Uzi Maalum: My Adsense Journey to $100 per month

AVO28

Senior Member
Jan 4, 2018
140
240
AVO28

Kwanza heshina ziende kwa bloggers wote wakubwa kwa wadogo ndani forum hii, nimekua nikisoma mada na comments na zimekua zikinifunza vitu vingi tu,

Historia yangu katika blogging ni ndefu kidogo na nimeshapitia kila aina ya shida ambayo mabloggers wadogo wanapitia, na nimeona na kujifunza mengi kwakweli,

Leo 5/1/2018 siku ya tano kati ya siku 365 za mwaka huu nimeamua kuanza safari hii ya kutengeneza pesa kupitia blog, na lengo langu ni kutengeneza $100 ndani ya miezi mitatu kuanzia sasa.

Nimeamua kuweka kiwango hicho cha $100 japo ni kidogo ili ku inspire na wengine watakao amua kwenda na mimi sambasamba kwenye safari hii wasikate tamaa.

NOTE: Safari ya blogging ni ngumu na ina changamoto Kibao, Ndio maana nikaamua kuanzisha uzi huu ili twende sambamba na bloggers wachanga kwenye shida na raha, Kila challenge ntakayokutana nayo nitaiweka hapa ili wakongwe watusaidie, na pia kila mafanikio ntakayopata yawe kwa wote watakao amua kwenda na mimi:

Nitatumia Adsense kama njia ya kutengeneza pesa hyo.

VITENDEA KAZI NILIVYONAVYO MPAKA SASA
  1. Adsense account
  2. Blog + TLD
  3. Facebook accounts (4) (Nimepanga kua na jumla ya account 50 ndani ya wiki moja ijayo)
  4. Computer + Internet
  5. Time
Leo tarehe 5 mpaka 10 my mission ni kua na facebook account 50 kwa kuanzia na kila account itakua na page yake yenyewe, kila account ntakua nikishare kwenye group 5 tu kwa kila saa moja,kwa maana hyo kila lisaa ntakua nikishare mara 250, na ntakua nikifanya manual (Sio kazi ndogo na inataka moyo) lakini nimeshaamua kufanya, na hizi account sitatengeneza mwenyewe ndio maana nimejipa siku 5 kuzitafuta, Sitatumia account mpya kwasababu nina bahati mbaya sana na account mpya huwa zinafungiwa fasta sana na facebook, kwahyo ntakachofanya ni kutafta account za zamani, zenye miaka miwili na zaidi, najua wengi mtajiuliza "Utazipata wapi hzo account?" sitazungumzia sana hili kwasababu sio lazima na wewe utafte account mpya unaweza zitengeneza tu na pengine zikapiga kazi bila kufungiwa but kwangu mimi nina rafiki yangu atanisaidia kuzipata hzo account na nimetarget nipate account za wanigeria au wa south afrika hii itanisaidia zaidi kwasababu target yangu ya traffic ni itoke south afrika kwa kuanzia.

Wakati nikisubiri account hizo ziwe tayar, kazi ntakayofanya kwa siku hizi 5 ni kuset my blogg vizuri na kutafta template nzuri na simple na responsive na iwe rafiki wa adsense,

Kuhusu articles ntakazo kuwa na weka kwenye blogg yangu, nimepanga kupost article zozote ntakazoona zinaendana na sehemu ntapokua na share articles hizo huko facebook, kwakua ntakua nikishare kwenye groups za south africa bas ntakua nikizistudy hzo group na kuona topic gan itapata views then ndio ntaenda kutafta articles ya kuweka kwenye blog,

Mi sio muandishi wa articles lakini nimepanga kutafta articles kwenye site mbali mbali ambazo hazitumii adsense na ambazo sio maarufu sana kisha nta edit kidogo ndio niweke kwenye blog yangu "Wakongwe mtanisaidia hapa kama ntakua na kosea kutumia njia hii kupata articles"

Blog itakapokua tayari na articles kadhaa ntaweka screenshot ili muione:

wish me goodluck guys,

Ntakua nikitoa update kila siku juu ya wapi nilipofikia

UPDATES 10/1/2018


Wakuu mtanisamehe kidogo kwa kua kimya lakini kimya hiki kina maana, kama mwanzo nilivyosema blogging ina challenge kibao, kuanzia tarehe 5 nilipoleta uzi huu mpaka leo tayari nimeshakutana na machellenge yakufa mtu ambayo yanakatisha tamaa kwakweli, japo pia mafanikio yapo kwa mbali,

Challenge niliyokutana nayo kubwa ni ya Kufungiwa account zangu 6 za facebook (naambiwa ni verify) na pia Link zangu kua marked as a spam huko huko facebook wakongwe nitaomba maoni yenu kwenye hili

Najua nilisema sitaanza kushare mpaka nipate account za kushare 20, lakini mtu ambae alikua akipa hizo account na yeye kwa bahati mbaya nikakuta account old zile hana alibakiwa nazo 10 tu hivyo akanipatia hizo hizo, nikasema kwakua nimepata chache tofauti na lengo wacha nijaribu kitu nione,

nikaanza kujoin zile group za wa south africa ambazo nilikua nazo kama 20 hivi kwa kuanzia Thanks kwa hii post Bloggers wenzangu nahitaji msaada wenu kuna member altupa baadhi ya groups za south afrika hivyo nikajoin hizo pamoja na zangu nnazozijua zikafika kama 40 (sikujiunga zote kwa siku moja, siku ya kwanza nilijoin 20 na siku ya pili 20) lakini nikakutana na challenge hapa pia kwamba group nyingi mpaka sasa sijawa accepted, nikama 10 tu ndio zimeshanikubalia kua member,

Yote kwa yote, kuna rafki yangu ni blogger na anafanya blogg ya udaku tu na anapiga pesa nzuri tu kwa traffic ya ndan tz, nikasema kabla ruka kwenye traffic ya south ebu nijaribu kama anavyofanya jamaa nione kama nitaambulia kitu,

Basi nikaset blog yangu fresh nikaweka na post kama 15 kwa kuanzia kisha nika weka na codes za adsense, na nikaanza kazi, ilikua juzi yani tarehe 7, nikaanza kazi saa 6 mcahana, nilichelewa kwasababu ya kuset mambo,
Capture4.PNG

Nikapost post mbili tu kwenye page yangu ya facebook, kisha kwa kutumia account hyo hyo moja ya facebook nika share kwenye magroup mawili tu ya udaku hapa bongo, yani nikashare tu post 2 kwa pamoja kwenye group kisha nikasema ngoja niache nione mpaka saa 6 usiku ntaambulia nini, Duh, nikapiga dola zangu 2
Capture5.PNG

Najua ni pesa ndogo lakini nikapata moyo kwamba kama post 2 tu nikashare mara moja moja kwenye group 2 na nikaambulia $2 vipi nikishare post 20 kwa siku na nikashare kwenye group 20 nitapata nini?

Naam hapo ndo nahisi mchawi alipoingia kwani jana na leo nilipotest kama kawaida kuweka post za blog kwenye page kisha kutumia kila account yangu (nnazo 10) kushare post 7 zilizopo kwenye page kwenda kwenye groups ndipo nikapoteza account zangu 6 na sasa nimebaki na 4 na Domain zangu 2 za blog zangu tayari facebook wanasema ni spam na nikijaribu kuwaambia sio spam lakini bado wanamark as a spam

Wakongwe tunaomba msaada hapo kwenye Links kua marked as aspam na pia kuhusu na post nazo kua marked as a spam, ntashkuru sana nikijua wapi nakosea ili nirekebishe fasta

Ni hayo tu kwa leo.
 
Ukiweza kuiteka audience ya SA utapiga mpunga ndugu yangu tena hiyo 100$ itakuwa ni ndani ya 1 day... Kuna jamaa ana audience ya south niliona kuna siku alipiga mpaka $400 mpka leo nilishindwa kuamini. Site yake ilikuwa na page RPM ya 49$ ...

Baada ya kufanya uchunguz ndy nikagundua kweli kumbe SA ni moja ya country ambazo zinalipa sana kwenye AdSense
 
Mm mwenyewe naamia south mkuu bongo tunatumia nguvu nyingi sana bt hakuna $$... Utapata jina tu kupitia site bt hauwez kumake mpunga wa heshima... Twende zetu SA MKUU
 
Ukiweza kuiteka audience ya SA utapiga mpunga ndugu yangu tena hiyo 100$ itakuwa ni ndani ya 1 day... Kuna jamaa ana audience ya south niliona kuna siku alipiga mpaka $400 mpka leo nilishindwa kuamini. Site yake ilikuwa na page RPM ya 49$ ...

Baada ya kufanya uchunguz ndy nikagundua kweli kumbe SA ni moja ya country ambazo zinalipa sana kwenye AdSense
wanabonyeza matangazo wakati wanayaona kwani wanata kuua zaidi kwani lugha inayotumika na adsense ni familiar sana kwako kukiko TZ
 
Sijakuelewa
Matangazo yanawekwa kwa lugha ya kingereza mara nyingi, na wakiliona tangazo wanabonyeza, kujua zaidi sio kama TZ watu wanayaona matangazo lakini hawaya bonyezi . ni wachache sana wanao taka kujua zaidi ya ads
 
Mkuu hongera sana, Binafsi nakushauri kama unatumia blogger platform iache, tumia wordpress ambayo ipo very simple na ina themes nzuri mfano sahifa na pia ina plugins kibao zitakazokurahisishia kazi yako.

Sauzi ukiwa na views 5,000 na clicks kama 1,000 tayari ushalaza dola 200 kina cha chini, so kule ni kwepesi sana tofauti na bongo ambako unaweza pata hata views 10,000 lakini wanaoclick tangazo hata 1,000 hawafiki ukizingatia pia cpc ni mabua unaweza kupata dola 10 tu kwa hizo views 10,000

Hapo kwenye facebook accounts jaribu kutumia hata proxy moja kwa accounts za fb tatu, Wale fb wakijua unafanya spamming wanablock accounts zote ambazo zinatumia ip moja mbadala wake tengeneza multiple devices kwa kutumia memu android emulator na enye kila emulated android device tumia account tatu.

usiweke hapa blog yako,,Sio wote wataopenda mafanikio yako...It is likely watu wenye roho mbaya watakutumia invalid clicks ilii ufungiwe
 
mkuu kwa page views 5000 na clicks 2000 hapo page ctr ni 40% hivi hapo pesa inaweza kutoka kweli?????? Mi najitahidi sana ctr isizidi 15%
Ctr ikizidi 10% tu ni hatari mkuuu... Normal ctr 3-5% ikizidi sana 5-8%. Kuanzia 10% hayo ni matatizo lazima wataramba account
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom