Samaki ni chanzo kizuri cha protini. Samaki wenye mafuta kama salmon ni vyanzo vyema zaidi vya protini.Pia ulaji wa samaki ni muhimu kwa afya ya ubongo, kukinga mwili dhidi ya maradhi mbalimbali, chanzo cha madini ya chumvi na mafuta.
Maziwa ni chanzo muhimu cha protini kwa binadamu na wanyama. Maziwa ya mama ni chanzo ambacho ni cha kipekee kilicho salama zaidi kwa mtoto mchanga kuliko hata yale ya ng’ombe. Mbali na kutupatia protini, maziwa pia ni chanzo cha vitamini. Maziwa ni bidhaa iliyo katika kategoria ya vyakula vilivyokusanya viinilishe vyote muhimu. Ni vyema kuyachemsha maziwa kabla ya kuyanywa ili kuepuka baaadhi ya matatizo ya kiafya.
Tunaweza kupata protini kwa kiasi kikubwa kwa kula nyama. Inaweza kuwa nyama nyekundu ama nyama nyeupe. Nyama nyeupe ni kama kuku na samaki. Nyama nyekundu ni ile inayotokana na mbuzi, kondoo na wanyama wengi wengineo.
Hii ni mimea ambayo inatambaa kama kunde na maharagwe na mimea ya jamii hii. Mimea hii inatambulika kuwa na kiasi kikubwa cha protini. Kwa watu wenye kipato cha chini, mimea hii ni chanzo cha msingi cha kupata protini. Maharagwe yapo ya aina nyingi. Ulaji wa aina zote hizi unaweza kutupatia protini.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.