Uzibaji mashimo barabarani viongozi wa kitaifa wawapo tu ziarani

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,823
35,828
Kuna huu utamaduni uliojengeka wa wahusika kutoshughulika na ukarabati wowote hasa wa barabara hadi viongozi wa kitaifa wanapofanya ziara.

Nimekuwa katika maeneo tofauti siku za karibuni ambako palikuwa na ziara za wakuu tofauti hawa.

Hali ni hivyo hivyo hata kwenye ziara za Waziri Mkuu, Makamu wa Rais nk nk.

Hivi utamaduni huu wa kinafiki hadi lini? Hivi hawa viongozi wetu hawayaoni au kweli wanadanganyika kuwa hali za barabara ndiyo huwa hazinaga mashimo siku zote?
 
Sisi wananchi tungekua tunajitambua,watendaji wazembe kama hao wasingekuwa na nafasi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu wananchi wafanyeje? Alitembelea Rais Ngara, barabara yote mbovu Rusahunga Benako yapata 80km mashimo yalizibwa kwa udongo uliodumu kama wiki 1.

Hivi sasa Samia yuko njiani Shinyanga. Ulizia huko usikie.
 
Back
Top Bottom