Uzi maalum kwako waziri Lukuvi na watendaji wa Wizara ya Ardhi kwa ujumla

Bhikalamba

JF-Expert Member
Dec 6, 2015
1,698
2,346
Kwanza kabisa napenda nikupongeze kwa juhudi zako za kutatua migogoro ya ardhi nchini.

Pamoja na pongezi hizo, naomba utilie mkazo suala la upimaji ardhi kwa nchi nzima, na udhibiti wa makazi holela. Niseme tu wazi kuwa ujenzi holela na mpangilio mbovu wa makazi katika miji yote nchini ni uzembe, kutopewa kipaumbele na utendaji ulio zorota wa idara ya Ardhi.

Katika halimashauri nyingi nilizotembelea, suala la upimaji ardhi, liko chini; ukiuliza wanasema hakuna fedha za kulipa fidia wananchi ili halimashauri ipate kumiliki eneo, kupima viwanja na kuviuza. Na hapo ndipo naliona tatizo lilipo; kimsingi hapo ndipo tulipokwamia.

Hakika tukienda kwa mkitadha huu itakuwa vigumu sana kupata fedha za kutosha kulipa wananchi fidia ya ardhi , kisha halimashauri au mamlaka za miji kuyachukua maeneo husika na kuyapima ili wauze viwanja.

Ushauri wangu, idara za ardhi kila wilaya au halimashauri waje na master plan, wapime ardhi na watoe title deeds kwa wenye maeneo husika. Ikiwa MTU akitaka kujenga tayari mipaka inakuwepo wazi kuonyesha eneo la barabara, na mipaka ya kiwanja chake. Pia akitaka kuuza, mnunuzi atanunua eneo lililokwisha pimwa na process ya kubadilisha title deed inafanyika.

Kuna halimashauri zingine idara ya ardhi wapo tu kwa ajili ya kuripoti kazini asubuhi na kurudi nyumbani jioni, hakuna kazi pale ofisini. Hakuna upimaji ardhi, ukienda ofisi ya ardhi unataka kununua kiwanja, wanakwambia hawana labda ukanunue kwa watu binafsi, lakini pia huko hupati viwanja vilivyo pimwa au kuwa na hati. Mwenye eneo atakupigia hatua kadhaa kulingana na makubaliano, mtaandikishana kwa mtendaji tu kazi imeisha. Matokeo yake ni ujenzi holela.

Rafiki yangu alinunua ardhi Mbulu mjini, baada ya kujenga MTU mwingine akaja kunua pembeni yake, wengine wakafuata kumzunguka. Sasa ikawa ni shida namna ya kuingia na gari nyumbani kwake baada ya hao majirani zake kujenga. Na huo ni mfano mmoja tu kwa kadhia hii inayotokea katika miji karibu yote inayoendelea kusitawi nchini.

Hainiingii akilini pale idara ya ardhi wanapokaa tu ofisini, huku wakipokea mishahara kila mwezi halafu kupima ardhi inasubiriwa eti fungu kutoka serikalini. Kwani, ni lazima halimashauri ipime na kujimilikisha? Kwanini wasipime tu na kutoa hati kwa wenye maeneo, wao wakabaki kukusanya maduhuri yatokanayo na kodi ya ardhi? Na hii itaongeza mapato kwa halimashauri na serikali kwa ujumla.

Ikiwa halimashauri inao maafisa na watendaji wa ardhi wanaolipwa mshahara kila mwezi, si haya ndo majukumu yao!!? Je, suala la kupima ardhi linahitaji tena fungu lingine kutoka serikalini? Nadhani hii mentality inatakiwa kuondolewa, na watu wawe wabunifu na wachapa kazi.

Zaidi, naona msisitizo wa upimaji ardhi na mpango wa makazi rasmi umewekwa zaidi mijini lakini tuelewe pia baadhi ya vijiji ndo miji ya kesho. Kwahiyo hili lifanyike kote mijini na vijijini nchi nzima, ardhi ipimwe na makazi yapangwe vizuri.

Hii itasaidia kuondoa foleni na mafuriko katika baadhi ya miji yetu mikubwa. Badala ya kutumia gharama kubwa kujenga flyovers, tungeweza kupanga vyema makazi, tukawa na barabara nyingi za mitaa kila kona, tungepunguza traffic jams kwenye highways.
 
Ukishapima hayo maeneo kwa kuwa bado ni mapori/mashamba na uhitaji wa kufyeka walime waweke mbegu wapate chakula basi wananchi wanaingiza matrekta na kulima wanang'oa bikoni, ndo hali halisi ilivyo uwandani.
 
Upimaji wote ni gharama.

Usije ukadhani ni kutoka tu ofisin na kwendaa Site ndo mana makampuni yanachaj 150000 kwenye upimaji na mawazir wanajua hillo.
Kwa kua upimaji ni gharama sio wizara au halmashauri zinatoa pesa ya kutosha kufanya upimaji ndo mana squatter kibao..kifup bajet za upimaji zikiongezw maeneo meng yatapimwa..au unataka watumishi watengeneze bikons kwa hela zao mfukon mkuu?
 
Maofisa wengi wa ardhi wanakwenda ofisini na kutafuta jinsi ya kutumia nafasi zao kujinufaisha na ardhi za watu na nia zao sio kuipatia serikali mapato.
 
Ukishapima hayo maeneo kwa kuwa bado ni mapori/mashamba na uhitaji wa kufyeka walime waweke mbegu wapate chakula basi wananchi wanaingiza matrekta na kulima wanang'oa bikoni, ndo hali halisi ilivyo uwandani.
Kuna sheria iliyotungwa kusimamia hilo. Ni suala la usimamizi na ufuatiliaji.
 
Upimaji wote ni gharama.
Usije ukadhani ni kutoka tu ofisin na kwendaa..site..ndo mana makampuni yanachaj 150000 kwenye upimaji na mawazir wanajua hillo.
Kwa kua upimaji ni gharama sio wizara au halmashauri zinatoa pesa ya kutosha kufanya upimaji ndo mana squatter kibao..kifup bajet za upimaji zikiongezw maeneo meng yatapimwa..au unataka watumishi watengeneze bikons kwa hela zao mfukon mkuu?
Sikusema upimaji ni 100% free of charge, lakini halimashauri nyingi hazipimi ardhi eti kwa kukosa beacons, no. Hiyo ingewezekana hata kwa kuweka alama za muda na kumtaka mumiliki wa eneo kuchangia gharama.

Tatizo ni kwamba Halimashauri nyingi zimebaki kwenye Sera ya zamani yaani kupata fedha kulipa watu fidia halafu eneo limilikiwe na halimashauri kisha wapime na kuuza viwanja. Na kwa mtindo huu tatizo la squatters halitaisha. Sera na utendaji wa idara ya ardhi uangaliwe upya.

Pengine tunahitaji idara hii ifanye kazi kama wakala inayo jitegemea (parastatal organization) kama ilivyo Tanroads, Tarura, Tanesco n.k badala ya kuwa chini ya halimashauri. Labda itaongeza ufanisi.
 
Yeah uko sahihi ..ago n mambo ya kisera na kibungee..ni kwl tukitaka miji yetu ikuw na squatter zipungue..hi idara ipew kipaumbele...haiwezekan kwa mwaka mzima jiji linapangiwa kupima viwanja 2000 tu kwa mujibu wa bajeti..ilitakiwa approach ibadilike upimaji upewe fedha za kutoshaa..watu wanaongezeka na mahitaj ya kupanga mini ni makubwa lakin n kama wanasiasa wameamua kuchuna tu
 
Hivi wizara ya ardhi huwa inakaguliwa na CAG?? Hela wanazokusanya zinakwenda wapi?? Wanamatumizi gani??kwa sababu kama wangekusanya kodi vizuri wangapata mapato kama TRA
 
Mh Waziri Wa Ardhi Watendaji wako wa Ardhi Manispaa ya Sumawanga wanapokonya Wamiliki HALALI wa Viwanja wenye Title Deed bila kufua Sheria na kutoa Barua kwa Matapeli wa Ardhi
 
Lukuvi mwenyewe anapokea mshahara wa Bure tu, nae astaafu tu awaachie vijana watuonyeshe wameelimika kwa kiasi gani. Mzee Lukuvi amekuwa kama mhubiri tu, hakuna kitu cha maana anafanya huko ardhi.
 
Why’s this happening??
Inashangaza sana na KAMISHNA MSAIDIZI anaona Ukiukwaji wa Sheria Wanasingizia Eti wenye washamba Wanadai Fidia wakati Manispaa ndio inapaswa kulipa Fidia ya Pesa au Viwanja kwani ndio waliotwaa Mashamba na kuwalipa Baadhi Fidia
 
Lukuvi mwenyewe anapokea mshahara wa Bure tu, nae astaafu tu awaachie vijana watuonyeshe wameelimika kwa kiasi gani. Mzee Lukuvi amekuwa kama mhubiri tu, hakuna tuna huko ardhi.

Kweli Lukuvi siku hizi amekuwa muhubiri tu utekelezaji wa watu wake wa Ardhi ni sifuri kabisa. Kule wilaya ya Hai afisa Ardhi anajifanyia mambo anayotaka yeye, rushwa inaombwa nje nje kwa kuwatesa wananchi kupata haki zao za kumiliki Ardhi!!
 
Back
Top Bottom