7d2c1393aad664ca2dd21ea2f95bf141.jpg
 
He should have let it go
Watu 3 wakazi wa Kijiji cha Busekera Wilayani Musoma, Mara wamefariki Dunia katika tukio linalohusisha wivu wa kimapenzi ambapo Kijana aliyefahamika kwa jina moja la Omari anadaiwa kumuua mpenzi wake Paulina Paul kwa kumchoma kisu tumboni mara mbili akidai arejeshewe simu yake ambayo alimpa wakati mahusiano yao yakiwa mazuri.
_
Paulina alikataa kutoa simu na wakaamua kwenda kwa sheikh awasuluhishe, wakiwa kwa sheikh mzozo uliibuka na Omari akachomoa kisu Sheikh akatimua mbio na kuwaacha ndipo Omari akamshambulia Mpenzi wake huyo wa zamani tumboni hadi akafariki.
_
Baadae alijitokeza Mwanamke mwingne kuzuia Omari asifanye mauaji lakini Omari akamkata na panga kisha kumchinja, baada ya kuwaua wawili hao na yeye akajichoma kisu tumboni.
_
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Daniel Shillah amesema Omari alifia Zahanati na kwakuwa wote wamefariki kesi imefikia tamati hapo hapo.
 
915 Reactions
Reply
Back
Top Bottom