Vasectomy inataka kuleta balaa!

Bishanga

JF-Expert Member
Jun 29, 2008
15,323
10,050
Baada ya jana kukiri nimelikoroga nawashukuru mlionipa pole,mambo yote kwa sasa ni muswano.
Sasa ndugu zangu hebu tushauriane hapa.Nina jamaa yangu ambaye alipata sekeseke miaka michache iliyopita akaachana na mkewe. Kwa kuwa watoto wao walikuwa bado ni wadogo mahakama iliamua wabaki na mama yao na jamaa yangu apeleke matunzo,na kwa kweli anafanya hivyo. Nadhani kwa sababu ya stress za talaka (sina hakika na hili) jamaa aliapa kuwa hataki kuzaa tena,nilimshauri awe na subiri akakataa na hivyo kuna siku tulikanyaga kiguu na njia hadi Marie Stopes na jamaa akafanyiwa vasectomy.
Bahati mbaya au nzuri two years ago alipata mwanamke mwingine wakaoana na apparently hakumwambia hii maneno ya vasectomy.Mama anataka kuzaa,mimba haishiki,na hospitali zote amezimaliza. Kwa kuwa mmewe ana watoto na yeye vipimo vinaonyesha yuko ok basi yeye anaamini tatizo sio mme ila damu zao hazipatani.Shemeji tumeshibana sana,sasa kanifuata anaomba ushauri,anataka aende kwa siri India (yeye ni mfanyabiashara mzuri tu) ili akafanyiwe IVF kwa kupandikiza mbegu ya mtu mweusi ili mradi tu azae ndani ya familia, anasema hataki ku cheat na mwanaume mwingine ili apate mimba. Kanitaka ushauri na contact za clinics za huko. Ukisikia pasua kichwa ndo hii,nimemwambia atulie kwanza niulizie nitampa jibu.To tell or not to tell?
 
Hivi ukifanyiwa Vasectomy ndo imetoka huwezi tena kuiunga ile mirija ukapata watoto
Ahhh hiyo mbaya sana
 
Kwa nini guyo mwanamke hataki kucheat wakati huyom mwanamume amemficha kilema chake?
 
Huyo jamaa ndo maana aliachana na mkewe kazidi roho mbaya na ni muuwaji anajua kuwa hawezi
kuzaa na hamwambii mkewe wa sasa hiyo ni tabia mbovu sana. (Kama unaweza cheat naye azae) ila usimwambie chochote kuwa
muweze hawezi kuzaa tena.
Hapo tu ndipo huwa napandwa hasira na wanaume sijui mkoje roho mbaya tuuu
 
da bishanga leo umekuja na pasua kichwa sema mimi nina aleji na maswala ya ndoa magumuuuuu.......
 
Hivi ukifanyiwa Vasectomy ndo imetoka huwezi tena kuiunga ile mirija ukapata watoto
Ahhh hiyo mbaya sana
you can ila chances ni 50/50 na ni very expensive (inaweza kufikia hata USD 50,000.- kutegemea na class ya hospital)
 
Huyo jamaa ndo maana aliachana na mkewe kazidi roho mbaya na ni muuwaji anajua kuwa hawezi
kuzaa na hamwambii mkewe wa sasa hiyo ni tabia mbovu sana. (Kama unaweza cheat naye azae) ila usimwambie chochote kuwa
muweze hawezi kuzaa tena.
Hapo tu ndipo huwa napandwa hasira na wanaume sijui mkoje roho mbaya tuuu
wasiwasi wangu mimba ikishika njemba si itaua mtu? kama ni roho mbaya hata nyie kinamama wakati mwingine Adolf Hitler cha mtoto kwa jinsi huwa mnatutenda.
 
you can ila chances ni 50/50 na ni very expensive (inaweza kufikia hata USD 50,000.- kutegemea na class ya hospital)

Mhhh hiyo ngumu kabisa
Aongee na mkewe amwambie ukweli kuwa alishafanyiwa hiyo kitu na waangalie namna ya kupandikiza mbegu
Ili hata kama mke akipata mimba asije akatolewa mbio
Ila kufanya hiyo kitu aise ni noma
 
Huyo jamaa ndo maana aliachana na mkewe kazidi roho mbaya na ni muuwaji anajua kuwa hawezi <br />
kuzaa na hamwambii mkewe wa sasa hiyo ni tabia mbovu sana. (<font color="#ffffff">Kama unaweza cheat naye azae</font>) ila usimwambie chochote kuwa <br />
muweze hawezi kuzaa tena.<br />
Hapo tu ndipo huwa napandwa hasira na wanaume sijui mkoje roho mbaya tuuu
<br />
<br />
hilo lijamaa lingekuwa karibu ungelitwanga ngumi!!?
Tatizo mke akicheat akapata mimba jamaa atajua kabisa si yake. Tena huyo mke ni mwaminifu sana, nimeyapenda mawazo yake.
 
Chanzo cha yote ni ukilaza wa huyo jamaa yako,sasa acha wife akapandikizwe mbegu na yeye aendelee kukaa kimya tu alee si amejifanya yeye mfalme wa kuficha siri?
 
Duh! Jamaa yako alifanya makosa kutomweka wazi. Mshauri ashauriane na mumewe hilo swala la kupandikizwa mbegu.
Ni kweli. Kwani siku huyo mke akitangaza kuwa ana mimba wakati mume anajua hana uwezo wa kutia mimba, atajua kuwa mke wake amepoteza uaminifu na hivyo amegawa uroda nje....chuki itakayozuka kuanzia hapo huenda ikawa kubwa zaidi ya kukosa mtoto!.
 
<br />
<br />
hilo lijamaa lingekuwa karibu ungelitwanga ngumi!!?
Tatizo mke akicheat akapata mimba jamaa atajua kabisa si yake. Tena huyo mke ni mwaminifu sana, nimeyapenda mawazo yake.

Tena mangumi ya uso reception yote is laitioff kabisa shenzi sana hili jamaa pambaf zake
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom