?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1rpzyqs2u8bg0.jpg
J0
 
Wikiendi hii katika Ligi ya Bundesliga kutakuwa na mchezo wa kukatana shoka kwa kuzikutanisha timu za Schalke 04, dhidi ya Borrusia Dortmund.
Schalke 04, watakuwa nyumbani dhidi ya Borrusia Dortmund ambao wanaongoza ligi huku wakiwa hawajapoteza mchezo wowote ndani ya Bundesliga tangu msimu huu ulipoanza. Borussia Dortmund wamefunga jumla ya mabao 37, huku Schalke wakifunga magoli 14, tu katika michezo 13, ya ligi na wanashikilia nafasi ya 12 katika msimamo wa ligi ambayo Dortmund wanaongoza.
 
Schalke 04 wanategemea kupata matokeo katika mtanange huo wa watani maarufu kama ‘River Derby’ dhidi ya kikosi imara cha Dortmund chini ya Kocha Lucian Fevre.
Kikosi hiki kiliondokewa na kiungo wao tegemeo, Leon Goretzka ambaye alitimkia Bayern mwanzoni mwa Msimu huu, hawajafanya uwekezaji wakutosha kupambana na kasi ya klabu zingine.
 
Inasemekana staa wa Chelsea, Eden Hazard amekubaliana maslahi binafsi na Real Madrid hivyo inajiandaa kuanzisha mazungumzo na Chelsea huku ikitazamiwa kuweka mezani dau la Pauni 150 milioni kukamilisha uhamisho wake katika dirisha kubwa lijalo la majira ya joto.
 
Madrid inataka kumtumia staa wake, Mateo Kovacic anayekipiga kwa mkopo Chelsea kama chambo wa kukamilisha uhamisho huo na inamuona Hazard kama mchezaji ambaye atapunguza maumivu ya pengo la Cristiano Ronaldo.
 
Mkataba wa Hazard na Chelsea unatazamiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao na Chelsea haitazamiwi kupanga dau kubwa kwa staa huyo na endapo atakuwa hajasaini mkataba mpya mpaka kufikia mwishoni mwa msimu huu itafungua mlango wa kuondoka.
 
915 Reactions
Reply
Back
Top Bottom