Katika maisha mtu akifanya jambo lilelile kila siku, tena kwa njia ileile, na kutarajia kupata matokeo tofauti au mapya, hii inakuwa ishara mojawapo ya upungufu wa akili, uendawazimu au udumavu wa fikra.
Tukubali kubadilika. Kuna methali ya Hausa isemayo: “Muziki ukibadilika na dansi inabadilika.” Katika maisha mabadiliko yanapotokea, huibuka makundi matatu ya watu. Wapo wale wanaokubali mabadiliko, ‘mabadiliko huwatunza’.
Umaskini unadhalilisha. Deepa Narayan, alimnukuu maskini mmoja katika utafiti wake alioufanya katika nchi 50 duniani na kuuchapisha katika kitabu chake kiitwacho: ‘Voices of the poor: Can anyone hear Us?”
Anasema: “Kwa mtu maskini kila kitu kwake ni balaa. Maskini ni kama takataka ambayo kila mtu anaikimbia, maskini huambulia kudhalilishwa, kutukanwa na kubaguliwa pale anapohitaji msaada.”
Francois-Marie Arouet, mwanafalsafa wa Ufaransa anasema: ‘Mwenyezi Mungu alitupatia zawadi ya maisha, hivyo ni juu yetu kujipatia zawadi ya kuishi maisha mema.”
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.