Uzi maalumu wa kumbukumbu za usanii wa Serikali ya awamu ya tano

Lituye

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
1,862
5,680
Jamani hebu tukumbushane baadhi ya matukio ya kisanii ya awamu hii ya tano chini ya Magufuli toka iingie madarakani hapa wakituona sisi wananchi ni wajinga kumbe sisi tunawacheka tuu kuwaona ni waigizaji.

Mimi nitaonesha maigizo yao mawili kisha wewe utaongeza mengine kuonesha usanii wa hawa Matapeli wa siasa hapa nchini.

1. Tukio la kwanza la kisanii ni lile la kukamata Askari 9 Mwanza ikidaiwa walikuwa wanatorosha madini yenye thamani ya bilioni 27. Kiongozi wa Malaika alijitapa kuwa anazo taarifa za uhakika kuwa Askari wale walikuwa wakisindikiza Madini hayo na kuahidiwa kupewa bilioni moja na pia walishapewa milioni300. Cha kushangaza baadae Kiongizi wa Malaika akasikika anaagiza Askari wote warudishwe kazini na kesi yao ikawa imeishia angani.

2. Tukio la pili ni la kutekwa Mfanya biashara Mo Dewji. Kamanda Mambosasa alisema mfanya biashara huyo alitekwa na raia wa kigeni wazungu wawili.

Cha kushangaza zaidi raia hao wazungu eti wanazungumza lugha za kusini mwa Afrika. Na pia wakaja na gari lao mpaka Posta mjini wakaacha gari lao na silaha zao na kumuacha Mo Dewji hapo mjini kabisa wakatoweka.

Halafu yule Kiongozi Mkuu akaja na kibwagizo chake akimuuliza Kamanda Mambosasa kuwa eti msifikilie Watanzania ni wajinga.

Je, wewe una igizo gani la hawa jamaa? Lete hapa tuwaeleze hawa jamaa kuwa sisi Watanzania sio wajinga.
 
"Tumeibiwa sana kwenye madini, wanatorosha madini mengi sana kupitia makinikia, ripoti ya mruma na ossoro inaonyesha kuna tani 5 za dhahabu kwenye container moja LA makinikia, kuanzia Leo tunazuia kusafirisha makinikia nje"
 
"Hatuwezi kuwa na Waziri kama Simbachawene ameshirikiana na Acacia kutunyonya
Tena tumenyonywa kweli kweli" Jiwe 2016.

"Najua Simbachawene ni mchapakazi mwadilifu, nimekifuatilia toka ukiwa mwenyekiti wa kamati.

Nakupeleka kule ukashughulikie nasikia kuna matatizo ya muungano" Jiwe 2019
 
mugah di mathew,
Alijiingiza kichwa kichwa "kuwasadia" wakulima wa korosho, kununua korosho yao kwa bei nzuri. Hiyo ilikuwa ni kuweweseka baada ya kupiga hela ya mfuko wa korosho. Vituko vingi vilifuata:

1) "kuhakiki" mashamba, zoezi ambalo hata halikuwepo mwanzo na halikupangiwa bajeti.

2) kutumia jeshi, na kuahidi kwamba ikibidi korosho zitabanguliwa kwa buti za wanajeshi.

3) ucheleweshaji mkubwa wa malipo kwa wakulima, usumbufu mkubwa, na kiama kwa "makangomba". Mpaka hivi leo kuna wengi hawajalipwa korosho ya mwaka juzi.

4) Profesa wa jalalani kuibuka na kampuni feki ya kununua korosho zilizosota muda mrefu. Profesa aliitetea kampuni hiyo pale mwanzo kwa hoja kwamba walikuja kwa ndege ya kukodi!!!
 
"Tumeibiwa sana kwenye madini, wanatorosha madini mengi sana kupitia makinikia, ripoti ya mruma na ossoro inaonyesha kuna tani 5 za dhahabu kwenye container moja LA makinikia, kuanzia Leo tunazuia kusafirisha makinikia nje"
Nakushangaa sana Dr. Shein umewateu wapinzani ktk serikali yako mimi kwangu siteui mmpinzani. Baadae kateu Anna Mghwira, Kitila mkumbo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom