Bishanga
JF-Expert Member
- Jun 29, 2008
- 15,323
- 10,050
Baada ya jana kukiri nimelikoroga nawashukuru mlionipa pole,mambo yote kwa sasa ni muswano.
Sasa ndugu zangu hebu tushauriane hapa.Nina jamaa yangu ambaye alipata sekeseke miaka michache iliyopita akaachana na mkewe. Kwa kuwa watoto wao walikuwa bado ni wadogo mahakama iliamua wabaki na mama yao na jamaa yangu apeleke matunzo,na kwa kweli anafanya hivyo. Nadhani kwa sababu ya stress za talaka (sina hakika na hili) jamaa aliapa kuwa hataki kuzaa tena,nilimshauri awe na subiri akakataa na hivyo kuna siku tulikanyaga kiguu na njia hadi Marie Stopes na jamaa akafanyiwa vasectomy.
Bahati mbaya au nzuri two years ago alipata mwanamke mwingine wakaoana na apparently hakumwambia hii maneno ya vasectomy.Mama anataka kuzaa,mimba haishiki,na hospitali zote amezimaliza. Kwa kuwa mmewe ana watoto na yeye vipimo vinaonyesha yuko ok basi yeye anaamini tatizo sio mme ila damu zao hazipatani.Shemeji tumeshibana sana,sasa kanifuata anaomba ushauri,anataka aende kwa siri India (yeye ni mfanyabiashara mzuri tu) ili akafanyiwe IVF kwa kupandikiza mbegu ya mtu mweusi ili mradi tu azae ndani ya familia, anasema hataki ku cheat na mwanaume mwingine ili apate mimba. Kanitaka ushauri na contact za clinics za huko. Ukisikia pasua kichwa ndo hii,nimemwambia atulie kwanza niulizie nitampa jibu.To tell or not to tell?
Sasa ndugu zangu hebu tushauriane hapa.Nina jamaa yangu ambaye alipata sekeseke miaka michache iliyopita akaachana na mkewe. Kwa kuwa watoto wao walikuwa bado ni wadogo mahakama iliamua wabaki na mama yao na jamaa yangu apeleke matunzo,na kwa kweli anafanya hivyo. Nadhani kwa sababu ya stress za talaka (sina hakika na hili) jamaa aliapa kuwa hataki kuzaa tena,nilimshauri awe na subiri akakataa na hivyo kuna siku tulikanyaga kiguu na njia hadi Marie Stopes na jamaa akafanyiwa vasectomy.
Bahati mbaya au nzuri two years ago alipata mwanamke mwingine wakaoana na apparently hakumwambia hii maneno ya vasectomy.Mama anataka kuzaa,mimba haishiki,na hospitali zote amezimaliza. Kwa kuwa mmewe ana watoto na yeye vipimo vinaonyesha yuko ok basi yeye anaamini tatizo sio mme ila damu zao hazipatani.Shemeji tumeshibana sana,sasa kanifuata anaomba ushauri,anataka aende kwa siri India (yeye ni mfanyabiashara mzuri tu) ili akafanyiwe IVF kwa kupandikiza mbegu ya mtu mweusi ili mradi tu azae ndani ya familia, anasema hataki ku cheat na mwanaume mwingine ili apate mimba. Kanitaka ushauri na contact za clinics za huko. Ukisikia pasua kichwa ndo hii,nimemwambia atulie kwanza niulizie nitampa jibu.To tell or not to tell?