Uzi wa kutupia hadithi fupi zenye hekima na mafunzo ndani yake

crankshaft

JF-Expert Member
Jun 12, 2019
1,410
3,376
Katika kijiji kimoja alitokea kijana mmoja aliyekuwa mahiri sana katika mchezo wa drafti.
Yoyote aliyejitokeza kucheza naye alimshinda,kutokana na hilo kijana alijawa na sifa majivuni na kiburi.

umaarufu wake ulikuwa mkubwa sana kijijini hapo kutokana na uwezo wake mkubwa wa kucheza mchezo huo na hakutokea mtu yeyote aliyeweza kumfunga kutoka kijijini pale.

siku moja alitokea mzee mmoja kutoka kijiji kingine. Alipofika katika kijiji kile kutokana na umaarufu wa yule kijana alipata kusikia habari zake.

basi mzee akaomba mechi na kijana lakini kijana kwa sababu alikuwa anajiona kuwa mkubwa akasema yeye hachezi na mtu bure ukitaka mechi na yeye lazima umlipe.

kwa bahati mbaya yule mzee hakuwa na pesa yoyote kwa wakati ule lakini alikuwa na punda ambaye alikuwa akimtumia kama usafiri wake.

ikabidi amuweke rehani yule punda ili kama akifungwa kijana atamchukua mpaka atakapompatia pesa zake. Kijana akakubali mchezo ukaanza. Mchezo ukapigwa paleee mwisho wa mchezo kijana akashindaaa.

(inaendelea)
 
Basi kama yalivyokuwa makubaliano ikabidi mzee amtoe yule punda wake.

dah kijana alitamba sana alitembea kijiji kizima akiwa amepanda yule punda kwa majigambo na kujitambulisha kama mfalme wa drafti katika kijiji kile.

baada ya muda kupita yule mzee akaonekana tena pale kijijini. Akamtafuta kijana na kuomba rematch. Kama ilivyo ada kijana hakutaka kucheza bure. Mzee akaahidi kuwa endapo angeshindwa kwa wakati ule angempa kijana pesa nyingi lakini akishinda yeye atamuhitaji tu punda wake.

kijana alimsikitikia sana mzee kwa sababu aliona anaenda kumfilisi lakini kwa sababu aliyataka mwenyewe hakuwa na jinsi.

basi mpango ukapangwa, watu wakakusanyika kushuhudia mtanange huo game ikachezwa, lakini kwa wakati huu mzee alishinda aisee.

kwa mara ya kwanza kijana anapoteza mchezo mbele ya watu aliaibika sanaaa hakuamini macho yake bwana mdogo watu walimcheka sana, heshima yake yote ilipotea siku ile.
(inaendelea).
 
basi kama ilivyokuwa makubaliano yao,ikabidi kijana arudishe punda wa watu kwa sababu ameshindwa.

kijana hakuamini kabisa kama amefungwa. Wakati mzee anajianda kuondoka kijana akamsogelea amuulize aliwezaje kumshinda wakati mechi ya kwanza alimshinda kirahisi tu? Mzee akamjibu "nilikuja hiki kijiji kuna mahali nilikuwa naenda kufuatilia mafao yangu.

Kwa bahati mbaya huko ninakoenda hawaruhusu kwenda na punda hivyo niliposikia habari zako nikaona ngoja nimuhifadhi kwa muda ili nikimaliza nije nimchukue. Leo ndio nimekuja kumchukua farasi wangu"

dah kijana alistaajabu sana kwa majibu yale. Akagundua kumbe hata mechi ya kwanza mzee alijifanyisha tu na sio kwamba halikuwa hajui.

Toka siku ile bwana mdogo aliacha dharau kutokana na funzo kubwa alilolipata.
 
Katika nchi moja kulikuwa na mfalme mmoja,huyo mfalme alikuwa na wafanyakazi wake wawili peter na paul.

siku moja peter alimwona mwenzake paul akiingia ndani ya hekalu la mfalme na kuiba kito cha thamani kutoka katika hekalu lile.

bwana paul akidhani kuwa hajaonekana akaendelea na maisha yake kama kawaida. Basi siku moja peter akamuomba paul amsaidie kazi zake za siku hiyo, paul akakataa kwani yampasa kila mmoja kutimiza wajibu wake.

Ndipo bwana peter akaamua kumwambia kuwa siku ile aliyoiba kwa mfalme alimwona na kama akithubutu kuja kumgomea tena ombi lake atamtaarifu mfalme.

bwana paul kusikia vile alijawa na wasiwasi mkubwa na alilazimika kufanya kazi za watu wawili ili aendelee kuwa salama katika maisha yake pale hekaluni kwani kwa hakika aliijua ghadhabu ya mfalme wao.

maisha ya bwana paul yalikosa furaha, yakajawa na mateso na kutumikishwa kusikokoma kila siku kwa sababu ya kosa lile la siku moja, hakika alijuta sana.

(inaendelea)
 
Mwendelezo... Basi siku moja peter alikuwa na majukumu ya kusomba maji mtoni, akaona asipate tabu sana alimfata paul na kumwomba waende wote mtoni kuteka maji.
Wakiwa njiani peter ametangulia na ndoo ya maji juu ya kichwa chake wakirejea nyumban, Paul ndipo alianza kuingiwa na mawazo ya kishetan ghafla alichomoa kisu kikubwa alichokuwa ameficha na kumvamia peter bila kujuwa. Peter aligongwa mabisu maeneo mbali mbali ya mwili wake.
Peter alianguka kwa kishindo na kupoteza uhai hapo hapo!!. Kuwanzia siku hiyo paul alikuwa huru, hakuwepo tena wa kumuhenyesha kiboya.
{THE END}
 
Mwendelezo... Basi siku moja peter alikuwa na majukumu ya kusomba maji mtoni, akaona asipate tabu sana alimfata paul na kumwomba waende wote mtoni kuteka maji.
Wakiwa njiani peter ametangulia na ndoo ya maji juu ya kichwa chake wakirejea nyumban, Paul ndipo alianza kuingiwa na mawazo ya kishetan ghafla alichomoa kisu kikubwa alichokuwa ameficha na kumvamia peter bila kujuwa. Peter aligongwa mabisu maeneo mbali mbali ya mwili wake.
Peter alianguka kwa kishindo na kupoteza uhai hapo hapo!!. Kuwanzia siku hiyo paul alikuwa huru, hakuwepo tena wa kumuhenyesha kiboya.
{THE END}
Story ya kipuuuuuuuuuuuuuuuuuuzi zaidi hapa JF
 
Paul,siku zote akijulikana kama mfanyakazi mwenye bidii na muaminifu pale hekaluni, alipatwa na tatizo kubwa ambalo lilimlazimu kuiba ili kulitatua. Asijue kwamba anajipeleka katika kifungo na utumwa katika maisha yake.

siku moja aliamua kukaa chini na kutafakari juu ya maisha yale anayopitia. Alichoshwa sana na maisha yale ya utumwa ,mateso na manyanyaso. Akakata shauri ya kwenda kuomba toba kwa mfalme,lolote litakalotokea sawa tu.

basi kesho yake akaenda kwa mfalme kukiri kosa lake na kuomba toba ili aya rudie maisha yake ya zamani. Mfalme baada ya kumsikiliza kwa muda mrefu akamwambia
"paul, kati ya wafanyakazi waaminifu katika ufalme wangu wewe ni namba 1. Huyu mwenzako amekuwa akiniibia mara kwa mara lakini nimekuwa nikimsamehe lakini sikupata kujua kuwa ni mkatili kiasi hiki kwako."

basi mfalme akamsamehe paul na akaamuru yule mfanyakazi muovu, peter atolewe kazini na kupelekwa jela mara moja.

paul alishukuru sana na maisha yake yenye furaha yakarejea tangu siku hiyo.
(mwisho)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom