Swet-R
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 5,613
- 8,042
Umenikumbusha mbali sana enzi hizo mbeya. Umemsau mwasimba wa nonde. Alikuwepo mwakayugu kipindi hicho stand ya chunya ilikuwa chini hapo karibu na rift Varey hotel. Kipindi hicho dhahabu inatema mbaya chunya,wasukuma walikuwa wanapolwa balaaaa pale stand na akina mwakayugu. Alikuwa anawapora milioni 20,50 kipindi hicho au dhahabu za kiwango hicho ilikuwa kitu cha kawaida. Alikuwa anachomeka nato refu kuanzia kuanzia kwenye buti lake refu,kuja juu kwenye ka-jeans kake ka kubana. Siku moja ilikuwa inapigwa gemu (kamali)kule nyuma mtoni sinde. Mwakayugu akaliwa hela yote,mpaka buti,nguo,akabakiwa na chupi tu. Sasa kulikuwa na mtindo wa aliye-win siku hiyo anawapa arifu aliowala,hiyo arifu ilikuwa kama nauli ya kwendea home. Sasa mwakayugu alipewa arifu ya kwanza akaliwa nayo. Jamaa alie win siku hiyo akamwambia kula mjusi yule nitakupa arifu nyingine. Duuh...! Lile lijamaa mwakayugu lilikuwa kama mnyama hivi. Likaurukia ule mjusi na kuukata na meno,likaanza kuutafuna mjusi bwana. Basi pale karibu wote tulistuka tukataka kukimbia,yule jamaa aliemwambia ale mjusi,akamwambia acha acha acha,chukua hela arifu hii hapa. Aaah...! Wapi jamaa likaendelea tu kuutafuna ule mjusi,likaumaliza. Likainama chini mtoni pale likachota maji na viganja vyake likanywa maji,likachota likanywa,hapo limeliwa kila kitu mpaka nato(kisu kikubwa) lake limebakiwa na njupi tu. Jamaa lilikuwa hatari balaa. Lilipanda juu hivi,bingwa lililojizira zira hivi,likimya,linaongea kwa vitendo tu. Nasikia liko south Africa nownlikuwa na jamaa yangu ananipa visa na mikasa mbali mbali ya Jiji la Mbeya miaka ya 1980s mpaka 1990s. alianza kunambia jinsi ambavyo miaka hiyo vijana wengi jijini mbeya ilikuwa lazima waende GYM, wajifunze Karate/Kung fu au Tae kwon do na michezo mingine mbalimbali ya mapigano.
mwenyeji wangu ananitajia mmoja ya watu anaowakumbuka miaka ile alikuwepo Daud. huyu kwa watu wengi wa Mbeya miaak ile wanamkumbuka jamaa likuwa amejenga mwili na kujichora tattoo kadhaa mwilini mara nyingi akitembea amevaa singlet kuonesha tattoo zake na misuli yake iliyokuwa imejaa vyema kabisa. huyu alikuwa mbabe,ngumi jiwe miaka hiyo akipiga ngumi uliyepigwa unaona kama umepigwa na jiwe zito sana kutokana na kuwa na nakozi kwenye mikono. wengi walikuwa wakizimia kutokana na ngumi alizokuwa akipiga watu.akaendelea kunipa historia ya wababe wengine waliowahi kutokea jijini humo miaka ya kale.
anasema miaka hiyo alitokea jamaa mmoja alikuwa anaitwa Shetani. jamaa alikuwa ana uwezo mzuri sana wa kutembeza kipigo kwa raia na askari kiasi kwamba askari wenyewe walikuwa wakimgwaya sana. alikuwa kwa mbeya mjini yeye ndiye mtemi anayefahamika. na kama hukukubaliana naye ilikuwa ni jambo rahisi tu mnakubaliana siku ya weekend mnaenda kukutana eneo flani kwa ajili ya kutembezeana mkono mpaka apatikane mshindi.
utawala wa huyu bwana ulikuja kukomeshwa na jamaa mmoja ambaye alikuja kupewa jina la yesu. huyu aliitwa yesu baada ya yeye kuja kumtembezea kipigo kikubwa sana huyo shetani. huyu yesu inasemwa kuwa yeye alitokea Zambia. kufika Mbeya mjini akawa amesikia habari hizo za uwepo wa shetani kuwa ndiye mbabe ile kinyama. na ikatokea siku moja wakakutana katika mizunguko ya maisha katika kutunishiana misuli ikaamuliwa zichapwe.
msimualiaji anasema miaka hiyo walipata nafasi ya kushuhudia ngumi kama za kwenye movie live kabisa bila chenga. zilipigwa ile kinyama. mapigo na ufundi mbalimbali mpaka dakika za mwisho shetani alikuwa hoi vibaya sana na kuamua ku surrender. ndipo yule mbabe mpya alipopewa jina la yesu.tofauti na shetani wanasema huyu yesu alikuwa ni mstaarabu hakuwa akionea watu au kufanya mambo kibabe.
hayo ni mambo ya Jiji la Mbeya miaka hiyo. pamoja na kuwepo pia wababe wengi maeneo mbalimbali jijini humo hasa akisema maeneo kama machinjion,sisimba,sinde,meta,soko matola,mwanjelwa n.k
nikakumbuka miaka ya 200s dar es salaam alikuwepo jamaa mmoja naye shababy sana al maarufu kwa jina la van dame wa sinza. huyu jamaa nilishasikia sana habari zake miaka hiyo na kwa bahati mbaya mimi umri wangu ulikuwa umeshasogea sogea sikuwa naendelea tena na mchezo nliokuwa nikiupenda wa MMA. maana nlijifunza kung fu, nilikuwa mzuri kwenye Katare na kiasi judo. hii ilinipelekea pia nicheze michezo mingi kama Kick Boxing n.k miaka hiyo ya nyuma.
Van Dame alikuwa anasifika sana kwa uwezo mzuri aliokuwa nao wa kurusha mateke. na wepesi katika kuruka na kukimbia inapohitajika. polisi wengi walikuwa wakimgwaya na hata hawakuwa wakitamani kwenda mkamata maana alikuwa na uwezo wa kuwatembezea kipigo kikubwa sana hata wakarudi kituoni wakiwa hoi na wenye hali mbaya kimwili.
tatizo kubwa la Van Dame lilikuwa nasikia ni usela choo mwingi sana. alikuwa akikaba watu au kupora vitu vya thamani na ilikuwa akikufanyi hivyo huna cha kumfanya . ukimpeleka polisi wataishia tu kuandika maelezo na kuanzia hapo wao ndo wanaanza kumkwepa ili wasije wakajikuta wapo katika mazingira ambayo walipaswa kumshika halafu ikawa ngumu.
hivyo polisi wenyewe ikawa ukiwaambia vn dame nimemwona mwenye .... au kijitonyama.. basi siku hiyo polisi hawakanyagi kabisa maeneo ya huko. hali ilikuwa ikizidi sana wanaenda kumwomba aende kituoni naye atawaambia basi haina shida ntakuja baadaye au kesho.
van dame wanasema alikuwa mbabe kinyama.... sifahamu mwishowe aliishia wapi lakini ni mmoja ya watu ambao walikuwa na sifa lukuki katika sanaa za mapigano.
JE MKOANI MWAKO ALIKUWEPO NANI MBABE NA SASA YUPO WAPI? TUENDELEE KUJULISHANA HAYA MAMBO YA KIBABE... KWA SASA UTU UZIMA NA KAZI ZETU HIZI ZINATUZUIA SISI WENGIE TUSIISHI MAISHA HAYA. LAKINI KIUKWELI NI MAISHA AMBAYO MIMI HUWA NAYAMISS SANA. NA ILIKUWA NGUMU KUSIKIA WANAKUWEPO AKINA JUMA LOKOLE... sababu wanaume ilikuwa ni kugangamaa toka ukiwa mdogo. unakua kiume hasa. siku hizi watoto wanavaa mlegezo?
zamani ungevaa mlegezo kuna mbabe mmoja angekuita na kukwambia asikuone tena unakanyaga mtaani KWAKE ukiwa umevaa hivyo sababu next time atakugonga makwenzi kinyama mpaka akili yako ikae sawa. au akuone unatembea kishoga shoga... angekucharaza viboko na kukwambia asikuone tena mtaani unachafua hali ya hewa.
GuDume Bujibuji Mshana Jr Chizi Maarifa @ na wadau wengi wenyeji wa dar na mikoa mingine. Hasa Arusha Macharliee mtupe habari za wababe waliowah kuwepo na walipo mpaka sasa.