Uzi maalum wa kupeana Likes: Comment chochote upate "Like"

G'morning wana likes.
Bwana eeeh leo nimeota ndoto moja imeniacha njia panda.

***************************************
Ilikuwa saa 1 jioni muda huo kulikuwa bado kuna kimwanga hafifu cha jua, nikiwa nyumbani kwangu mara akatokea kijana mwenye ulemavu wa miguu (Kiwete), simjui wala sijawahi muona b4..Akawa anauelekea moja kwa moja mlango wa nyumba yangu pasipo kuongea lolote, nikapatwa wasiwasi, nikapata uamuzi wa kuingia ndani niufunge mlango kabla yeye hajaufikia mlango ule lakini ghafla nguvu na akili za kuufunga mlango vikawa vinapotea....Akafanikiwa kuingia ndani (sitting room), basi mawazo yangu yakanipeleka nimsaidie chochote kitu, nikampatia noti 1 sikumbuki ilikuwa Tsh.ngapi......Nikajua ataondoka lakini haikuwa hivyo, nikajawa na uoga kukaa na mtu nisiyemfahamu usiku ule na sijui anatokea wapi...
Basi nikachukua uamuzi wa kukimbilia chumbani na kumwacha pale peke yake. Mara nikasikia akiongea (Ndo ikawa mara yake ya kwanza kufungua mdomo pale ndani) eti anataka unyumba, akawa kafungua kabisa zipu ya suruali kakiacha nje kidudu chake...Akazidi kunitia hofu, nikatamani nitokee dirishani ikashindikana, Baada ya muda kimya kikapita nikajaribu kufungua mlango kidogo nikifikiri labda kaondoka, nikashangaa kumuona kasimama wima sio kiwete tena.
Alivyonishtukia kama namshangaa akarudi tena katika hali yake ya mwanzo ya ulemavu.

Baada ya kushtuka usingizini nimeitafakari pasipo kupata majibu ya maana ya ndoto hii.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
A6C0EF5F-1343-4F60-885C-EC3A518F431E.gif

Valentines Day! Loading...
 
Back
Top Bottom