Uzoefu wangu kwa wachangia mada JF

Amavubi

JF-Expert Member
Dec 9, 2010
30,141
13,215
1. Ukiona umerusha mada ikaanza kuchangiwa kwa kuungwa mkono ujue mwisho wake huenda ikaishia kwa kupingwa sana... Hii huenda nachangiwa na kwamba kuna wachangiaji wamejipanga kiitikadi yaani kama uzi utaelekea chama fulani basi atakeyanza inategemea ni wa chama chenye mrengo wa kuunga mkono hoja ama kupinga na baada ya uda wataanza mapovu wenye itikadi nyingine. Kiitikadi hapa namaanisha hata wapenzi wa mpira na dini wamo humo.

2. Wapo wanaosoma tu kichwa cha habari na kwenda mja kwa moja uzi ulipoishia ili achangie msimamo wake.

3. Kuna watu wameumbiwa kuponda tu mada hata iwe ya mrengo gani

4. Mustakabali wa kuweka au kupewa Like hautabiriki inagwa wengi hufanya kwa malipizi, yaani kama kwake huweki na kwako haweki japo pia wapo wanaweka kwa kuangalia umaarufu/nafasi/itikadi ya mtu maana imenenwa kila mtu na mtuwe.

5. Wachangiaji wengi wa usiku ndi huchangia kimashiko ilihali wale wa mchana wengi ni kama wapita njia tu.

6. Kauzoefu kangu kanaonyesha wakongwe/maarufu hata waanzishe thread au kuchangia pumba husifiwa tu na km ni kukosolewa basi ukosolewa kwa heshima.

7. Sasa wewe ambaye siyo maarufu andika thread ya maana husifiwi kivile na km umeandika pumba tegemea kutukanwa kila sina ya tusi. Utasikia Rudi Facebook.

8. Na tupo ambao wa tunapita tu bila kuacha hata comment kama hatupo vileUZI HUU NI LIVING NA UTAKUA UKIJAZIWA KADRI UTAFITI UNAVYOIBUA..

Wewe umegundua nini?
 
Kauzoefu kangu kanaonyesha wakongwe/maarufu hata waanzishe thread au kuchangia pumba husifiwa tu na km ni kukosolewa basi ukosolewa kwa heshima

Sasa wewe ambaye siyo maarufu andika thread ya maana husifiwi kivile na km umeandika pumba tegemea kutukanwa kila sina ya tusi
Utasikia Rudi Facebook
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom