Joseverest
JF-Expert Member
- Sep 25, 2013
- 51,985
- 69,371
Habarini za muda huu wakuu,
Leo nimeona tuzungumze jambo moja hasa kwa sisi WANAUME.
Nimeanzisha thread hii kwa ajili ya sisi kujadili "mambo yetu" kwa lengo la kufundishana, kuhabarishana, kuonyana na kuelekezana kadiri ya "miiko ya jinsi ya kiumeni"
Najua kuna watu wataniona mtu wa ajabu na kusema mambo gani haya lakini si kwa ubaya.. Nafahamu pia kuwa kuna wachache watanielewa na wengine hawataelewa au itachukua muda kuelewa lengo la huu uzi.
Leo acha nije kitofauti..wanaume tuna hulka ya kukaa na vitu sana moyoni na mwisho wa siku tunapata majanga, stress,sonona, kupelekea kufa mapema na kuonekana dhaifu, kwa hiyo ni vizuri kufunguka na kusema ya moyoni (Japo sijalazimisha mtu kufunguka mambo yake ya ndaaani sana/too personal) ili waliopitia changamoto kama zako wajifunze pia. Ukitoa mzigo ulio nao moyoni itasaidia kutibu tatizo ulilonalo kwa maana wanaume wenzako tuko hapa tutakushauri na kukupa a,b,c.... kuliko ufie na tai shingoni ni bora uje hapa kurefresh.
Vilevile katika ulimwengu wa leo, baadhi ya "miiko na asili ya uanaume" naweza kusema imeanza na inaendelea kupotea siku hadi siku kiasi kwamba inahatarisha ustawi wa kizazi imara cha wanaume kijacho huko mbeleni katika "malezi na makuzi". Kwa mfano, Wote ni mashahidi kuwa siku hizi kuna wanaume wanapenda kuwa kama wanawake, wana tabia za kike.. "Unakuta mwanaume amelegea, hawezi kukaza" kakaa kizembekizembe tu... inafikia stage 'mwana' anafanya mambo mpaka unashindwa kumtofautisha yeye na wa kike.
Kiukweli huwa naumia sana kuona "watani zetu" wakitusema sana kuwa Hatusimamii nafasi na wajibu wetu, mara tunapenda vitonga, ooh wewe dume suruali, wakiitwa wanaume na wewe utatoka? hatujiamini mara sijui hatujui kuhudumia na shombo zingine ambazo haziandikiki hapa zenye lengo la kutudhalilisha.
Tuelezee changamoto mbalimbali tunazopitia iwe ni kazini, kwenye ndoa/familia, mahusiano,mtaani, sehemu za ibada,sokoni n.k.. Tusemezane na tuinuane kama sio kusaidiana katika kuiweka jamii kwenye mstari na kuiweka nafasi ya kiumeni kama ilivokuwa zamani . Kama ni ishu binafsi kama ana ushauri anaweza kukufuata private DM au hata hapahapa kadiri kama unaona itafaa..
Wanaume tusonge mbele, tusikate tamaa na kusimama kidete/imara, TUSITETEREKE. Tukosoane na tuambizaneni ukweli kuhusu mambo kadhaa yanayohatarisha kupoteza 'hulka ya uanaume' ili kupunguza malalamiko kwenye jamii kwa namna moja au nyingine
Naamini kupitia uzi huu wanaume kadhaa watajifunza, watahabarika na wengine kutatua changamoto mbalimbali katika jamii yetu hii yenye changamoto lukuki. Mungu pia atulindie watoto wetu maana kizazi cha sasa hivi kinateketea kwa kivuli cha ''utandawazi'' tofauti na zamani.
Kuongezea machapisho au "maoni fundishi" kutoka vyanzo mbalimbali inaruhusiwa ilimradi tu iendane na maudhui ya uzi.
NB: -Naomba tutumie lugha zenye "staha" na nzuri kuepusha uzi huu kufutwa au kufungiwa comments, kwa kuwa lengo la huu uzi ni kuelimisha {mizaha, porojo na majungu si mahala pake hapa}
- Uzi huu ni kwa ajili ya kuelekezana, mnaosema ''umekuwa kungwi wa kiume'' shauri zenu chukua linalokufaa, halikufai pita tu pembeni.
Asanteni, lets discuss!
"Real masculinity is not dominating the weak, Real masculinity is empowering the weak"
"A man who is truly masculine embraces responsibility and loves, honours, protects and provides for his family and loved ones. He lives with integrity, motivated by conviction, not comfort or convenience. True masculinity is not determined by how much physical strength a man has but rather the strength of his character''
MEN ARE MADE
Leo nimeona tuzungumze jambo moja hasa kwa sisi WANAUME.
Nimeanzisha thread hii kwa ajili ya sisi kujadili "mambo yetu" kwa lengo la kufundishana, kuhabarishana, kuonyana na kuelekezana kadiri ya "miiko ya jinsi ya kiumeni"
Najua kuna watu wataniona mtu wa ajabu na kusema mambo gani haya lakini si kwa ubaya.. Nafahamu pia kuwa kuna wachache watanielewa na wengine hawataelewa au itachukua muda kuelewa lengo la huu uzi.
Leo acha nije kitofauti..wanaume tuna hulka ya kukaa na vitu sana moyoni na mwisho wa siku tunapata majanga, stress,sonona, kupelekea kufa mapema na kuonekana dhaifu, kwa hiyo ni vizuri kufunguka na kusema ya moyoni (Japo sijalazimisha mtu kufunguka mambo yake ya ndaaani sana/too personal) ili waliopitia changamoto kama zako wajifunze pia. Ukitoa mzigo ulio nao moyoni itasaidia kutibu tatizo ulilonalo kwa maana wanaume wenzako tuko hapa tutakushauri na kukupa a,b,c.... kuliko ufie na tai shingoni ni bora uje hapa kurefresh.
Vilevile katika ulimwengu wa leo, baadhi ya "miiko na asili ya uanaume" naweza kusema imeanza na inaendelea kupotea siku hadi siku kiasi kwamba inahatarisha ustawi wa kizazi imara cha wanaume kijacho huko mbeleni katika "malezi na makuzi". Kwa mfano, Wote ni mashahidi kuwa siku hizi kuna wanaume wanapenda kuwa kama wanawake, wana tabia za kike.. "Unakuta mwanaume amelegea, hawezi kukaza" kakaa kizembekizembe tu... inafikia stage 'mwana' anafanya mambo mpaka unashindwa kumtofautisha yeye na wa kike.
Kiukweli huwa naumia sana kuona "watani zetu" wakitusema sana kuwa Hatusimamii nafasi na wajibu wetu, mara tunapenda vitonga, ooh wewe dume suruali, wakiitwa wanaume na wewe utatoka? hatujiamini mara sijui hatujui kuhudumia na shombo zingine ambazo haziandikiki hapa zenye lengo la kutudhalilisha.
Tuelezee changamoto mbalimbali tunazopitia iwe ni kazini, kwenye ndoa/familia, mahusiano,mtaani, sehemu za ibada,sokoni n.k.. Tusemezane na tuinuane kama sio kusaidiana katika kuiweka jamii kwenye mstari na kuiweka nafasi ya kiumeni kama ilivokuwa zamani . Kama ni ishu binafsi kama ana ushauri anaweza kukufuata private DM au hata hapahapa kadiri kama unaona itafaa..
Wanaume tusonge mbele, tusikate tamaa na kusimama kidete/imara, TUSITETEREKE. Tukosoane na tuambizaneni ukweli kuhusu mambo kadhaa yanayohatarisha kupoteza 'hulka ya uanaume' ili kupunguza malalamiko kwenye jamii kwa namna moja au nyingine
Naamini kupitia uzi huu wanaume kadhaa watajifunza, watahabarika na wengine kutatua changamoto mbalimbali katika jamii yetu hii yenye changamoto lukuki. Mungu pia atulindie watoto wetu maana kizazi cha sasa hivi kinateketea kwa kivuli cha ''utandawazi'' tofauti na zamani.
Kuongezea machapisho au "maoni fundishi" kutoka vyanzo mbalimbali inaruhusiwa ilimradi tu iendane na maudhui ya uzi.
NB: -Naomba tutumie lugha zenye "staha" na nzuri kuepusha uzi huu kufutwa au kufungiwa comments, kwa kuwa lengo la huu uzi ni kuelimisha {mizaha, porojo na majungu si mahala pake hapa}
- Uzi huu ni kwa ajili ya kuelekezana, mnaosema ''umekuwa kungwi wa kiume'' shauri zenu chukua linalokufaa, halikufai pita tu pembeni.
Asanteni, lets discuss!
"Real masculinity is not dominating the weak, Real masculinity is empowering the weak"
"A man who is truly masculine embraces responsibility and loves, honours, protects and provides for his family and loved ones. He lives with integrity, motivated by conviction, not comfort or convenience. True masculinity is not determined by how much physical strength a man has but rather the strength of his character''
MEN ARE MADE