Uzoefu wa kusafiri na Rocket kati ya Misri na Afrika ya Kusini

Rocket ni usafiri wa anga kama ilivyo hizi ndege za kawaida na helicopter, lakini Rocket hairuki umbali mrefu sana kutoka usawa wa bahari kama ilivyo ndege ambazo hutembea juu futi hadi 36,000 na speed ya 900km/hr.

Rocket hutoa moshi mzito kutokana na aina ya engine yake ambayo hutaka kufanana na ya train ya mafuta (diesel).

Rocket huruka wima (vertically) tofauti na ndege.

Inasemekana, kwa Afrika kuna viwanja viwili tu vya rocket , cha Johannesburg Afrika ya Kusini na Cairo nchini Misri.

Sifahamu rocket hubeba mizigo au abiria !

Ni usafiri ambao ni wa hatari sana, kutokana na urukaji wake na pia ikianza kutua. Kashkash ni kubwa sana inayoambatana na moto mkali unaoiwezesha Engine kuendesha rocket.


Mwenzangu umewahi kupanda rocket ?

Binafsi nina mpango wa kupanda hii jet aisee View attachment 2074878View attachment 2074879
Kwa kifupi ni kuwa umeandika UTOPOLO
 
wajameni sasa mtoto ameuliza!! nyie mizee mizima na mandevu yenu yenye mvi hayo,,,mnakaponda! nani mjinga kati yenu na yeye??...tulipokuwa wadogo kwa bibi huko vijijini wooote humu!!

tuliambiwa na mabibi zetu zile ni rockets! eti bibi anasema ''sasa hivi wanakunywa chai! na mikate!'''...eti kuna uwanja mmoja tu africa hii Cairo!...utauliza ''na mimi nkiwa mkubwa nitaendesha rockt Bibi??

Bibi ata jibu '''Soma sana ufaulu uendeshe .......mweee!
 
Enzi zile hata mimi niliaminishwa kama mleta uzi kua rocket husafirisha magari meengi na mizigo mizito kati ya misri na S.A.

Daah ila nikaja kujua kumbe ni kutupoteza tu sie madogo wa kipindi kile na ndahani hata wale wakubwa hawakuujua ukweli.
 
Mkuu tangu lini ukasikia rocket inasafirisha watu toka nchi moja kwenda nyingine mkuu? Hapo umeweka picha za rocket na shuttle.

Shuttle NASA washaipiga chini iko kwenye makumbusho nayo ilikuwa haisafirishi watu from nchi moja kwenda nyingine, bali ilikuwa inapeleka mizigo, satelites na wanaanga kwenye space.

Unachoona kama.mstari ni mandege makubwa yanayotumia jet engine. Ule mosho ni difference ya joto na humidity. Yani ni sawa na wewe unavyotoa moshi mdomoni wakati wa abridi kali kama la makete.

Ulichoandika ni story za vijiweni hakuna hata ukweli wowote.
yani nyakati hizi hadi dar mambo ya mvuke mdomoni hadi dar yapo
 
Haya mambo tuliyawaza utotoni baada ya kuona alama mbili za moshi tukadanganyana kwamba hiyo ni rocket na ujinga mwingine kama ulivyoelezea hapo, eti viwanja vipo viwili tu!!!😂😂😂

Unaandaa kabisa uzi kwa taarifa za uongo na za kitoto!!! 😂

🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮🚮
 
Jamani Dunia imebadilika na Kukua sana haswa ki sayansi . Vichwani mwetu tunazo Stori Nyingi sana za Vijiweni ambazo tulisimuliwa na Kuziamini. Kwa hiyo Kabla ya Kupost kitu kwenye Watu wengi jitahidi uingie GOOGLE Ili uweze kujiridhisha na Kuongeza Ufahamu.
 
Mtoto: Baba, ni kipi kinafanya ndege ipae angani.?
Baba: eh eh eh mwanangu hayo ni mambo ya kitaalam, kwanza inakupasa usome pia ulale kwenye chandarua chenye dawa ya kuzuia mbu waenezao malaria
😂😂
 
Rocket ni usafiri wa anga kama ilivyo hizi ndege za kawaida na helicopter, lakini Rocket hairuki umbali mrefu sana kutoka usawa wa bahari kama ilivyo ndege ambazo hutembea juu futi hadi 36,000 na speed ya 900km/hr.

Rocket hutoa moshi mzito kutokana na aina ya engine yake ambayo hutaka kufanana na ya train ya mafuta (diesel).

Rocket huruka wima (vertically) tofauti na ndege.

Inasemekana, kwa Afrika kuna viwanja viwili tu vya rocket , cha Johannesburg Afrika ya Kusini na Cairo nchini Misri.

Sifahamu rocket hubeba mizigo au abiria !

Ni usafiri ambao ni wa hatari sana, kutokana na urukaji wake na pia ikianza kutua. Kashkash ni kubwa sana inayoambatana na moto mkali unaoiwezesha Engine kuendesha rocket.


Mwenzangu umewahi kupanda rocket ?

Binafsi nina mpango wa kupanda hii jet aisee View attachment 2074878View attachment 2074879
Daaah!
 
You seem to be well educated and exposed. Umeelezea kisayansi na ukweli kwenye kila kitu.

Hii ndio tunahitaji kwenye JF sasa zitaanza comment za chura, sijui mapunga wataharibu Uzi sasa hivi, Kuna kizazi fulani kimakuja Kuna wapumbavu wengi sana, hawawezi kuongea bila kuanza kutaja kufirana na mambo ya ushoga.

Yani wanaanzisha mada ndani ya mada na inapoteza kabisa lengo la thread.
Mashoga njia nyingi sana kufikisha ujumbe kama hivi...
 
Back
Top Bottom