Kwanza OCD na RPC waliochoma walikamatwa? Kwamba bado wapo tu? Hamuwajui? Bahati yenu mlichoma nikiwa sio Rais - Si wamechoma hapa, tungeshika kijiji kizima. Wangepiga ‘Push Ups’, wangelamba mchanga, kisha wangetajana tu
Mpeni asilimia na ole wake asifanye kazi Haki ya Mungu atakoma mwenyewe, akishapata hizo fedha ndani ya siku tano afanye kazi usiku na mchana, msinisamehe waheshimiwa Maaskofu wanasema usilitaje bure jina la Mungu najua mmenisamehe, lakini kwa hawa wakandarasi ngoja nilitaje
Mkandarasi wa uwanja wa ndege hatakuwa na sababu ya kuchelewesha kuanza kufanya kazi kwa nguvu zote na fanye kazi usiku na mchana, mkandarasi huyu wa hapa ambaye tangu mwaka jana anahangaika tu na kilometa 50, angepewa kilometa 200 naona angemaliza miaka 200
Kweli mkuu wa mkoa wa Mtwara umeshindwa hata kumtuma OCD au RPC wako ukamtandika pingu kwa sababu ule ni uhujumu uchumi kwa maendeleo ya Wanamtwara akashughulikiwe kule, hilo nalo lilikushinda? Wewe DC una mamlaka ya kumweka mtu masaa 48 lokapu, wakati mwingine mnawaonea raia wa kawaida, ulishindwaje?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.