Veta chang'ombe dsm

Electronian

Member
Sep 1, 2013
16
0
Kwa anae fahamu ada ya kozi ya udereva (DRIVING COURSE) Veta chang'ombe DSM
Naomba anambie ni bei gan kwa mwaka wa 2014.
 
Kuna udereva wa awali, udereva mahiri, udereva wa mabasi, udereva wa malori, sijui we unataka upi ..ila ada ni 150000 hadi 200000 inategemea na kozi unayotaka
 
udereva mahiri na awali ni aina gan ya udereva naomba unifahamishe.
ila kama mimi ambae cjaanza kozi yoyote je nitaweza kuanza kozi gan kati ya ulizo zitaja
 
kama ndo unaanza unapaswa kusoma udereva wa awali ada ni 150000-180000 pia unaweza kupitia pale chang'ombe utapewa joining instructions bure. kama unataka udereva uwe ndo ajira yako, baada ya kumaliza hayo mafunzo utapewa cheti kisha utapelekwa usalama barabarani makao makuu kwa ajili ya mtihani wa mwisho ambao ukipita utapewa leseni daraja d ambalo linakuruhusu kuendesha magari madogo yasio ya biashara wala mizigo unatakiwa ukae na hii leseni miaka mitatu ndipo uweze kusomea magari makubwa ya abiria au mizigo......swali lingine
 
kama ndo unaanza unapaswa kusoma udereva wa awali ada ni 150000-180000 pia unaweza kupitia pale chang'ombe utapewa joining instructions bure. kama unataka udereva uwe ndo ajira yako, baada ya kumaliza hayo mafunzo utapewa cheti kisha utapelekwa usalama barabarani makao makuu kwa ajili ya mtihani wa mwisho ambao ukipita utapewa leseni daraja d ambalo linakuruhusu kuendesha magari madogo yasio ya biashara wala mizigo unatakiwa ukae na hii leseni miaka mitatu ndipo uweze kusomea magari makubwa ya abiria au mizigo......swali lingine
Sina swali mkuu ila nashukuru xana kwa maelezo yko.
Mungu akipenda mwakan nataka nkajiunge.
 
mkuu hapo juu ametoa maelezo mazuri sana,hayo malipo hayausiani na malipo ya lesen,lesen inatoka tra kwa bei ya 40000 tu.
 
Shukra kwenu wote ambao mmefanikisha kunipa mwangaza kutokana na jambo hili.
MUNGU hawa bariki
 
Ndugu wananchi. Elimu yangu ni form four lakn kwa bahati mbaya nilipata matokeo mabaya yaani failure.
Naomba mnafahamishe kama nitaruhusiwa kujiunga VETA ndugu zanguni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom