Uzoefu wangu kuitwa na Kamati ya Bunge: Japo ameitwa kwa dharau, kwa kutishiwa pingu, lakini kiukweli CAG ameheshimiwa sana!

Sasa Paskali Assad ni Profesa NA tena ni Alhaj, hii maana yake ni kwamba anakubalika kote Mbinguni na Duniani kwa viwango vya juu lazima aheshimiwe.

Wewe na Mdee na huyo aliyewaita mnakubalika hapa duniani tu tena kwa kiwango cha vidigirii tu hata udaktari wa falsafa hamna ni halali yenu kuitwa kama aitwavyo PUSI aka Nyau.

Prof alhaj Assad ni level nyingine mkuu......... Na huo ndio ukweli mchungu!
Kwa mtu mwenye hekima na busara kila binadamu anastahili kuheshimiwa bila kujali hadhi yake katika jamii. Ila kwa mpumbavu daima hujiona yeye ni bora kuliko wengine utadhani minyama yake haitarudi udongoni
 
Wanabodi,

Japo CAG ameitwa na Spika kwa dharau kwa kutishiwa kuletwa kwa pingu, lakini nikilinganisha na mimi nilipoitwa na kamati hiyo, kiukweli kabisa CAG ameheshimiwa sana haswa kwa ile tuu kuitwa na kutajiwa tarehe ya wito.
My Story.

Tangu nilipoitwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kwa kosa kama la CAG la kulidhalilisha Bunge, sijawahi kuleta mrejesho wa nini kilijiri katika mahojiano hayo, na huu sio mrejesho bali ni uzoefu tuu wa kulinganisha kuitwa kwangu na kuitwa kwa CAG.
Chanzo cha Mimi Kuitwa.

Mimi niliuliza tuu humu jf kama " Jee Bunge Linajipendekeza kwa serikali?..". Gazeti lika peak na kuiifanya ni headline story ila alama ya kuuliza ikiwemo.

Mhe. Mbunge mmoja kama vile ni kilaza fulani, akaibuka na gazeti bungeni, akaisoma headline as a statement bila kuweka alama ya kuuliza.

Ndipo Spika akalipokea.

Spika na Maneno Mbofumbofu!.
Hata mimi nilipoitwa, Spika alitamka maneno fulani ya hovyo hovyo kunihusu ambayo hayahusu, ila kwa vile mimi ni nobody, maneno ya hovyo hovyo ya Spika kwa someone who is nobody, didn't matter much, lakini kumuita GAG kwa maneno ya kumtishia kwa pingu, kiukweli kabisa, it was uncalled for. Bunge letu lisikubali udhaifu binafsi wa viongozi wa Bunge kulifanya Bunge lidharauliwe. Mhe Spika nae ni binadamu tuu kama sisi na sio malaika, hivyo anaweza kukosea kubinaadamu tuu, lakini tusikubali kuutetea udhaifu binafsi wa kibinadamu kwa kuuoanisha au kuuingiza kwenye uspika wa Bunge letu tukufu.

GAG Kapewa Muda wa Kutosha, Hii ni Heshima Kubwa.
Mimi nilipoitwa na Spika, alitangaza tuu Bungeni kuwa tutaitwa, lakini hakutangaza siku. Lakini kuitwa kwa CAG, tangu ile Press Conference, Spika ameitaja tarehe 21 Jan.

Barua Rasmi ya Wito.
Mimi tangu nilipotangwa kuitwa hadi kupewa barua, kilipita kipindi kirefu, lakini CAG kaitwa kwa kupangiwa tarehe tayari na baada ya siku 3, amepelekewa barua rasmi akiwa na siku zaidi ya 10 za kujiandaa kabla hiyo tarehe ya kuhojiwa.

Mimi niliitwa Ofisi ya ndogo ya Bunge na kukabidhiwa barua ya wito saa 9:00 mchana wa leo, kuifungua barua unatakiwa uwepo viwanja vya Bunge kesho yake asubuhi. Sasa mtu unajiuliza huu wito wa saa 9:00 mchana, kutakiwa Dodoma asubuhi ya siku inayofuata kwa usafiri gani wa public transport?!, unless kila anayeitwa kuhojiwa na kamati ya Bunge ana assume perliamentarian status anakuwa na shangingi, anajaza tuu mafuta na kuelekea Dodoma.

Thanks God, sisi wengine kwetu ni Gambosh, ile kufunga tuu macho, kufungua unajikuta uko Bungeni Dodoma tayari kuhojiwa, umekujaje, umetumia usafiri gani, only God knows!.

Hivyo kuitwa kwa CAG, wengi wanaona kama ameitwa kwa kudharauliwa kwa kutishiwa asipoitika wito, atapelekwa kwa pingu, mimi naamini mtu kama mimi niliyeletewa barua leo na kutakiwa kuripoti kesho yake ningeshindwa ndio pingu zingenihusu, lakini kwa mtu kama CAG kuitwa kwa kutishiwa pingu, is not right at all.

Justification ya Wito.
Mamlaka ya Spika kumsummon mtu yoyote mbele ya kamati kwa kulidharau Bunge yako kwenye sheria na kanuni na sio kwenye katiba. Kinga ya CAG kutokuhojiwa na yeyote zaidi ya Mahakama iko kwenye katiba na kwenye sheria. Inapotokea sheria yoyote ikakinzana na Katiba, Katiba ndio supremacy na sheria inayompa mamlaka Spika kumsummon mtu yoyote ni batili.Tangu lini sheria na kanuni tuu ikaizidi katiba?.

Huku ni sawa na masikio kuzidi kichwa!. Japo Spika amemuita CAG kwa mujibu wa mamlaka yake, lakini mkisikia mambo ya mihimili kujiinua kuvuka mipaka ya mamlaka yake ndiko huku, watu wote wenye kuheshimu katiba na sheria, watamshangaa sana CAG kama ataitika wito huu kwa kuogopa tishio la pingu. Sisi ambao ni washabiki wa kuheshimiwa kwa katiba na kutekelezwa kwa sheria, taratibu na kanuni, tunapenda kuona huu mtanzuko ukimalizika kwa kufunuliwa kwa sheria batili ya mamlaka ya Spika na katiba ikiheshimiwa.

Tunasubiri kwa hamu hiyo tarehe 21, ila kwa sisi waelewa, ukiona watoto wawili wa baba mmoja, mmoja anasema ukweli wa udhaifu wa mwenzake mbele ya baba, halafu yule mwenye udhaifu badala ya kukanusha udhaifu wake ndio kwanza anamtishia mwenzake kuwa atamkomesha, na huku baba amenyamaza kimya tuu, wa kuelewa tumeelewa!.

NB. Naomba msiniulize kilichojiri kwenye mahojiano yale, nawaombeni sana mniruhusu ni reserve my comments.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Paskali
Crystal clear, gotcha.
 
Badala ya kusikitika nimebaki nacheka tu kwa jinsi ulivyowasilisha ujumbe wako , hata hivyo pamoja na kupewa vitisho huko kwenye kamati ya bunge lakini bado msimamo wako umebaki palepale...

Hata hivyo lile swali la kikatiba ulilouliza pale ikulu, litasimama siku zote za utawala huu.!
aliulizajee swali gani mkuu ??
 
Wanabodi,

Japo CAG ameitwa na Spika kwa dharau kwa kutishiwa kuletwa kwa pingu, lakini nikilinganisha na mimi nilipoitwa na kamati hiyo, kiukweli kabisa CAG ameheshimiwa sana haswa kwa ile tuu kuitwa na kutajiwa tarehe ya wito.
My Story.

Tangu nilipoitwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kwa kosa kama la CAG la kulidhalilisha Bunge, sijawahi kuleta mrejesho wa nini kilijiri katika mahojiano hayo, na huu sio mrejesho bali ni uzoefu tuu wa kulinganisha kuitwa kwangu na kuitwa kwa CAG.
Chanzo cha Mimi Kuitwa.

Mimi niliuliza tuu humu jf kama " Jee Bunge Linajipendekeza kwa serikali?..". Gazeti lika peak na kuiifanya ni headline story ila alama ya kuuliza ikiwemo.

Mhe. Mbunge mmoja kama vile ni kilaza fulani, akaibuka na gazeti bungeni, akaisoma headline as a statement bila kuweka alama ya kuuliza.

Ndipo Spika akalipokea.

Spika na Maneno Mbofumbofu!.
Hata mimi nilipoitwa, Spika alitamka maneno fulani ya hovyo hovyo kunihusu ambayo hayahusu, ila kwa vile mimi ni nobody, maneno ya hovyo hovyo ya Spika kwa someone who is nobody, didn't matter much, lakini kumuita GAG kwa maneno ya kumtishia kwa pingu, kiukweli kabisa, it was uncalled for. Bunge letu lisikubali udhaifu binafsi wa viongozi wa Bunge kulifanya Bunge lidharauliwe. Mhe Spika nae ni binadamu tuu kama sisi na sio malaika, hivyo anaweza kukosea kubinaadamu tuu, lakini tusikubali kuutetea udhaifu binafsi wa kibinadamu kwa kuuoanisha au kuuingiza kwenye uspika wa Bunge letu tukufu.

GAG Kapewa Muda wa Kutosha, Hii ni Heshima Kubwa.
Mimi nilipoitwa na Spika, alitangaza tuu Bungeni kuwa tutaitwa, lakini hakutangaza siku. Lakini kuitwa kwa CAG, tangu ile Press Conference, Spika ameitaja tarehe 21 Jan.

Barua Rasmi ya Wito.
Mimi tangu nilipotangwa kuitwa hadi kupewa barua, kilipita kipindi kirefu, lakini CAG kaitwa kwa kupangiwa tarehe tayari na baada ya siku 3, amepelekewa barua rasmi akiwa na siku zaidi ya 10 za kujiandaa kabla hiyo tarehe ya kuhojiwa.

Mimi niliitwa Ofisi ya ndogo ya Bunge na kukabidhiwa barua ya wito saa 9:00 mchana wa leo, kuifungua barua unatakiwa uwepo viwanja vya Bunge kesho yake asubuhi. Sasa mtu unajiuliza huu wito wa saa 9:00 mchana, kutakiwa Dodoma asubuhi ya siku inayofuata kwa usafiri gani wa public transport?!, unless kila anayeitwa kuhojiwa na kamati ya Bunge ana assume perliamentarian status anakuwa na shangingi, anajaza tuu mafuta na kuelekea Dodoma.

Thanks God, sisi wengine kwetu ni Gambosh, ile kufunga tuu macho, kufungua unajikuta uko Bungeni Dodoma tayari kuhojiwa, umekujaje, umetumia usafiri gani, only God knows!.

Hivyo kuitwa kwa CAG, wengi wanaona kama ameitwa kwa kudharauliwa kwa kutishiwa asipoitika wito, atapelekwa kwa pingu, mimi naamini mtu kama mimi niliyeletewa barua leo na kutakiwa kuripoti kesho yake ningeshindwa ndio pingu zingenihusu, lakini kwa mtu kama CAG kuitwa kwa kutishiwa pingu, is not right at all.

Justification ya Wito.
Mamlaka ya Spika kumsummon mtu yoyote mbele ya kamati kwa kulidharau Bunge yako kwenye sheria na kanuni na sio kwenye katiba. Kinga ya CAG kutokuhojiwa na yeyote zaidi ya Mahakama iko kwenye katiba na kwenye sheria. Inapotokea sheria yoyote ikakinzana na Katiba, Katiba ndio supremacy na sheria inayompa mamlaka Spika kumsummon mtu yoyote ni batili.Tangu lini sheria na kanuni tuu ikaizidi katiba?.

Huku ni sawa na masikio kuzidi kichwa!. Japo Spika amemuita CAG kwa mujibu wa mamlaka yake, lakini mkisikia mambo ya mihimili kujiinua kuvuka mipaka ya mamlaka yake ndiko huku, watu wote wenye kuheshimu katiba na sheria, watamshangaa sana CAG kama ataitika wito huu kwa kuogopa tishio la pingu. Sisi ambao ni washabiki wa kuheshimiwa kwa katiba na kutekelezwa kwa sheria, taratibu na kanuni, tunapenda kuona huu mtanzuko ukimalizika kwa kufunuliwa kwa sheria batili ya mamlaka ya Spika na katiba ikiheshimiwa.

Tunasubiri kwa hamu hiyo tarehe 21, ila kwa sisi waelewa, ukiona watoto wawili wa baba mmoja, mmoja anasema ukweli wa udhaifu wa mwenzake mbele ya baba, halafu yule mwenye udhaifu badala ya kukanusha udhaifu wake ndio kwanza anamtishia mwenzake kuwa atamkomesha, na huku baba amenyamaza kimya tuu, wa kuelewa tumeelewa!.

NB. Naomba msiniulize kilichojiri kwenye mahojiano yale, nawaombeni sana mniruhusu ni reserve my comments.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Paskali
Nadhani Prof. Asad akienda itampa sifa kubwa zaidi .
Spika atajinyenyekesha mbele yake sana.
Mana Prof. Asad ni mteule wa Rais mwenye Kinga ya kuitwa na kuhojiwa mambo ya ajabu ajabu kama hayo.

Kwanza Pof.Asad akienda sio kujidhalilisha bali itampa sifa kubwa sana mana itaonyesha ulimwengu wazi jinsi ubinadamu wanavyoweza kuundiwa mashtaka ya uongo chini kwa vitisho.

Baada ya kuitikia witi ndipo Wanaharakati watakapofungua Kesi kuhoji kwa nini spika ametumia mamlaka yake vibaya kumtisha na kumdhalilisha CAG kinyume na katiba.

Spika anataka kuonyesha kuwa uimara wa Bunge ni kuwashughulikia wananchi wanaotoa maoni yao huku likishindwa kuisimamia na kuiwajibisha serikali.

CAG asipoenda spika ataendelea kumtisha kwa sababu spika anajua kiti chake hakiguswi na yeyote nje ya Bunge kwa sababu mpaka sasa hatuoni Chama tawala kikizungumza jambo lolote juu ya CAG kudhalilishwa na kutishwa kama kibaka.
Spika Job anajukwa la kuendelea kumtisha na kumdhalilisha CAG ndani na nje ya Bunge wakati ambapo CAG hana pa kusemea mpaka ahojiwe na vyombo vya habari.
Kumkata kilimilimi Job na baadhi ya bendera fuata upepo walioko ndani ya CCM ni CAG kwenda kwa heshma yote ili amalize mjadala na vitisho.

Pia itakua ni fursa nzuri kwa CAG kuwapa somo ili waone udhaifu wao wakati wa kijadili ripoti aliyoiibua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi,

Japo CAG ameitwa na Spika kwa dharau kwa kutishiwa kuletwa kwa pingu, lakini nikilinganisha na mimi nilipoitwa na kamati hiyo, kiukweli kabisa CAG ameheshimiwa sana haswa kwa ile tuu kuitwa na kutajiwa tarehe ya wito.
My Story.

Tangu nilipoitwa kuhojiwa na Kamati ya Bunge kwa kosa kama la CAG la kulidhalilisha Bunge, sijawahi kuleta mrejesho wa nini kilijiri katika mahojiano hayo, na huu sio mrejesho bali ni uzoefu tuu wa kulinganisha kuitwa kwangu na kuitwa kwa CAG.
Chanzo cha Mimi Kuitwa.

Mimi niliuliza tuu humu jf kama " Jee Bunge Linajipendekeza kwa serikali?..". Gazeti lika peak na kuiifanya ni headline story ila alama ya kuuliza ikiwemo.

Mhe. Mbunge mmoja kama vile ni kilaza fulani, akaibuka na gazeti bungeni, akaisoma headline as a statement bila kuweka alama ya kuuliza.

Ndipo Spika akalipokea.

Spika na Maneno Mbofumbofu!.
Hata mimi nilipoitwa, Spika alitamka maneno fulani ya hovyo hovyo kunihusu ambayo hayahusu, ila kwa vile mimi ni nobody, maneno ya hovyo hovyo ya Spika kwa someone who is nobody, didn't matter much, lakini kumuita GAG kwa maneno ya kumtishia kwa pingu, kiukweli kabisa, it was uncalled for. Bunge letu lisikubali udhaifu binafsi wa viongozi wa Bunge kulifanya Bunge lidharauliwe. Mhe Spika nae ni binadamu tuu kama sisi na sio malaika, hivyo anaweza kukosea kubinaadamu tuu, lakini tusikubali kuutetea udhaifu binafsi wa kibinadamu kwa kuuoanisha au kuuingiza kwenye uspika wa Bunge letu tukufu.

GAG Kapewa Muda wa Kutosha, Hii ni Heshima Kubwa.
Mimi nilipoitwa na Spika, alitangaza tuu Bungeni kuwa tutaitwa, lakini hakutangaza siku. Lakini kuitwa kwa CAG, tangu ile Press Conference, Spika ameitaja tarehe 21 Jan.

Barua Rasmi ya Wito.
Mimi tangu nilipotangwa kuitwa hadi kupewa barua, kilipita kipindi kirefu, lakini CAG kaitwa kwa kupangiwa tarehe tayari na baada ya siku 3, amepelekewa barua rasmi akiwa na siku zaidi ya 10 za kujiandaa kabla hiyo tarehe ya kuhojiwa.

Mimi niliitwa Ofisi ya ndogo ya Bunge na kukabidhiwa barua ya wito saa 9:00 mchana wa leo, kuifungua barua unatakiwa uwepo viwanja vya Bunge kesho yake asubuhi. Sasa mtu unajiuliza huu wito wa saa 9:00 mchana, kutakiwa Dodoma asubuhi ya siku inayofuata kwa usafiri gani wa public transport?!, unless kila anayeitwa kuhojiwa na kamati ya Bunge ana assume perliamentarian status anakuwa na shangingi, anajaza tuu mafuta na kuelekea Dodoma.

Thanks God, sisi wengine kwetu ni Gambosh, ile kufunga tuu macho, kufungua unajikuta uko Bungeni Dodoma tayari kuhojiwa, umekujaje, umetumia usafiri gani, only God knows!.

Hivyo kuitwa kwa CAG, wengi wanaona kama ameitwa kwa kudharauliwa kwa kutishiwa asipoitika wito, atapelekwa kwa pingu, mimi naamini mtu kama mimi niliyeletewa barua leo na kutakiwa kuripoti kesho yake ningeshindwa ndio pingu zingenihusu, lakini kwa mtu kama CAG kuitwa kwa kutishiwa pingu, is not right at all.

Justification ya Wito.
Mamlaka ya Spika kumsummon mtu yoyote mbele ya kamati kwa kulidharau Bunge yako kwenye sheria na kanuni na sio kwenye katiba. Kinga ya CAG kutokuhojiwa na yeyote zaidi ya Mahakama iko kwenye katiba na kwenye sheria. Inapotokea sheria yoyote ikakinzana na Katiba, Katiba ndio supremacy na sheria inayompa mamlaka Spika kumsummon mtu yoyote ni batili.Tangu lini sheria na kanuni tuu ikaizidi katiba?.

Huku ni sawa na masikio kuzidi kichwa!. Japo Spika amemuita CAG kwa mujibu wa mamlaka yake, lakini mkisikia mambo ya mihimili kujiinua kuvuka mipaka ya mamlaka yake ndiko huku, watu wote wenye kuheshimu katiba na sheria, watamshangaa sana CAG kama ataitika wito huu kwa kuogopa tishio la pingu. Sisi ambao ni washabiki wa kuheshimiwa kwa katiba na kutekelezwa kwa sheria, taratibu na kanuni, tunapenda kuona huu mtanzuko ukimalizika kwa kufunuliwa kwa sheria batili ya mamlaka ya Spika na katiba ikiheshimiwa.

Tunasubiri kwa hamu hiyo tarehe 21, ila kwa sisi waelewa, ukiona watoto wawili wa baba mmoja, mmoja anasema ukweli wa udhaifu wa mwenzake mbele ya baba, halafu yule mwenye udhaifu badala ya kukanusha udhaifu wake ndio kwanza anamtishia mwenzake kuwa atamkomesha, na huku baba amenyamaza kimya tuu, wa kuelewa tumeelewa!.

NB. Naomba msiniulize kilichojiri kwenye mahojiano yale, nawaombeni sana mniruhusu ni reserve my comments.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Paskali
Hatutakuuliza kwa sababu tunajua uliitikia wito, ukaenda bungeni ukatishiwa na ukatishika kwelikweli ndio maana umefyata mkia! Waelewa tumekuelewa.
 
Nadhani Prof. Asad akienda itampa sifa kubwa zaidi .
Spika atajinyenyekesha mbele yake sana.
Mana Prof. Asad ni mteule wa Rais mwenye Kinga ya kuitwa na kuhojiwa mambo ya ajabu ajabu kama hayo.

Kwanza Pof.Asad akienda sio kujidhalilisha bali itampa sifa kubwa sana mana itaonyesha ulimwengu wazi jinsi ubinadamu wanavyoweza kuundiwa mashtaka ya uongo chini kwa vitisho.

Baada ya kuitikia witi ndipo Wanaharakati watakapofungua Kesi kuhoji kwa nini spika ametumia mamlaka yake vibaya kumtisha na kumdhalilisha CAG kinyume na katiba.

Spika anataka kuonyesha kuwa uimara wa Bunge ni kuwashughulikia wananchi wanaotoa maoni yao huku likishindwa kuisimamia na kuiwajibisha serikali.

CAG asipoenda spika ataendelea kumtisha kwa sababu spika anajua kiti chake hakiguswi na yeyote nje ya Bunge kwa sababu mpaka sasa hatuoni Chama tawala kikizungumza jambo lolote juu ya CAG kudhalilishwa na kutishwa kama kibaka.
Spika Job anajukwa la kuendelea kumtisha na kumdhalilisha CAG ndani na nje ya Bunge wakati ambapo CAG hana pa kusemea mpaka ahojiwe na vyombo vya habari.
Kumkata kilimilimi Job na baadhi ya bendera fuata upepo walioko ndani ya CCM ni CAG kwenda kwa heshma yote ili amalize mjadala na vitisho.

Pia itakua ni fursa nzuri kwa CAG kuwapa somo ili waone udhaifu wao wakati wa kijadili ripoti aliyoiibua

Sent using Jamii Forums mobile app
ingependezaa kama tukio lingekuwaa live kama membe alivyowapa condition wana lumumba mpakaa sasa hawajamuitaa tena
 
Mkuu una maana gani unaposema ASSAD hatoweza kufika katika kamati ya Bunge? Huoni kama italeta machafuko makubwa ya kisiasa?

Ukizingatia Prof. Assad anaonekana kuwa na Adui zaidi ya mmoja.

Sent from my SM-J530F using Tapatalk
 
Back
Top Bottom