changaule
JF-Expert Member
- Jan 10, 2020
- 5,587
- 9,179
Umeongea huku umejipinga mwenyewe mwishoni kwamba morali ya kuwa nyumbani haifanyi kazi kwembe mpira wa miguu labda uwe na mbinu zinginezo lakini sio kutegemea morali ikubebe. Timu ikufunge goli tano kwake halafu timu hiyo hiyo ije Dar na kubadilika kuwa timu amateur.Maswali yako anajiuliza shabiki wa rede. Kwa mashabiki wa soka inajulikana kabisa kuwa timu ikiwa nyumbani inakuwa na morali ya juu na ndio maana kuna sheria ya faida ya away goal(mechi za mtoano). Kwa hiyo timu ikiwa nyumbani halafu ikiwa na ubora wa timu unaoshabihiana au kuwazidi timu pinzani basi ni rahisi kupata matokeo.
Ndio maana pamoja na morali waliokuwa nayo utopolo walipokutana na pyramid pale Kirumba mbele ya mashabiki lukuki lakini walipigwa 2-0 kutokana na kiwango kusaliti hata kama morali ilikuwepo.