Van Dame(Sinza), Yesu (Mbeya) kati ya Wababe waliowahi tikisa Tanzania

nlikuwa na jamaa yangu ananipa visa na mikasa mbali mbali ya Jiji la Mbeya miaka ya 1980s mpaka 1990s. alianza kunambia jinsi ambavyo miaka hiyo vijana wengi jijini mbeya ilikuwa lazima waende GYM, wajifunze Karate/Kung fu au Tae kwon do na michezo mingine mbalimbali ya mapigano.

mwenyeji wangu ananitajia mmoja ya watu anaowakumbuka miaka ile alikuwepo Daud. huyu kwa watu wengi wa Mbeya miaak ile wanamkumbuka jamaa likuwa amejenga mwili na kujichora tattoo kadhaa mwilini mara nyingi akitembea amevaa singlet kuonesha tattoo zake na misuli yake iliyokuwa imejaa vyema kabisa. huyu alikuwa mbabe,ngumi jiwe miaka hiyo akipiga ngumi uliyepigwa unaona kama umepigwa na jiwe zito sana kutokana na kuwa na nakozi kwenye mikono. wengi walikuwa wakizimia kutokana na ngumi alizokuwa akipiga watu.akaendelea kunipa historia ya wababe wengine waliowahi kutokea jijini humo miaka ya kale.

anasema miaka hiyo alitokea jamaa mmoja alikuwa anaitwa Shetani. jamaa alikuwa ana uwezo mzuri sana wa kutembeza kipigo kwa raia na askari kiasi kwamba askari wenyewe walikuwa wakimgwaya sana. alikuwa kwa mbeya mjini yeye ndiye mtemi anayefahamika. na kama hukukubaliana naye ilikuwa ni jambo rahisi tu mnakubaliana siku ya weekend mnaenda kukutana eneo flani kwa ajili ya kutembezeana mkono mpaka apatikane mshindi.

utawala wa huyu bwana ulikuja kukomeshwa na jamaa mmoja ambaye alikuja kupewa jina la yesu. huyu aliitwa yesu baada ya yeye kuja kumtembezea kipigo kikubwa sana huyo shetani. huyu yesu inasemwa kuwa yeye alitokea Zambia. kufika Mbeya mjini akawa amesikia habari hizo za uwepo wa shetani kuwa ndiye mbabe ile kinyama. na ikatokea siku moja wakakutana katika mizunguko ya maisha katika kutunishiana misuli ikaamuliwa zichapwe.

msimualiaji anasema miaka hiyo walipata nafasi ya kushuhudia ngumi kama za kwenye movie live kabisa bila chenga. zilipigwa ile kinyama. mapigo na ufundi mbalimbali mpaka dakika za mwisho shetani alikuwa hoi vibaya sana na kuamua ku surrender. ndipo yule mbabe mpya alipopewa jina la yesu.tofauti na shetani wanasema huyu yesu alikuwa ni mstaarabu hakuwa akionea watu au kufanya mambo kibabe.

hayo ni mambo ya Jiji la Mbeya miaka hiyo. pamoja na kuwepo pia wababe wengi maeneo mbalimbali jijini humo hasa akisema maeneo kama machinjion,sisimba,sinde,meta,soko matola,mwanjelwa n.k

nikakumbuka miaka ya 200s dar es salaam alikuwepo jamaa mmoja naye shababy sana al maarufu kwa jina la van dame wa sinza. huyu jamaa nilishasikia sana habari zake miaka hiyo na kwa bahati mbaya mimi umri wangu ulikuwa umeshasogea sogea sikuwa naendelea tena na mchezo nliokuwa nikiupenda wa MMA. maana nlijifunza kung fu, nilikuwa mzuri kwenye Katare na kiasi judo. hii ilinipelekea pia nicheze michezo mingi kama Kick Boxing n.k miaka hiyo ya nyuma.

Van Dame alikuwa anasifika sana kwa uwezo mzuri aliokuwa nao wa kurusha mateke. na wepesi katika kuruka na kukimbia inapohitajika. polisi wengi walikuwa wakimgwaya na hata hawakuwa wakitamani kwenda mkamata maana alikuwa na uwezo wa kuwatembezea kipigo kikubwa sana hata wakarudi kituoni wakiwa hoi na wenye hali mbaya kimwili.

tatizo kubwa la Van Dame lilikuwa nasikia ni usela choo mwingi sana. alikuwa akikaba watu au kupora vitu vya thamani na ilikuwa akikufanyi hivyo huna cha kumfanya . ukimpeleka polisi wataishia tu kuandika maelezo na kuanzia hapo wao ndo wanaanza kumkwepa ili wasije wakajikuta wapo katika mazingira ambayo walipaswa kumshika halafu ikawa ngumu.

hivyo polisi wenyewe ikawa ukiwaambia vn dame nimemwona mwenye .... au kijitonyama.. basi siku hiyo polisi hawakanyagi kabisa maeneo ya huko. hali ilikuwa ikizidi sana wanaenda kumwomba aende kituoni naye atawaambia basi haina shida ntakuja baadaye au kesho.

van dame wanasema alikuwa mbabe kinyama.... sifahamu mwishowe aliishia wapi lakini ni mmoja ya watu ambao walikuwa na sifa lukuki katika sanaa za mapigano.

JE MKOANI MWAKO ALIKUWEPO NANI MBABE NA SASA YUPO WAPI? TUENDELEE KUJULISHANA HAYA MAMBO YA KIBABE... KWA SASA UTU UZIMA NA KAZI ZETU HIZI ZINATUZUIA SISI WENGIE TUSIISHI MAISHA HAYA. LAKINI KIUKWELI NI MAISHA AMBAYO MIMI HUWA NAYAMISS SANA. NA ILIKUWA NGUMU KUSIKIA WANAKUWEPO AKINA JUMA LOKOLE... sababu wanaume ilikuwa ni kugangamaa toka ukiwa mdogo. unakua kiume hasa. siku hizi watoto wanavaa mlegezo?

zamani ungevaa mlegezo kuna mbabe mmoja angekuita na kukwambia asikuone tena unakanyaga mtaani KWAKE ukiwa umevaa hivyo sababu next time atakugonga makwenzi kinyama mpaka akili yako ikae sawa. au akuone unatembea kishoga shoga... angekucharaza viboko na kukwambia asikuone tena mtaani unachafua hali ya hewa.


GuDume Bujibuji Mshana Jr Chizi Maarifa @ na wadau wengi wenyeji wa dar na mikoa mingine. Hasa Arusha Macharliee mtupe habari za wababe waliowah kuwepo na walipo mpaka sasa.
Umenikumbusha mbali sana enzi hizo mbeya. Umemsau mwasimba wa nonde. Alikuwepo mwakayugu kipindi hicho stand ya chunya ilikuwa chini hapo karibu na rift Varey hotel. Kipindi hicho dhahabu inatema mbaya chunya,wasukuma walikuwa wanapolwa balaaaa pale stand na akina mwakayugu. Alikuwa anawapora milioni 20,50 kipindi hicho au dhahabu za kiwango hicho ilikuwa kitu cha kawaida. Alikuwa anachomeka nato refu kuanzia kuanzia kwenye buti lake refu,kuja juu kwenye ka-jeans kake ka kubana. Siku moja ilikuwa inapigwa gemu (kamali)kule nyuma mtoni sinde. Mwakayugu akaliwa hela yote,mpaka buti,nguo,akabakiwa na chupi tu. Sasa kulikuwa na mtindo wa aliye-win siku hiyo anawapa arifu aliowala,hiyo arifu ilikuwa kama nauli ya kwendea home. Sasa mwakayugu alipewa arifu ya kwanza akaliwa nayo. Jamaa alie win siku hiyo akamwambia kula mjusi yule nitakupa arifu nyingine. Duuh...! Lile lijamaa mwakayugu lilikuwa kama mnyama hivi. Likaurukia ule mjusi na kuukata na meno,likaanza kuutafuna mjusi bwana. Basi pale karibu wote tulistuka tukataka kukimbia,yule jamaa aliemwambia ale mjusi,akamwambia acha acha acha,chukua hela arifu hii hapa. Aaah...! Wapi jamaa likaendelea tu kuutafuna ule mjusi,likaumaliza. Likainama chini mtoni pale likachota maji na viganja vyake likanywa maji,likachota likanywa,hapo limeliwa kila kitu mpaka nato(kisu kikubwa) lake limebakiwa na njupi tu. Jamaa lilikuwa hatari balaa. Lilipanda juu hivi,bingwa lililojizira zira hivi,likimya,linaongea kwa vitendo tu. Nasikia liko south Africa now
 
Naona amekusimulia sehemu nyingine anekuchanganya Daud Masonke wa Mafiati alijichora tatuu moja kwenye bega D...na pia alivuliwa ukuu kwa kupigwa na jamaa mmoja wa Isanga akiitwa Brigadier Mwakayugu huyu jamaa alikua hana mwili ila alikomaa mbaya na akipigwa havimbi siku wapo Mount Living stone disco kila mtu akawa anatangaza yeye mbabe walitoka Nje walipigana mpaka maeneo ya Rift Valley hotel baadae wakaanza kitupiana Mawe ikawa vita kati ya wababe wa Isanga na Mafiati huko maguruweni ilifikia mpaka vijana wa Mafiati hawaruhusiwi kukatiza Isanga kwenda kuzika makaburi ya huko wazee wa pande zote mbili waliingilia kati huku kuna kijana mdogo Marehemu Atu Mwaijande ilikua ni hatari...kuhusu Shetani na Yesu walikua washkaji sikumbuki kama walishawahi kupigana nachokumbuka walizima disco lililofanyika Iyunga sec na Chuo cha MTC wao wakitaka kuondoka walikua wanataka disco liishe hao ndio wababe wa Zamani Mbeya miaka hiyo Mbeya usipokua Nunda unaonewa sana...Disco tunaenda kwa mguu popote pale na kurudi usiku muda mwingine hata peke yako....
Jambazi JoMbi ndio mwisho wamaneno mbeya..
 
Miaka ya kuanzia 2004 au 2005 km sikosei nikiwa primary alitokea jamaa mmoja maarufu Mbeya aliitwa zebedayo huyu jamaa alikuwa ni balaa kwenye kufukuza upepo achana na ubabe wa kupigana

Kuna mbwa aliiba samaki kwake bwana huyu alimfukuza mbwa yule na hakutaka kumkamata ni swala la kwenda nae sambamba tu. Mbwa yule alikufa kwa kukosa pumzi ligi ilikuwa kubwa

Bwana huyu pia alishawahi kukimbia kutoka town mpaka tukuyu kwenye msiba na wale walipanda magari kutoka town walishangaa kumkuta zebedayo ameshafika eneo la msiba na gari hakupanda
 
kwa nini zamani alikuwa hakamatwi? na je zile stories za uwezo mkubwa wa kupigana ni za kweli kwa jinsi unavyo mfahamu?
Sio kweli kwamba polisi walikuwa wanamwogopa , hv kweli Askari Ana silaha wewe upigane nao si wanakumaliza tu, Yule alikuwa anakaba watu akikamatwa wahusika hawafuatilii kesi mahakamani anaachiwa, anarud Tena mtaan anendelea na vurugu, ila alisumbua Sana sinza
 
kwa nini zamani alikuwa hakamatwi? na je zile stories za uwezo mkubwa wa kupigana ni za kweli kwa jinsi unavyo mfahamu?
1. Alikuwa hakatwi ksbb zamani askari walikuwa wachache,halafu walikuwa na uzoefu,ujuzi mdogo. Zamani sheria zilikuwa hazifuatwi sana,kwa hiyo hata askari wenyewe walimezeshwa hiyo tabia. 2. Ni kweli walikuwa na uwezo wa kupigana. Zamani vijana wengi waliokuwa wanatoka zambia,hata sasa wana uwezo mkubwa wa kupigana. Kule sehemu za kujifunzia sanaa za mapigano na karibu kila sehemu ni kama jadi
 
Naona amekusimulia sehemu nyingine anekuchanganya Daud Masonke wa Mafiati alijichora tatuu moja kwenye bega D...na pia alivuliwa ukuu kwa kupigwa na jamaa mmoja wa Isanga akiitwa Brigadier Mwakayugu huyu jamaa alikua hana mwili ila alikomaa mbaya na akipigwa havimbi siku wapo Mount Living stone disco kila mtu akawa anatangaza yeye mbabe walitoka Nje walipigana mpaka maeneo ya Rift Valley hotel baadae wakaanza kitupiana Mawe ikawa vita kati ya wababe wa Isanga na Mafiati huko maguruweni ilifikia mpaka vijana wa Mafiati hawaruhusiwi kukatiza Isanga kwenda kuzika makaburi ya huko wazee wa pande zote mbili waliingilia kati huku kuna kijana mdogo Marehemu Atu Mwaijande ilikua ni hatari...kuhusu Shetani na Yesu walikua washkaji sikumbuki kama walishawahi kupigana nachokumbuka walizima disco lililofanyika Iyunga sec na Chuo cha MTC wao wakitaka kuondoka walikua wanataka disco liishe hao ndio wababe wa Zamani Mbeya miaka hiyo Mbeya usipokua Nunda unaonewa sana...Disco tunaenda kwa mguu popote pale na kurudi usiku muda mwingine hata peke yako....
Kipindi hicho mount Livingston ilikuwa kama huna ubavu usiende na demu mkali
 
Sio ubabe tuu walikua watundu sana pia walikua wanatengeneza Tiketi feki za sehemu yeyote iwe Sokoine uwanjani walikua na Tiketi zao walikua wanatambulika kama FAT ya Isanga... huko kwenye disco wanaenda na muhuri watu wakianza kutoka tuu wanagonga kama ule ule na anagongwa mtu anatoa hela anazama ndani...Baunsa mbabe wa Living stone kuna siku aliyakanyaga alivutiwa Nje jamaa walikua wakorofi sana alipigwa aisee bila sababu na mademu kama huna kundi lenye nguvu hutoki nae hata akiwa wako baadae wakaibuka wakina Kambasonic wa Sangu na kundi lake na Wababe wa Nonde huko walikua wanashindana kuangusha ng'ombe mtu mmoja hapo machinjioni...Ila pamoja na maugomvi yao yote vijana wengi darasani walikua wanaweza hiyo ndio Mbeya enzi za Docks Mwanjelwa kabla soko halijaungua...
Hivi mwakayugu yuko wapi?. Nakumbuka mara mwisho enzi hizo aliwaporaga wasukuma karibu milioni 100
 
Miaka ya kuanzia 2004 au 2005 km sikosei nikiwa primary alitokea jamaa mmoja maarufu Mbeya aliitwa zebedayo huyu jamaa alikuwa ni balaa kwenye kufukuza upepo achana na ubabe wa kupigana

Kuna mbwa aliiba samaki kwake bwana huyu alimfukuza mbwa yule na hakutaka kumkamata ni swala la kwenda nae sambamba tu. Mbwa yule alikufa kwa kukosa pumzi ligi ilikuwa kubwa

Bwana huyu pia alishawahi kukimbia kutoka town mpaka tukuyu kwenye msiba na wale walipanda magari kutoka town walishangaa kumkuta zebedayo ameshafika eneo la msiba na gari hakupanda
Zebedayo ni fiction character mkuu?
 
Sio kweli kwamba polisi walikuwa wanamwogopa , hv kweli Askari Ana silaha wewe upigane nao si wanakumaliza tu, Yule alikuwa anakaba watu akikamatwa wahusika hawafuatilii kesi mahakamani anaachiwa, anarud Tena mtaan anendelea na vurugu, ila alisumbua Sana sinza
Ayubu Van Damme amepitia visa vingi sana maisha yake so unachokisikia kibaya cha hovyo jua ni kweli... yule alishapewa pambano na Askari makaburini alipigwa for the first time akienda chini akainuka akatengeneza stamina so yule Askari akawa anampiga Damme haendi chini anapangua na alipoanza kupiga yeye Askari alianguka chini na polisi wengine wakamchangia kwa vitako vya bunduki akatulia akatiwa pingu lumande.. kesi zilizomaliza baada ya kuchomekewa silaha baada ya kuiba akatiwa ndani muda mrefu sijui walimpiga sindano za kupunguza nguvu aliopotoka akawa sio yule but hakuacha kuiba akasekwa tena babake akafa aliyekuwa akimtetea nyumba yao ikauzwa mamake alihamia mwana nyamala alipotoka akahamia huko kwa maza ake akaendeleza ukabaji.

Tatizo anakupa ukimtizama tu kosa anakupa na kukusachi na watu huwa wanamtizama lilivyo na mimacho yake mibaya anawaumiza sana... anavisa zaidi ya milioni
 
Alichofanya yesu huyo ili kumpata shetani alimchukua demu wa shetani na shetani akapewa taarifa kuwa wapo bar ya mwasa pale mabatini na ngumi zilipigiwa hapo na yesu akaondoka na demu wake baada ya kumuadhibu shetani lakini hakukupa habari ya demu anaitwa rodar waulize oss kwa nini walikuwa hawakanyagi mbeya wanaogopa rodar demu hatari huyo ukipata simulizi zake
 
Miaka ya kuanzia 2004 au 2005 km sikosei nikiwa primary alitokea jamaa mmoja maarufu Mbeya aliitwa zebedayo huyu jamaa alikuwa ni balaa kwenye kufukuza upepo achana na ubabe wa kupigana

Kuna mbwa aliiba samaki kwake bwana huyu alimfukuza mbwa yule na hakutaka kumkamata ni swala la kwenda nae sambamba tu. Mbwa yule alikufa kwa kukosa pumzi ligi ilikuwa kubwa

Bwana huyu pia alishawahi kukimbia kutoka town mpaka tukuyu kwenye msiba na wale walipanda magari kutoka town walishangaa kumkuta zebedayo ameshafika eneo la msiba na gari hakupanda

Mmh
 
Wizi hajaacha van Damme ananifahamu Kama jirani sinza na akikutana na watoto wangu anawaita uncle lakini huwez amini siku amekutana na mtoto wangu sinza makaburini akamwambia Mambo ya uncle weka pembeni naomba simu au la nikupige panga
Ayubu Van Damme amepitia visa vingi sana maisha yake so unachokisikia kibaya cha hovyo jua ni kweli... yule alishapewa pambano na Askari makaburini alipigwa for the first time akienda chini akainuka akatengeneza stamina so yule Askari akawa anampiga Damme haendi chini anapangua na alipoanza kupiga yeye Askari alianguka chini na polisi wengine wakamchangia kwa vitako vya bunduki akatulia akatiwa pingu lumande.. kesi zilizomaliza baada ya kuchomekewa silaha baada ya kuiba akatiwa ndani muda mrefu sijui walimpiga sindano za kupunguza nguvu aliopotoka akawa sio yule but hakuacha kuiba akasekwa tena babake akafa aliyekuwa akimtetea nyumba yao ikauzwa mamake alihamia mwana nyamala alipotoka akahamia huko kwa maza ake akaendeleza ukabaji.

Tatizo anakupa ukimtizama tu kosa anakupa na kukusachi na watu huwa wanamtizama lilivyo na mimacho yake mibaya anawaumiza sana... anavisa zaidi ya milioni
 
Wizi hajaacha van Damme ananifahamu Kama jirani sinza na akikutana na watoto wangu anawaita uncle lakini huwez amini siku amekutana na mtoto wangu sinza makaburini akamwambia Mambo ya uncle weka pembeni naomba simu au la nikupige panga
Si atakua kaishaanza kuzeeka?
 
Back
Top Bottom