Humble African
JF-Expert Member
- Jul 28, 2013
- 4,779
- 14,303
Maisha hayajawahi kuwa magumu hata siku moja bali ni sisi tu binadamu ndio tunakuwaga na mioyo migumu na tunashindwa kujipekecha sahihi ili kuendana na kasi ya Dunia.
Kasi ya Dunia ni kujua fursa zikoje kwa wakati sahihi na kisha kufanya maamuzi sahihi ili hatimae kila kitu kiende sawa sawia. Na hii yote inawezekana kama tukitafuta taarifa bila kuchoka na kuzifanyia kazi kwa wakati maana in this age of information, ignorance is rather your choice.
Hivyo ni choice ya watu wengi kutoji updates na kupata taarifa kwa wakati ili wapige hela zao kwa uzuri. Imagine wale watu waliopata taarifa mapema za M-pesa na kuzifanyia kazi wakati, walinufaika sana na M-Pesa kiuchumi... Achili mbali hiyo kuna Bitcoin wale watu walioijua tangu ilipokuwa changa mwaka 2011 huko ikiuzwa kwa dola $2 na wakachangamkia fursa leo hii ni mamilionea sababu Bitcoin ilishafikia dola $19000. Anyways, labda hii ya Bitcoin inaweza kuwa ngumu je unaikumbuka ile ya kuhama kutoka kwenye kanda za cassette kwenda kwenye CD... Wale waliochungulia fursa mapema walipiga hela nzuri tu kwa kuuza CD kwa bei wanayotaka. Hata lile ombwe la kuhamia kwenye simu za mkononi... Anko wangu alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzoni kabisa kuchungulia hii fursa mapema then akapiga pesa ndefu sana.
Cha kuzingatia hapa ni kuifahamu fursa kwa undani zaidi mapema kabla ya wengine then uwezekano wa kuyaona maisha katika mwana bora zaidi hauepukiki.
Hapa ndipo linapokuja suala la kujua na kuifahamu kwa undani zaidi Neema ya vanilla iliyopanda bei maradufu zaidi ya madini ya silver ndani ya mwaka huu ambapo vanilla imeipiku silver ikiuzwa $600 na silver ikiuzwa dola $550, kupanda kwa bei kumesababishwa na kuongezeka kwa matumizi ya vanilla Duniani kwa kutengenezea madawa na pia kupungua kwa uzalishaji kwa mzalishaji mkuu wa vanilla Duniani ambayo ni nchi ya Madagascar.
Kwa hapa Tanzania kule Kagera kuna wakulima wa Vanilla ambayo wanaiuza Tsh 150,000/= kwa kilo. Then Kwenye soko la Dunia ndio inauzwa Tshs million1.5. Kama unataka kununua reja reja jipeche zaidi maeneo ya Kagera na kama unata kulima maeneo yenye hali ya hewa ya tropic ndio favourable conditions kwa hili zao.
Ukiwa na kilo 50 za Vanilla kwa bei ya million 1.5 kwa kilo utakuwa na jumla ya Tshs milioni 75 hapa ndipo jina lako linabadilika mtaani na unapewa jina jipya la Freemason, sio jina tu hata wewe unaanza kutembea umetanua mikono kama una majipu kwenye makwapa vile kwa ukwasi na kujiamini.
Information is power, And now you know.
I'm gone!
Sent using Jamii Forums mobile app
Kasi ya Dunia ni kujua fursa zikoje kwa wakati sahihi na kisha kufanya maamuzi sahihi ili hatimae kila kitu kiende sawa sawia. Na hii yote inawezekana kama tukitafuta taarifa bila kuchoka na kuzifanyia kazi kwa wakati maana in this age of information, ignorance is rather your choice.
Hivyo ni choice ya watu wengi kutoji updates na kupata taarifa kwa wakati ili wapige hela zao kwa uzuri. Imagine wale watu waliopata taarifa mapema za M-pesa na kuzifanyia kazi wakati, walinufaika sana na M-Pesa kiuchumi... Achili mbali hiyo kuna Bitcoin wale watu walioijua tangu ilipokuwa changa mwaka 2011 huko ikiuzwa kwa dola $2 na wakachangamkia fursa leo hii ni mamilionea sababu Bitcoin ilishafikia dola $19000. Anyways, labda hii ya Bitcoin inaweza kuwa ngumu je unaikumbuka ile ya kuhama kutoka kwenye kanda za cassette kwenda kwenye CD... Wale waliochungulia fursa mapema walipiga hela nzuri tu kwa kuuza CD kwa bei wanayotaka. Hata lile ombwe la kuhamia kwenye simu za mkononi... Anko wangu alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzoni kabisa kuchungulia hii fursa mapema then akapiga pesa ndefu sana.
Cha kuzingatia hapa ni kuifahamu fursa kwa undani zaidi mapema kabla ya wengine then uwezekano wa kuyaona maisha katika mwana bora zaidi hauepukiki.
Hapa ndipo linapokuja suala la kujua na kuifahamu kwa undani zaidi Neema ya vanilla iliyopanda bei maradufu zaidi ya madini ya silver ndani ya mwaka huu ambapo vanilla imeipiku silver ikiuzwa $600 na silver ikiuzwa dola $550, kupanda kwa bei kumesababishwa na kuongezeka kwa matumizi ya vanilla Duniani kwa kutengenezea madawa na pia kupungua kwa uzalishaji kwa mzalishaji mkuu wa vanilla Duniani ambayo ni nchi ya Madagascar.
Kwa hapa Tanzania kule Kagera kuna wakulima wa Vanilla ambayo wanaiuza Tsh 150,000/= kwa kilo. Then Kwenye soko la Dunia ndio inauzwa Tshs million1.5. Kama unataka kununua reja reja jipeche zaidi maeneo ya Kagera na kama unata kulima maeneo yenye hali ya hewa ya tropic ndio favourable conditions kwa hili zao.
Ukiwa na kilo 50 za Vanilla kwa bei ya million 1.5 kwa kilo utakuwa na jumla ya Tshs milioni 75 hapa ndipo jina lako linabadilika mtaani na unapewa jina jipya la Freemason, sio jina tu hata wewe unaanza kutembea umetanua mikono kama una majipu kwenye makwapa vile kwa ukwasi na kujiamini.
Information is power, And now you know.
I'm gone!
Sent using Jamii Forums mobile app