Uzio Mrefu Wa Nyumba! Wamwogopa Nani?

kaisa079

Member
Nov 16, 2007
20
0
:(
Kama unaishi katika nyumba iliyozungushiwa uzio ,tena na wengine wanaweka ‘electrical security system’ na Mageti makubwa na walinzi milangoni hivi umewahi kufikiri ni kwa nini uliamua au mzazi wako aliamua kuweka uzio?.Waweza sema ni kwa ajiri ya ulinzi wako mwenyewe na usalama wa mali,hiyo ni mojawapo ya fikra,ila umewahi kufikiri kama mimi nnavyofikiri?
Ni kawaida kuona watu wako katika magari ya ‘tintled’ wasionekane,acha hawa wenye uzio mrefu wa nyumba,hivi kweli imefikia hatua binadamu tunaogopana kiasi hiki?.Yaani watanzania ka watanzania tunaogopana? Why? Kwa nini? Jibu ni TOFAUTI KUBWA ZA KIMAISHA kati ya walionacho na wasionacho! Leo wenye nacho inabidi waweke uzio kuwazuia wezi au vibaka,vibaka na wezi ambaowameamua kuwa wezi kwa kuwa kuna mgawanyo usio sawasiwatetei kwa matendo yao,lakini sku moja nliwahi kuporwa nauli yangu katika mtaa wa kongo na kibaka,bahati mbaya kwake na nzuri kwangu nilimshika mkono wake alokuwa akupenyeza mfukoni mwangu,huweziamini niliuwa na 500 kama nauli ya kunifikisha uswahilini nilikoishi,nilimuangalia sana Yule kibaka,kasha nikagundua alionekana hajapata japo Break Fast mmh! Nikaamua kutafuta chenji nikamgawia 250 hii ni kwa sababu niligundua ni hali ngumu ya maisha ilimsukuma kunipora na hata kama angeenda kwa Matajiri waliozoea kujizolea misifa mikubwa kwa kutoa msaada kwa vikundi mbalimbali huku wakiambatana na waandishi wa habari wakawarushe katika ‘news’ asingepewa hata sumuni.Na iwapo nisingempa fedha shida ilomfanya aibe bado ingebaki pale na labda ‘victim’ mwingine angekwa ndugu yako!Jao sijui kama siku hiyo hakumuibia tena mwingine lakini jambo nialosisitiza hapa ni kuwa kwa kuwa hakuna mgawanyo sawa wa rasilimali ni lazima vibaka watakuwa wengi,majambazi watakuwa wengi na wenye nazo watazidi kuweka nyaya za umeme mpaka katika vioo vya magari ili kibaka akiguswa anaswe.
Hebu fikiria kama wote tungekuwa na mali kwa kiwango kinacholingana japo bado wangekuwapo akina ‘Yuda Iskarioti’ wengi wenye tama,lakini angalau huku kuogopana kusingekuwepo,imefikia hatua hata ukimsimaisha ‘bosi’ Fulani kumpa hi first impression yako kwake ni ‘Kibaka’
Hebu tusiogopane jama,kama hawa ‘matawi ya juu’ wanajiwekea mageti bwana acha sisi tuendelee kusaidiana chumvi,maharage na moto wa kuwashia mkaa huku kwetu uswahilini,ila wananiudhi saa hawa watu siku hizi wameanza kutufuata nakujenga na kujiwekea mageti hukuhuku uswahilini kwetu.Mbona mwatufuatafuta? Kwanza mlituona vibaka tukawapisha huko kwenye majina ya kizungu..sijui nini nini ….‘beach’,sijui nini nini…..’bay’,sijui nini nini …’panga’!
Tusichukiane wale iliowagusa hii ni haki yangu kusema ninachojisikia,’uhurumaoni’.Acha niishie hapa niwahi kibaruani bwana nsije nikaonwa nam Kibaka.Tajiri akinilipa kaujira nika save kidogo nitarudi tena hapa internet café nikupe mchapo mwingine.
Kwa maoni,Ushauri
Niandikie
Kaisa079@yahoo.com
 
mmmhh, mtu anaweka uzio mkubwa, juu anaweka nyaya za umeme, geti anaweka refu utafikiri la yard ya malori, mlango wa barazani anaweka mlango wa chuma, kisha mlango wa mbao kisha kwa ndani anapitisha bomba kama mbili kuuzuia huo mlango wa mbao. Kisha cha kushangaza, madirisha nayo yamezibwa kwa nondo kibao.

Sasa unategemea huyo mtu moto ukiwaka, ni jirani gani ataweza kubeba walau ndoo ya mchanga kwenda kuuzima, au ni jirani gani ataenda kufungua hiyo milango (from outside) kuwaokoa wahanga wa ajali hiyoooo ya moto. Jamani, ndio tujizuie na wezi, but sio mpaka kuwakosesha majirani nafasi ya kutuokoa pindi panapotokea tatizo.

Kama ni swala la ulinzi, basi fuga mbwa wa kutosha, plus weka walinzi wa mkataba (i.e. walinzi wa uhakika).

Hayo ni maoni tu, matajiri msiniangukie kwa matusi bureeee...!!
 
kaisa komaa kaka unaandika post na kujipa thank mwenyewe then unajipongeza kwenye post ya chini yake. U write a good message but you make me doubt your credibility. Usijikweze waccha wengine ndio wakukweze. Unakumbuka ule msemo Kila ajikwezaje.............
 
Unatisha kaka kwa kuandika,wewe ni mwandishi wa habari au mwanasiasa? umelonga mambo ya kweli

Vipi, ulisahau kutumia ID yako nyingine humu JF? any way mko wengi sio wewe peke yako. Kwako wewe ilikuwa ni siku yako ya 40, lazima utoke kama ulivyo.
 
Huyu kachemsha kweli kweli anaandika post na kujipa THANK mwenyewe.

Hawa ndio wale walioji -REGISTER mara mbili mbili kwa majina tofauti sasa huyu arobaini yake imefika kataka kujipa thank kwa jina lingine kakosea na kujikuta kajipa thank kwa jina lile lile alilotumia post.

Kuweni makini jamani.
 
Another One Bites the Dust!!!

Je huu ni mojawapo ya "ufisadi" tunao ukataa kata kata nchini mwetu?!

ha ha ha ha....ama kweli, wahenga walisha tuambia "ndege mjanja hunasa kwenye tundu bove"



SteveD.
 
Nilikugusa nini mzee maana naona umeamua kunipaka waziwazi hata hivyo poa toa huu uhuru maoni kama nimekugusa kwa msg yangu usijali hujauliza ilikiwaje hiyo shavu nikajirulishia enewei kwa kuwa ilikuwa siku yangu ya kwanza kupost makala nilikuwa najaribu kucheki maoni yataapia vipi.Usimind mtu wangu tuko pamoja
 
Nilikugusa nini mzee maana naona umeamua kunipaka waziwazi hata hivyo poa toa huu uhuru maoni kama nimekugusa kwa msg yangu usijali hujauliza ilikiwaje hiyo shavu nikajirulishia enewei kwa kuwa ilikuwa siku yangu ya kwanza kupost makala nilikuwa najaribu kucheki maoni yataapia vipi.Usimind mtu wangu tuko pamoja

Haingii akilini hata kidogo!!! kuwa mkweli, admit.
 
kaisa ni ustaarabu kuomba radhi na kusema hukufahamu porojo zingine hazibadilishi kuwa ulijaribu kujikweza. Admit tuendelee kukata issues
 
mmmhh, mtu anaweka uzio mkubwa, juu anaweka nyaya za umeme, geti anaweka refu utafikiri la yard ya malori, mlango wa barazani anaweka mlango wa chuma, kisha mlango wa mbao kisha kwa ndani anapitisha bomba kama mbili kuuzuia huo mlango wa mbao. Kisha cha kushangaza, madirisha nayo yamezibwa kwa nondo kibao.

Sasa unategemea huyo mtu moto ukiwaka, ni jirani gani ataweza kubeba walau ndoo ya mchanga kwenda kuuzima, au ni jirani gani ataenda kufungua hiyo milango (from outside) kuwaokoa wahanga wa ajali hiyoooo ya moto. Jamani, ndio tujizuie na wezi, but sio mpaka kuwakosesha majirani nafasi ya kutuokoa pindi panapotokea tatizo.

Kama ni swala la ulinzi, basi fuga mbwa wa kutosha, plus weka walinzi wa mkataba (i.e. walinzi wa uhakika).

Hayo ni maoni tu, matajiri msiniangukie kwa matusi bureeee...!!
👏👏
 
Back
Top Bottom