Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,603
- 29,744
Na Ndesumbuka Merinyo
Mbunifu wa Mavazi Afrika Sana
Kwa mara ingine hivi karibuni tumetangaziwa na Waziri mwenye dhamana na utamaduni wa taifa kwamba imeundwa kamati ya "kutafuta" vazi la taifa.
Hii ni mara ya tatu kwa serikali kufanya jambo hili. Mara ya kwanza ilikuwa miaka ya 2003-4 wakati ilipoandaa mashindano ya kupata vazi la taifa. Binafsi nilishiriki mashindano yale na nilikuwa mshindi wa jumla mkoani Kilimanjaro, na kitaifa moja ya mavazi niliyosanifu liliteuliwa kuwemo kama vazi la taifa upande wa wanaume.
Matokeo haya hayakutokea hivihivi, bali usanifu wangu uliegemea sana matokeo ya utafiti nilioshiriki wa mavazi ya asili ya makabila 9 maeneo kadhaa ya nchi yetu. Pale Dodoma kwenye mashindano kitaifa Vazi moja la kike lililobuniwa na maanii kutoka Kigoma lilishinda upande wa nguo za wanawake. Baada ya zoezi lile hapana chochote kilichofanywa na serikali kuhusu "matokeo" hayo.
Ukapita karibu muongo mmoja, na 2012 serikali ikatangaza "kutafuta" upya vazi la taifa. Ikaundwa kamati ya kitaifa, ambamo nilikuwa mjumbe. Safari ile kamati ikatembelea kanda sita nchi nzima na kupata maoni ya wananchi. Baada ya kukusanya maoni, kamati ikakaa na wataalam wa nguo - wasanifu vitambaa, watengeneza nguo viwandani na wasanii wachoraji.
Matokeo ya mchakato yakakusanywa katika kabrasha kubwa lenye maelezo ya kina na picha anuai. Ripoti rasmi ikakabidhiwa kwa Waziri mwenye dhamana. Kwa bahati nzuri niliikabidhi kwa mkono wangu kwa Waziri husika kwa niaba ya Mwenyekiti wa kamati aliyekuwa safarini. Kutoka hapo kikatokea kimya kizito cha muda mrefu kuhusu jambo la vazi la taifa.
Baadae, kwenye Awamu ya Tano ya uongozi wa nchi, Waziri mwenye dhamana na utamaduni, baada ya kubanwa kwa maswali kutoka kwa wadau na wabunge, akatamka kuwa serikali imefuta wazo hilo na kila Mtanzania atajishonea aonavyo inafaa kujiwakilisha kama Mtanzania.
Kabla maji yaliyomwagika hayajanyaushwa vema na joto la muda, tumeshtushwa tena kuona kwamba serikali ya Awamu ya Sita nayo imeamua kutengeneza fursa ingine ambayo bila kigugumizi naiita fursa ya kutumia vibaya rasimali za nchi.
Baada ya kushiriki mchakato wa mashindano ya kutafuta vazi ya mwaka 2003-4 na mchakato wa kamati wa 2012, niliona nina wajibu wa kushauri taifa letu kuhusu jambo hili. Niliandika makala iliyochapishwa kwenye magazeti ya Mwananchi na Nipashe ambayo kimsingi nilishauri kwamba mitindo iliyokuwa inatumiwa na serikali, ima kwa mashindano au kwa kamati, hayana tija na hayataleta matokeo yanayotarajiwa. Nilishauri kuwa serikali iangalie zaidi masuala ya sera zake zinazohusiana kwa namna moja au ingine na tasnia ya nguo nchini ili kutengeneza mazingira ambayo mavazi ya kitaifa yangeibuka bila matumizi ya kamati wala mashindano.
Mwaka jana nilirejea kufanya itafiti wa mavazi ya jadi ya jamii zetu za kikabila kwa undani zaidi nikiitumia mikoa mitatu ya Tanga, Arusha na Manyara. Utafiti wangu, pamoja na kuangazia uasili, malighafi, matumizi na maadili ya uvaaji, ulijaribu pia kuangalia manufaa na athari za utengenezaji wa mavazi ya jadi kwa tasnia ya usanifu mavazi kwa nyakati hizi nchini Tanzania. Niliwasilisha matokeo ya utafiti wangu serikalini kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) tarehe 7 Machi, 2022 pale ofisi za BASATA.
Tarehe 29 Julai, 2022 nitaendesha warsha jijini Arusha ambayo itakutanisha washiriki wa utafiti huo (wakiwemo maafisa utamaduni wa maemeo husika walioshiriki na BASATA wenyewe) kwa ajili ya kupata ithibati ya washiriki ili niweze kuhifadhi matokeo ya utafiti huu katika makavazi ya kidijitali kwa matumizi ya yeyote kwa vizazi vijavyo.
Baada ya maelezo haya, ni imani yangu kuwa viongoi wetu wanaopewa dhamana za ofisi mbalimbali ni watu weledi ambao wanaweza kuzingatia historian, uzoefu na tajiriba badala ya kufanya mambo kwa kufiata njia rahisi ambazo zimeshadhihirika kutoleta tija kwa taifa.
Ushauri wangu ni kwamba zoezi hili lisitishwe kabla hatujapoteza tena pesa za walipa kodi wa Tanzania kwa jambo ambalo lina muhali.
Mbunifu wa Mavazi Afrika Sana
Kwa mara ingine hivi karibuni tumetangaziwa na Waziri mwenye dhamana na utamaduni wa taifa kwamba imeundwa kamati ya "kutafuta" vazi la taifa.
Hii ni mara ya tatu kwa serikali kufanya jambo hili. Mara ya kwanza ilikuwa miaka ya 2003-4 wakati ilipoandaa mashindano ya kupata vazi la taifa. Binafsi nilishiriki mashindano yale na nilikuwa mshindi wa jumla mkoani Kilimanjaro, na kitaifa moja ya mavazi niliyosanifu liliteuliwa kuwemo kama vazi la taifa upande wa wanaume.
Matokeo haya hayakutokea hivihivi, bali usanifu wangu uliegemea sana matokeo ya utafiti nilioshiriki wa mavazi ya asili ya makabila 9 maeneo kadhaa ya nchi yetu. Pale Dodoma kwenye mashindano kitaifa Vazi moja la kike lililobuniwa na maanii kutoka Kigoma lilishinda upande wa nguo za wanawake. Baada ya zoezi lile hapana chochote kilichofanywa na serikali kuhusu "matokeo" hayo.
Ukapita karibu muongo mmoja, na 2012 serikali ikatangaza "kutafuta" upya vazi la taifa. Ikaundwa kamati ya kitaifa, ambamo nilikuwa mjumbe. Safari ile kamati ikatembelea kanda sita nchi nzima na kupata maoni ya wananchi. Baada ya kukusanya maoni, kamati ikakaa na wataalam wa nguo - wasanifu vitambaa, watengeneza nguo viwandani na wasanii wachoraji.
Matokeo ya mchakato yakakusanywa katika kabrasha kubwa lenye maelezo ya kina na picha anuai. Ripoti rasmi ikakabidhiwa kwa Waziri mwenye dhamana. Kwa bahati nzuri niliikabidhi kwa mkono wangu kwa Waziri husika kwa niaba ya Mwenyekiti wa kamati aliyekuwa safarini. Kutoka hapo kikatokea kimya kizito cha muda mrefu kuhusu jambo la vazi la taifa.
Baadae, kwenye Awamu ya Tano ya uongozi wa nchi, Waziri mwenye dhamana na utamaduni, baada ya kubanwa kwa maswali kutoka kwa wadau na wabunge, akatamka kuwa serikali imefuta wazo hilo na kila Mtanzania atajishonea aonavyo inafaa kujiwakilisha kama Mtanzania.
Kabla maji yaliyomwagika hayajanyaushwa vema na joto la muda, tumeshtushwa tena kuona kwamba serikali ya Awamu ya Sita nayo imeamua kutengeneza fursa ingine ambayo bila kigugumizi naiita fursa ya kutumia vibaya rasimali za nchi.
Baada ya kushiriki mchakato wa mashindano ya kutafuta vazi ya mwaka 2003-4 na mchakato wa kamati wa 2012, niliona nina wajibu wa kushauri taifa letu kuhusu jambo hili. Niliandika makala iliyochapishwa kwenye magazeti ya Mwananchi na Nipashe ambayo kimsingi nilishauri kwamba mitindo iliyokuwa inatumiwa na serikali, ima kwa mashindano au kwa kamati, hayana tija na hayataleta matokeo yanayotarajiwa. Nilishauri kuwa serikali iangalie zaidi masuala ya sera zake zinazohusiana kwa namna moja au ingine na tasnia ya nguo nchini ili kutengeneza mazingira ambayo mavazi ya kitaifa yangeibuka bila matumizi ya kamati wala mashindano.
Mwaka jana nilirejea kufanya itafiti wa mavazi ya jadi ya jamii zetu za kikabila kwa undani zaidi nikiitumia mikoa mitatu ya Tanga, Arusha na Manyara. Utafiti wangu, pamoja na kuangazia uasili, malighafi, matumizi na maadili ya uvaaji, ulijaribu pia kuangalia manufaa na athari za utengenezaji wa mavazi ya jadi kwa tasnia ya usanifu mavazi kwa nyakati hizi nchini Tanzania. Niliwasilisha matokeo ya utafiti wangu serikalini kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) tarehe 7 Machi, 2022 pale ofisi za BASATA.
Tarehe 29 Julai, 2022 nitaendesha warsha jijini Arusha ambayo itakutanisha washiriki wa utafiti huo (wakiwemo maafisa utamaduni wa maemeo husika walioshiriki na BASATA wenyewe) kwa ajili ya kupata ithibati ya washiriki ili niweze kuhifadhi matokeo ya utafiti huu katika makavazi ya kidijitali kwa matumizi ya yeyote kwa vizazi vijavyo.
Baada ya maelezo haya, ni imani yangu kuwa viongoi wetu wanaopewa dhamana za ofisi mbalimbali ni watu weledi ambao wanaweza kuzingatia historian, uzoefu na tajiriba badala ya kufanya mambo kwa kufiata njia rahisi ambazo zimeshadhihirika kutoleta tija kwa taifa.
Ushauri wangu ni kwamba zoezi hili lisitishwe kabla hatujapoteza tena pesa za walipa kodi wa Tanzania kwa jambo ambalo lina muhali.