Liverpool_Jr
JF-Expert Member
- Sep 7, 2019
- 1,220
- 1,411
Duh una moyo..Kutokana na hali Ngumu ya maisha na tatizo la ajira vijana wengi tumeamua kurudisha mpira kwa kipa huku tukisubilia mambo yakae sawa tujipange upya na sis tufanye maisha yetu kama awali.. Wengine wamerudisha mpira kwa wazazi wao, wengine wamerudisha mpira kwa Ndugu, ila sisi Ma Pro na Ma Legendary tumerudisha mpira kwa mashemeji zetu walipo olewa dada zetu na hatujali..
Kama ilivyo kawaida kila kitu kina kanuni, sheria na taratibu zake endapo ukizifata zitakusaidia sana jins ya ku survive kipindi hichi kigumu cha mpito. Haya ni mambo muhimu sana ya kuzingatia pindi unapo rudisha mpira kwa shemeji yako.
1. Usipige Gym. Gym inamfanya mtu awe na confidence sana hivyo kupelekea kuingilia ugomvi pindi Shem wako anapo mkata dada yako makofi.. Pia Gym hufanya kiwango cha kula kuongezeka ivyo unapo kaa kwa mtu jitahidi sana uwe una kula kiasi kama wenyeji ulio wakuta..
2. Kamwe usije ingilia Ugomvi wa dada yako na shemeji yako pindi wakikusana/ kuzozana au hata kurushiana makofi.. Jitahidi sana kubaki chumbani kwako jifanye kama hujasikia kitu.. Ugomvi wa mke na mume always unakuwa ni wa muda tu lazima watapatana.. Vip kama uliingilia? Itakuwa ndio mwisho wako kukaa kwa shemeji..
3. Kin'gamuzi kikiisha either Dstv or Azam mwambie dada yako amwambie Shemeji yako / mme wake.. Hili litafanyika kwa haraka zaidi sababu Shemeji yako atajua ni kwa ajiri ya mke wake.. Wew shughulika na mambo kama Luku zikibakia unit chache mjuze shemeji yako hii itasaidia akuone active sana mfatiliaji..
4. Siku za weekend shemeji yako akiwepo jitahidi sana usishinde sebleni kwenye Tv. Hata ukiwa seblen basi jitahidi kukaa mbali na remote.. Sababu wengi huwa wanapenda weekend kuinjoi na familia zao wew pale unahesabika kama mzigo na sio part ya familia only dada yako anakuona memba wa familia..
5. Kamwe usije kuwa shabiki wa Team tofauti na anayo shabikia Shemeji yako. Hii huwa inajenga sana chuki hivyo ili uishi kwa aman kuwa team moja na shemeji yako .. Pia jitahidi sana kumsifia sifia.. Kama ana gari pia jitahidi sana kusifia gari yake ajue ndio dream car yako hata kama ni starlet or Vitz.
6. Usiwe unaleta marafiki zako nyumbani kwa shemeji yako.. Jitahidi sana wanao wote muwe mnakutana nje uko.. Sababu shemeji yako. Mashemeji zetu huwa wanaona sisi tunao kaa kwao kama tumesha feli maisha.. Ivyo huwa wana hisi hata marafiki zetu ni wale walio feli maisha wanawaona ni wezi tu.. Hivyo jitahidi sana kutopeleka marafiki kwa nyumbani kwa shemeji yako.
7. Jitahidi kila ukikaa kimaongezi na shemeji yako mwambie kuna Interview fulani nilipiga wamesema watanipigia simu ivyo nasubilia waniite.. Hii itampa moyo sana shemeji yako atajua soon ukipata kazi utaondoka kwake na ukakae kwako..
NB: Kama kijana usione aibu kurudisha mpira kwa kipa mambo yanapo kuwa magumu sababu kila mtu na maisha yake. Maneno yapo tu binadamu huwa hakosi cha kusema.. Na always mambo huwa yanabadilika hivyi ishi maisha yako.
Hii dhana ya kutuona watu tunao kaa kwa mashemeji zetu ni watu wadhaifu ife leo, Sababu baadhi yetu tumesha pitia mambo magumu na struggle za kila aina na tumesha wai shika hela ambazo wengine mbaka mnakuja kufa haiji tokea ukazishika kwa mkupuo.
Dada angu kaolewa huko pwani.
Nikienda kumsalimia hata kulala siwezi.
Nafika asubuhi jioni nasepa.
Sina maana mbaya ila KULALA KWA SHEMEJI HAPANA SIWEZI..
#YNWA
Sent using Jamii Forums mobile app