Uzi maalumu kwa ajili ya kujifunza namna ya kutengeneza Android Apps

Developer Tips.

Developers na wote ambao wanajifunza utengenezaji wa android apps mnatakiwa kuwa updates na mabadiliko ya versions za android.

Google wanatarajia kuja na android 9(android pie) kuna mambo mapya yameongezwa.

Kwa upande wa developers pia kuna changamoto,

Google huwa wanaondoa baadhi ya class na methods hizi huwa zinaitwa (deprecated class au methods).

Ili kuzijua ni vizuri kuwa unatembelea google developer website vinginevyo unaweza jikuta tengeneza app ambayo haifanyi kazi kwenye versions mpya za android.

Katika somo letu kuna codes hapo nyuma nilitumia method ya managedQuery kwa ajili ya kuaccess mafile yalio kwenye simu.

In fact hii method haifanyi kazi kuanzia android 5 hivyo code iliyofuata nilitumia ContentResolver kufanya operation ya query.

Siku njema muda si mrefu nitaendelea na somo kama mnavyojua programming ni very complicated kuna kukosea.
 
Me java siijui yaani kiufupi sijui language yoyote ila napenda kufanya mambo haya unanisaidiaje?
Siku hizi kuna njia nyingi watu wanatumia kutengeneza apps za android.

Kuna platforms baadhi ambazo unaweza kuunda apps za simu za android bila kuwa na ujuzi wa code.

Just Google utazikuta, lakini pia kama unafahamu html,javascript,php unaweza kuunda app ya simu kwa kutumia apache cordova nk.

Lakini hizo apps zitakulimit mno kuunda ambazo zinahitaji kuaccess resource za android, kiuhalisia inabidi ujifunze java au kotlin kama upo serious na utengenezaji wa app.

Platform wanazounda app bila kuwa na ujuzi wa codes huwa ni kwa ajili ya kuunda app ambazo zimebase na blog au website.

Cha kukusaidia huitaji kuimaster sana java ili utengeneze android app.

Soma basics za java kwa wiki kama mbili halafu geuka sasa upande wa android.

Ni hayo tu.
 
50 Reactions
Reply
Back
Top Bottom