JamiiForums
JF Official Account
- Nov 9, 2006
- 6,202
- 4,996
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UZINDUZI WA AWAMU YA PILI YA SHINDANO LA “STORIES OF CHANGE”
Jamii Forums (JF) ni Asasi ya Kiraia iliyosajiliwa kisheria kufanya uchechemuzi wa Haki za Kidigitali, Demokrasia, Uwajibikaji na Utawala Bora. Vilevile, JF inaratibu jukwaa la JamiiForums.com ambalo ni maarufu duniani kwa maudhui ya Kiswahili na tovuti namba moja ya Kitanzania kwa wingi wa watembeleaji.
Katika kuhamasisha uandishi wa maudhui bora na yenye tija mtandaoni, kuhakikisha mtandao unabaki mahali salama ambapo umma unaweza kupata habari/taarifa bora, JamiiForums ilibuni shindano liitwalo Stories of Change linalolenga kuwapa nafasi raia wote wenye uwezo wa kutayarisha maudhui kushiriki uandishi wa maudhui mtandaoni wenye kuleta mabadiliko.
Shindano hili linakusudia kuongeza maudhui bora mtandaoni hususani ya lugha ya Kiswahili kwa ajili ya vizazi vya sasa na vya baadaye. Pia, shindano linalenga kuhamasisha ushiriki wa raia yakiwemo makundi yasiyopewa vipaumbele kama watu wanaoishi na ulemavu kushiriki katika ukusanyaji na utayarishaji wa taarifa nchini.
Awamu ya kwanza ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2021 ambapo jumla ya wananchi 1,509 walishiriki na kuandika jumla ya stori 1,536 na 936 kati yao kupitishwa kuingia kwenye shindano. Maudhui yaliyoshindanishwa yalihusu Maisha na Jamii (264), Uchumi, Ujasiriamali na Biashara (237), Utawala Bora (124), Afya (97), Elimu (83), Sayansi na Teknolojia (48), Kilimo na Ufugaji (33), Mahusiano (25), Mazingira (23) na Dini/Imani (2).
Washindi bora watano walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba 2021.
Miongoni mwa maudhui yaliyowasilishwa yameweza kuleta mabadiliko katika mfumo wa utoaji huduma katika taasisi za Serikali huku baadhi ya taasisi zikipokea mapendekezo na kuahidi kufanyia kazi.
Katika kuhamasisha uandishi wa maudhui bora na yenye tija mtandaoni, kuhakikisha mtandao unabaki mahali salama ambapo umma unaweza kupata habari/taarifa bora, JamiiForums ilibuni shindano liitwalo Stories of Change linalolenga kuwapa nafasi raia wote wenye uwezo wa kutayarisha maudhui kushiriki uandishi wa maudhui mtandaoni wenye kuleta mabadiliko.
Shindano hili linakusudia kuongeza maudhui bora mtandaoni hususani ya lugha ya Kiswahili kwa ajili ya vizazi vya sasa na vya baadaye. Pia, shindano linalenga kuhamasisha ushiriki wa raia yakiwemo makundi yasiyopewa vipaumbele kama watu wanaoishi na ulemavu kushiriki katika ukusanyaji na utayarishaji wa taarifa nchini.
Awamu ya kwanza ya shindano hili ilifanyika kuanzia Julai hadi Oktoba 2021 ambapo jumla ya wananchi 1,509 walishiriki na kuandika jumla ya stori 1,536 na 936 kati yao kupitishwa kuingia kwenye shindano. Maudhui yaliyoshindanishwa yalihusu Maisha na Jamii (264), Uchumi, Ujasiriamali na Biashara (237), Utawala Bora (124), Afya (97), Elimu (83), Sayansi na Teknolojia (48), Kilimo na Ufugaji (33), Mahusiano (25), Mazingira (23) na Dini/Imani (2).
Washindi bora watano walikabidhiwa zawadi mbalimbali katika hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Oktoba 2021.
Miongoni mwa maudhui yaliyowasilishwa yameweza kuleta mabadiliko katika mfumo wa utoaji huduma katika taasisi za Serikali huku baadhi ya taasisi zikipokea mapendekezo na kuahidi kufanyia kazi.
Awamu ya Pili (2022)
Kutokana na mafanikio yaliyopatikana katika awamu ya kwanza ya shindano, JamiiForums ikishirikiana na Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano kwa Umma, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (SJMC) na Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) imeandaa Awamu ya Pili ya Shindano la “Stories of Change” litakaloanza Julai 15, 2022 na kuisha Septemba 14,2022.
Vigezo na masharti ya kushiriki katika shindano hili:
- Mshiriki anatakiwa kutayarisha andiko linalochochea mabadiliko kwenye nyanja za Elimu, Biashara/Uchumi/Ujasiriamali, Afya, Utawala Bora, Demokrasia, Kilimo, Sayansi na Teknolojia na Afya.
- Andiko liwe kwa lugha ya Kiswahili lenye maneno kati ya 800 - 1000.
- Machapisho yanatakiwa kuwa habari au makala halisi zisizowahi kuchapishwa sehemu nyingine yoyote. Ubwakuzi (Plagiarism) hautaruhusiwa
- Matumizi ya picha au video yanaruhusiwa ili kushibisha andiko. Endapo picha na video sio za mshiriki atalazimika kutaja chanzo
- Mshiriki anaweza kutumia jina la kubuni ‘pseudonym’ lakini atatakiwa kutoa taarifa binafsi endapo ataibuka mshindi
- Watendaji wa Jamii Forums na ndugu zao wa karibu hawaruhusiwi kushiriki kwenye shindano hili
- Mtanzania yeyote mwenye umri wa miaka 18 na zaidi anaweza kushiriki, lakini ili kuchapisha Makala yake itamlazimu kuwa mwanachama wa JamiiForums.
- Maandiko yawasilishwe kati ya Julai 15 – Septemba 14, 2022 kwenye jukwaa la “JF Stories of Change” (Stories of Change )
- Baada ya kuweka andiko jukwaani, mshiriki atatakiwa AJITAHIDI kushiriki kwenye mjadala utakaotokana nalo kwa kutolea ufafanuzi hoja zitakazoibuka ili kuupa mjadala uhai na kuwashawishi wanachama kumpigia kura.
Upatikanaji wa Washindi
Washindi watapatikana kwa kuzingatia kura zitakazopigwa kwenye mnakasha (thread) husika (30%) na pia uamuzi wa jopo la majaji (70%).
Washindi watatangazwa kwenye jukwaa la JamiiForums “Stories of Change” na kurasa za Jamii Forums katika mitandao ya kijamii (Twitter, Facebook, Instagram na Telegram) na si vinginevyo
Zawadi Kwa Washindi zitakuwa kama ifuatavyo:-
Mshindi wa Kwanza atapata fedha taslimu shilingi Milioni 5
Mshindi wa Pili atapata fedha taslimu shilingi Milioni 3
Mshindi wa Tatu atapata fedha taslimu shilingi Milioni 2
Mshindi wa Nne atapata fedha taslimu shilingi Milioni 1
Mshindi wa Tano atapata fedha taslimu shilingi Laki 5
Mshindi wa Sita Mpaka wa Kumi watapata fedha taslimu shilingi laki 3 kila mmoja
Mshindi wa Kumi mpaka wa Ishirini watapata fedha taslimu shilingi laki 2 kila mmoja
Imetolewa na;
Jamii Forums
Masharti na vigezo soma Shindano: Uandishi wa Mtandaoni wenye kuleta tija (Stories of Change 2022)