Uzi maalumu: Wanaotumia Kikuu na Jumia kufanya manunuzi mtandaoni

Asante sana kwa taarifa mkuu
Habari, ndio walicho andika ni sawa na ni waaminifu na wana mawakala mikoani kwahio ukiagiza mzigo watakupigia ukiwa umefika. Shida yao kybwa ni lwba shipping yao ni ya muda mrefu sana. Kuhusu mzigo kufika hakuna cha kulipia ni kuchukua tu.
 
Kikuu kwa sasa wapo vizuri sana haswa kwa upande wa Simu na Accessories wapo vizuri ila sio kwa kununua bidhaa zingine nimeshaagiza simu kama mara kumi hivi na zinakuja vizuri tu sema ku deliver inachukua muda kidogo kama mwezi mmoja hivi mzigo unakuwa nao
 
mi kuna projector nimeipenda natka k
Kikuu kwa sasa wapo vizuri sana haswa kwa upande wa Simu na Accessories wapo vizuri ila sio kwa kununua bidhaa zingine nimeshaagiza simu kama mara kumi hivi na zinakuja vizuri tu sema ku deliver inachukua muda kidogo kama mwezi mmoja hivi mzigo unakuwa nao
uorder vp?
 
Huwa nanunua nguo huko japo huchukua takribani mwezi mmoja kunifikia.
tutapata uhakika gani kama siyo nyiye wenyewe mnajipigia promo hapa. unatakiwa kuwa makini sana unapofanya online shoping. Ndiyo maana nchi nyingine wanaweka middle company ya kulipa.
 
Chukua soda uzi mtaaamu huu
donlucchese
Pole Sana mkuu kwa yaliyo kukuta hiyo ni baadhi ya drawbacks za kufanya manunuzi ya online
Hii Mara nyingi hutokea kwasababu
1. Picha ya bidhaa huwa zinafanyiwa Photoshop na editing hivyo kukufanya uwe na expectations kubwa juu ya uzuri wa bidhaa kuliko uhalisia wa bidhaa yenye hasa ukizingatia manunuzi ya online yame lack touch and feel ya product ukilinganisha na hizi brick-and-mortar
2. Supplier kudeliver product tofauti kabisa hii hasa kwa wale supplier ambao wanapokea order nyingi na weza nikasema Ni makosa ya kibinadamu hutokea yakapelekea kuletewa bidhaa sio

Hizi pamoja na sababu nyingine hupelekea kupata bidhaa ambayo ni tofauti na ulichaagizia ama matarajio yako

Tukija kwenye swala la KiKUU kwa mm binafsi I used to prefer KiKUU kuliko online site nyingine kipindi ambacho KiKUU inaanza kuja Tanzania miaka 2 hivi iliyopita lakini tangu mwaka Jana mwishoni Hadi sasa nimeachana nayo hii ni kwasababu
1. Gharama kuongezeka. KiKUU ya mwanzo ilikuwa haina fees za ajabu Kama sasa. Sasa hivi unakuta bidhaa ni ndogo ila ukienda check out unakuta wameAdd shipping fees na handling fees. Tena usishangaie ukakuta shipping fees and handling fee ni 4times ya Bei ya bidhaa
2. Customer service imekuwa poor. Hasa pale ambapo unakuta ukitrack bidhaa ishafika dar lakini hawajafanya delivery ukiwapigia ama kuchat nao online Hawajibu kwa wakati
3. Huwa Hawa refund cash. Km utafanikiwa kurudisha bidhaa basi mtinyo wako utawekewa kwa K-pay yao ambayo huwezi kuitumia Tena labda kwa bidhaa za ndani ya KiKUU. Kwahiyo Kama ilipanga hela yako ununue viatu ukakosa KiKUU huwezi kuitoa hiyo pesa ukaenda kununua kkoo ama sehemu nyingine.

Licha ya hivyo bado na kushauri utumie KiKUU kwani hizo changamoto Ni common kwa e-commerce site nyingi tuu.
Lakini kwa KiKUU Ni rahisi kudeal nazo.

Kama umeletea bidhaaa mbovu ama huku ipenda claim refund seller akikubali ipeleke shoppers plaza mikocheni kwenye office zao KiKUU na kukurefund kwenye hilo hawanashida

Pia vile vile kabla ya kununua bidhaa hakikisha unaangalia rates za watu na feedback zao kwa hiyo bidhaa ndio ununue. Epuka kununua bidhaa ambayo watu hawaja rate ama kutoa positive feedback

Mwisho kabisa KiKUU kwa Sasa unaweza ukachati ba supplier kabla ya kuplace order. Hii itakufanya km una maswali ama unataka live video ya product husika akufanyie Hata Bei pia unaweza ukabargain
 
Habari wakuu,

Kwa wale wenzangu wa kuorder vitu online, kwa muda murefu nimekua nikifanya manunuzi kupitia mitandao ya Ebay, Amazon na Alibaba. Hivi juzi nilisema ngoja nijaribu kununua kwenye hizi platform zetu za kiafrika nikachagua Kikuu.

Nilivutiwa kwanza na UI ya app yake na mpangilio wa bidhaa na pia suprisingly vitu viko bei ya chini sana. Modes of payment ni rahisi pia kwani unaweza ukalipa kupitia hizi huduma za mobile money. Basi, Nilichagua raba flani hivi na jumla yote (bei ya bidhaa pamoja na shipping cost) ilikua kama 62,500/= hivi nikalipia kwa tigopesa nikisubiri mzigo wangu.

Within 1 1/2 week niliupata ila kufungua package nilistaaabu ya musa. Raba niliyoagiza ni tofauti kabisa na ile niliyoichagua na hili raba nilioletewa ni yale tunaita ‘MCHAGA KAWEZA’ yaan mdosho wa kiwango cha lami. Kwa kweli i was so dissapointed nikajiuliza what if ningeagiza mzigo ambao ni bulk.

Sijajua kama tatizo kama hili hutokea bahati mbaya ama vipi hivyo naomba feedback kwa wakuu ambao mlishawahi kutumia hizi platforms vipi mzigo yenu ilikuja kama mlivyoitarajia au ni yale yale tu?

Nawasilisha.
Kikuu arrived as odered...! jumia inazingua sana si wamikoan gharama inakuwa kubwa sana
 
NIshaagiza sana kupitia Jumia; si biadhaa si misosi! Sijawahi kupata tatizo la kuletewa bidhaa tofauti kwa sababu kimsingi, suppliers wa hizi bidhaa ni maduka yaliyopo sehemu mbalimbali Dar es salaam. Sometimes unaweza kuchelewa kupata mzigo, na hii hutokea pale endapo bidhaa uliyo-point, supplier husika hana na wanachofanya Jumia, ni kutafuta supplier mwingine! Na kwavile malipo ni baada ya mzigo kufika, HAKUNA RISK ya kuibiwa!
 
Kama hapo niliposema kua hapa ni kupeana ujuzi na ushauri kuusu manunuzi ya vitu kutoka Jumia Pamoja Na Kikuu Application Twende Sasa
 
Nimewahi kuagiza bidaa mara tatu kupitia kikuu mzigo ulifika ndani ya week mbili na nusu, sema quality ya bidhaa zao ni Mbovu Sana..

Jumia bado sijafanya manunuzi huko naomba aje hapa atuelezee.
 
Back
Top Bottom