Uzi maalum wa kupeana Likes: Comment chochote upate "Like"

4e039bd523159fe81589875b8eacaa84.jpeg
 
Kutokusahau mambo

Ni vigumu sana kusahau jambo ambalo lipo kwenye ratiba yako. Hii ni kutokana na sababu kuwa unafanya kazi kwa kufuata ratiba, kila mara utakuwa unatazama ratiba yako inataka ufanye nini na kwa muda gani.

Unaposahau mambo unayotakiwa kuyafanya, unapaswa kurejea kwenye ratiba yako na kutazama inataka ufanye nini.
 
Kupata muda wa kupumzika

Watu wengi wanakosa muda wa kupumzika kwa sababu wanafanya hiki mara kile bila mpangilio maalumu. Hili huwafanya kuhangaika siku nzima bila hata kujua wamekamilisha nini.

Utamsikia mtu akisema “leo nimechoka sana hata sijui nimefanya nini” “leo nahangaika tu hata hamna nilichofanya”. Hii inaonyesha kuwa mtu huyu amechoka bila hata kukamilisha kazi zake.

Kwa kujiwekea ratiba utaweza kupanga muda wa kazi na muda utakaoutumia kwa ajili ya kupumzika.
 
Utaweza kuacha tabia mbaya

Mbinu mojawapo nzuri ya kuacha tabia mbaya ni kujipangia ratiba ngumu na kuifuata. Kama kuna muda ambao unautumia kufanya matendo kamavile ulevi, matumizi ya madawa ya kulevya, uzinzi, umbea, n.k. Basi upangie muda huo majukumu mengi kwenye ratiba yako.

Kwa kuzingatia hili hutopata muda wa kupoteza kufanya matendo au tabia ambazo kimsingi siyo nzuri
 
Back
Top Bottom