maana yake hawakuwa na mtu hata mmoja katika kata nzima wa kugombea udiwani. Sasa kila kata ina vituo si chini ya kumi na tano, ikiwa mtu moja wa kugombea alikosekana hawawezi kuwa na watu kumi na tano katika kata hiyo hiyo wa kuwa mawakala.

Pili hao mawakala hata mkiwapa posho ya kununua chakula sh 20,000 maana watashinda hadi usiku, mnahitaji bajeti isiyopungua sh bilioni tatu ambazo hamna.

Hoja mnazotoa ni kuficha aibu ya kutokuwa na uwezo wa kuweka mawakala.katika vituo vyote elfu 81.
 
Hii ndio mbinu pekee tuliyobakiwa Nayo sisi ccm, mbinu zetu zote zimegonga mwamba, mnajifanya kila tunalopanga mnategua. Sasa nawaambia ,tutafukuza mawakala wote vituoni , Ccm tumepania kuiba kura ili tuitangazie dunia tumeshinda kwa kishindo na tutafanya hivyo. Wakuu wa mikoa na wilaya wanapita kuomba huruma ya wasimamizi wa kata,ili lengo letu litimie oktoba 28, marafuku kumtangaza mpinzani.na atakaye mtangaza ajiandae kwa kukimbilia baada ya uchaguzi. Tumesema juu ya 81% kila kituo,kila kata,na kila jimbo.huwezi acha kazi yetu urudi majalalani tuliko kutoa
 
Kama ni hivyo na vingingi hivyo kwamba vina ukweli ndani yake, daaaah najisikia kuvunjika moyo.
Kwa ajili ya uchaguzi huru na wa haki tume huru ya uchaguzi inahitaji sana sana.
2021-2024 kiwe kipindi cha kupigania tume huru ya uchaguzi ipatikane.
 
Kesho ndio siku ya kuapishwa mawakala wa vyama katika uchaguzi mkuu.

Tukumbuke kuwa wakala anaapa halafu anaondoka bila utambulisho wowote, yaani anaondoka kama mimi na wewe!

Eti wakala anaenda mikono mitupu kituo cha kupigia kura eti kujitambulisha kwa msimamizi wa uchaguzi ndio apewe barua ya uwakala?

Msimamizi wa uchaguzi atamtambuaje kama huyu ndiye yule aliyeapishwa?

Kwanza msimamizi wa uchaguzi atamuomba kitambulisho cha uraia au leseni ya udereva au pasi ya kusafiria ili atambue kuwa ni yeye -
1) Holaa, hana! anamkataa, anasema nitajuaje kama ni wewe! Mzozo unaanza! Anatolewa

2) Kama anavyo vitambulisho vitamulikwa kwa darubini kuhakikisha havitofautiana hata kidogo mpangilio wa majina au spelling ya jina. Kama kuna tofauti yoyote msimamizi anamkataa. Mzozo unaanza! Afande anapapasa AK47, wakala anatolewa!

Lengo la haya yote ni kuwachelewesha mawakala kuingia vituoni.

Simu zitapigwa weeee, mawakala wakija kukubalika ni baada ya masaa, hapo ujue kura bandia kibao zitakuwa zimeisha penyezwa.

Yaani CCM ni shiiiidaaaa!
Natabiri mzozo mkubwa mwanzo kabisa mwa kupiga kura.

TAHADHARI:

1). HAKIKISHA MWAKALA WANA VITAMBULISHO

2. HAKIKISHA MAJINA YA MAWAKALA MNAYOPELE KWA TUME YANAFANANA KWA MPANGILIO NA SPELLING KAMA VITAMBULISHO WALIVYONAVYO.

3). MAWAKALA MSIJESAHAU VITAMBULISHO VYENU IWE LESENI, PASPOTI, VYA NIDA, AU CHA KUPIGIA KURA, vinginevyo utatupiliwa mbali

Huo ni mtazamo wangu! We unasemaje!
Kwani ukienda na NIDA, LESENI YA UDREVA watakujua kama wewe uliapa jana?

Mahera is an idiots, hajui chochote katika siasa
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom