Fafanua kidogo
Mkuu myplusbee unaelewaje kipengele hiki cha 72:11-14????

""Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani,wala hatuwezi kumponyoka kwa kumkimbia.""

Je neno hili halionyeshi kulikuwa na wakati ulipita uliokuwa na historia ya hawa viumbe??

Hatuwezi ikiwakilisha jaribio lililopita na Hatutomshinda ikiwakilisha ukweli waliokuja kuugundua Baadae.
 
Maswala haya ya Dini ni magumu sana mm sipendi sana kupinga mtazamo wa mtu juu ya Imani yake
Kila mtu afanye anachoona ni sahihi juu ya nafasi yake
 
Mkuu myplusbee kuali ya kwamba ""Hatutomshinda duniani"" huoni kauli hii ikionyesha kuliwahi kuwa na mashindano??
Haiwezekani kuwa waliwahi kushindana??
Hivi kama Mungu anakuambia zinaa inamchukiza, halafu wewe unaamua kuifanya zinaa tena kwa fujo! Hivi huoni hapo unashindana na Mwenyezi Mungu?! Hata mzazi akikuambia usifanye hiki na kile, halafu wewe unaendelea tu kukifanya; hivi huoni kwamba unajaribu kushindana na mzazi wako?!

Anyway, simaanishi wewe kama wewe; wewe nimekutumia tu kama mfano! Ninachotaka kusema ni kwamba, kwa wanaoamini uwezo wa Mwenyezi Mungu, hakuna mingoni mwao anaweza kushindana nae! Na hata hao wasioamini katika Mwenyezi Mungu, miongoni mwao wapo wanaoamini katika supreme power ambayo na yenyewe hawawezi kushindana nayo! Matendo ya maovu ya majini ndiyo yanayoonesha kwamba walikuwa wanajaribu kushindana na Mwenyezi Mungu! Hata Shetani alipomchukua Yesu hadi kule kileleni na kumwambia amsujudie; kitendo kile cha Shetani kilikuwa ni kujaribu kushindana na Mwenyezi Mungu ambae ameshaweka bayana kwamba, hapana yeyote apaswae kusujudiwa isipokuwa ni yeye!! Hata leo hii shetani huyo huyo anapojaribu kuwapotosha ili wafanye yale yanayomchukiza Mwenyezi Mungu na kuyaacha aliyowaamrisha, huko ni kujaribu kushindana na Mwenyezi! Na kwa mana nyingine, hata shetani huyo huyo leo hii akaamua kumrudia Mwenyezi Mungu na kutamka "tulijua hatutomshinda" wala haina maana kwamba Shetani alikuwa kwenye mashindano na Mwenyezi hapo kabla bali tu uovu wake ndio utakaomfanya afahamu kwamba alikuwa anajaribu kushindana na Mwenyezi Mungu ambae katu hawezi kuwa na mshindani; at least from Islamic Beliefs, na sina shaka hata Wakristo ndivyo wanavyoamini na ndio maana hata baada ya shetani kumjaribu Yesu, according to Mathayo 4:10:
 
Usitazame muislam anafanya nini tazama Qur-ani inasemaje.
Mambo hata ya utabiri,nyota kiislam hayaruhusiwi lakini utakuta masheikh ndio zao hizo kuelezea kesho ya mja
EXACTLY!! Na hapa ndipo watu wanapochanganya! Wakimuona Sheikh Yahya anazungumzia ulinzi kwa kutumia majini, watu wanadhani ndio Uislamu wenyewe huo wakati Quran imeshasema wazi kwamba, hakuna ulinzi wowote zaidi ya ule unaopewa na Mwenyezi Mungu! Sasa sidhani hata huyo pagan anaamini Jini ndie Mwenyezi Mungu!!
 
Sio kwa mujibu wa Quran! Kwa mujibu wa Quran, majini ni miongoni tu mwa viumbe wa Mwenyeji Mungu vilivyoumbwa nae huku wakiwa wamefanana na binadamu kwenye suala la utashi! Lakini kwa kukengeuka tu, wakawa wanafanya yale yanayomchukiza Mwenyezi Mungu hadi pale miongoni mwao siku moja waliposikia Quran na kutoa hiyo kauli kwamba "Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani,wala hatuwezi kumponyoka kwa kumkimbia." Kauli hiyo inaonesha kwamba, pamoja na uovu waliokuwa wanafanya lakini walifahamu uwepo wa Mungu na nini wajibu wao mbele ya Mwenyezi Mungu! Ni kama ambavyo leo hii wanadamu tunavyofanya uovu usiomithirika wakati tunafahamu tufanyayo ni machukizo kwa Mwenyezi Mungu! Na pia tunafahamu katu hatuwezi kumshinda Mwenyezi Mungu, sema ndo vile tumekuwa Watumwa wa Shetani kuliko kuwa watumishi wa Mwenyezi Mungu!

Sasa katikati ya uovu wetu huu, watokee wengine miongoni mwetu watubie kwa Mwenyezi Mungu kwa matendo! Waamue kuacha yale yote yaliyo machukizo kisha ndipo wanakuja kusema "Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani,wala hatuwezi kumponyoka kwa kumkimbia." Kwamba, twafanya uovu wote huu sio kwamba hatujui uwepo wa Mwenyezi Mungu na yale yamchukizayo; au si kwamba wakati uliopita palikuwa na historia inayotuhusu watu kama sisi, bali ni vile tu tumeshukiwa na maono na kuamua kwa dhati kurejea kwa Mwenyezi Mungu!
Kwa hiyo ndo majini yakarudi kumuabudu Mwenyezi Mungu baada ya kushushwa aya ya quran
 
Maswala haya ya Dini ni magumu sana mm sipendi sana kupinga mtazamo wa mtu juu ya Imani yake
Kila mtu afanye anachoona ni sahihi juu ya nafasi yake
wewe huwezikupinga mim sipingi tnachotaka kuondoa extremists
 
Back
Top Bottom