Uzi wa vyakula tu

Wakulungwa
JamiiForums1637386431.jpg
 
Nipe utaratibu. Kg 3 kupungua umejitahd sn. Hatua kubwa hy
Kunywa kwanza dawa ya kusafisha tumbo ukae siku moja then unywe dawa ya minyoo.

Dawa ya kusafisha tumbo zipo za kienyeji kama huku kwetu umasaini kuna lodwaa au mukutan (hii mukutan usitumie mswahili unaweza kufa 😂). Au za kisasa tumia castor oil. Dawa za minyoo zipo nyingi.

Maji ya kunywa unachanganya na apple ciser vinegar kijiko cha chakula kwa kila glass. Pia maji unakunywa kwa wingi ili usished water weight uwe una loose fat.

Diet unakula low carb food na fruits mara mbili kwa siku asubuhi na jioni/usiku ila angalau iwe ni masaa manne kabla ya kulala. Unaweza ku refer kwenye picha zangu za last week kuona aina ya vyakula unavyotakiwa. Then kula kwa kiasi sio unakula kumaliza.

Kuhusu mazoezi unafanya cardio mara mbili kwa siku asubuhi na jioni kila siku angalau kwa dakika 45. Ukiweza kufanya jogging na kuruka kamba itasaidia zaidi. Jogging unaweza kufanya kwa mtindo wa ku sprint kwa dakika moja then una jog dakika mbili then una sprint tena dakika moja unarudia hiyo sequence kwa dakika 20 hadi 30. Hii ufanye angalau mara moja ila kama unaweza ufanye asubuhi na jioni.

Kumbuka kuwa cardio/aerobics ni lazima hata kama utakuwa umefanya hii ya high intensity.

Ukimaliza week moja usikimbilie kula high carb foods angalau kwa siku 7 nyingine.

Samaki kipande kimoja kwa mlo mmoja kiwe 140grams kama unaweza kupima ila kama huwezi basi kiwe kidogo tu sio mpande mkubwa. Nyanya mbili medium size. Pia kumbuka vyakula vyako hutakiwi kuweka chumvi wala mafuta.

Picha sina ngoja kuna mtu nimuombe anitumie maana nilimtumia. Akituma nitaweka.

Usipo cheat hapo hata siku moja matokeo lazima yawe chanya. Yani lazima ufanikiwe kwa zaidi ya asilimia 80.

Day 1.
IMG-20210610-WA0024.jpg


Day 2.
IMG-20210610-WA0025.jpg


Day 3.
IMG-20210610-WA0026.jpg


Day 4.
IMG-20210610-WA0028.jpg



Day 5.
IMG-20210610-WA0030.jpg



Day 6.
IMG-20210610-WA0031.jpg



Day 7.
IMG-20210610-WA0029.jpg
 
Nipe utaratibu. Kg 3 kupungua umejitahd sn. Hatua kubwa hy
Pia kuna diet nyingine ya tofauti. Hii nayo unaanza na kusafisha tumbo na kutumia dawa za minyoo.

Procedure za mazoezi ni zile zile isipokuwa kwenye kula sasa hii inakuwa affordable zaidi kwa watu wote maana unakula ndizi mbivu moja na glass ya maziwa fresh (yawe skimmed milk kwakuwa yatakuwa hayana mafuta sana, au kama hutapata skimmed haya ya kawaida unaweka na maji kiasi).

Kula ndizi mbivu moja na glass ya maziwa kisha baada ya lisaa kunywa maji glass tatu kisha baada ya hapo ni dash mpaka tena usiku unarudia hivyo hivyo. Maji haya usiweke kitu kunywa yakawaida ila avaoid kunywa maji ya baridi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom