Uzi maalum kwa wafanyakazi wenye mikataba mifupi mifupi i.e migodoni & NGO's kuhusu mustakabali wa mafao yao

kasenene

JF-Expert Member
Jun 6, 2008
1,632
2,413
Ndugu waheshimiwa katika ule muendelezo wa kujadili agenda muhimu kwa sasa inayolindima nchi nzima hasa kwa waajiriwa woote nchini au wahenga wanavyosema ni moto unaofukuta kwa chini chini..au ambavyo vijana wasiku hizi wanasema habari 'inayokick' mjini kuhusu swala la mafao ya wastaafu au wafanyakazi walioacha au kuachishwa kazi kutokana na mabadiliko yaliyofanywa na serikali kuhusu utaratibu wa kulipa mafao ya wastaafu ambao umepokelewa kwa hisia ya kinyoge saana na wadau woote hasa hasa pale baada ya wadau kueleweshwa vizuri kuwa lengo la serikali halikuwa kuwasaidia bali ni katika kujaribu ‘kiziba mashimo iliyotoboa’ bila mpangilio huko siku za yuma. Mimi kama mlengwa mmojawapo ambaye ni mwajiliwa katika sekta binfsi chini ya ajira za mda mfupi mfupi nimeona kama vile mjadala mkubwa umejikita zaidi katika kujadili swala la wastaafu na swala 25% na kusahau kabisa swal zima la wale wafanyakazi wa migodini au wale woote wenye mikataba mifupi mifupi kama kwenye mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) ambao wengi wao wamekuwa wakipewa mikataba mifupi mifupi kati ya miaka minne hadi mitano na baada ya hapo kwa uzoefu inakuchukua mtu si chini ya miaka minne au mitatu kupata kazi nyingine au kukosa kabisa kazi jambo ambalo limepelekea wengi wao kuamua kufanya shughuli nyingine za kujitegemea. Nia na madhumuni hasa ya kuanzisha uzi huu ni kujaribu kuhamasisha au kutafuta uungwaji mkono hasa hasa kutoka kwa wafanyakazi woote walio kwenye sekta binafsi hasa wenye mikataba mifupi mifupi kama NGOs,wale wa Migodini na hata wale ambao mikataba yao ya ajira imekwisha ili tuweze kuungana kwa pomooja kudai haki zeetu ..Nakaribisha mawazo ya ni jinsi gani tujadili na kufikia muafaka …UMOJA NI NGUVU ...tunaweza kukubaliana hata kuanzisha group la telegram kuhusu ni jinsi gani ya kurahisisha hii ajenda...Nawasiilisha....
 
Doh kweli niko na vimilion vyangu kadhaa hapo LPF, hata ningeanza ufugaji wa Chiken asee
 
unataka haki gani sasa kwani umeshastafu,sheria inawazungumzia wastaafu
 
Niko kwenye kampuni moja hv sikumoja nikamwambia mwajiri wangu unaonaje kama kiasi unachonikata tuwe tunakigawana tu ili usikipeleke huko kwenye mifuko ya kijamii? ,sabubu yangu ya msingi ilikuwa kukwepa kupata usumbufu au kukosa kabisa michango yangu kwa sababu nina mkataba wa muda mfupi ,
 
Niko kwenye kampuni moja hv sikumoja nikamwambia mwajiri wangu unaonaje kama kiasi unachonikata tuwe tunakigawana tu ili usikipeleke huko kwenye mifuko ya kijamii? ,sabubu yangu ya msingi ilikuwa kukwepa kupata usumbufu au kukosa kabisa michango yangu kwa sababu nina mkataba wa muda mfupi ,
ndio kilichobakia tu..
 
Ndugu waheshimiwa katika ule muendelezo wa kujadili agenda muhimu kwa sasa inayolindima nchi nzima hasa kwa waajiriwa woote nchini au wahenga wanavyosema ni moto unaofukuta kwa chini chini..au ambavyo vijana wasiku hizi wanasema habari 'inayokick' mjini kuhusu swala la mafao ya wastaafu au wafanyakazi walioacha au kuachishwa kazi kutokana na mabadiliko yaliyofanywa na serikali kuhusu utaratibu wa kulipa mafao ya wastaafu ambao umepokelewa kwa hisia ya kinyoge saana na wadau woote hasa hasa pale baada ya wadau kueleweshwa vizuri kuwa lengo la serikali halikuwa kuwasaidia bali ni katika kujaribu ‘kiziba mashimo iliyotoboa’ bila mpangilio huko siku za yuma. Mimi kama mlengwa mmojawapo ambaye ni mwajiliwa katika sekta binfsi chini ya ajira za mda mfupi mfupi nimeona kama vile mjadala mkubwa umejikita zaidi katika kujadili swala la wastaafu na swala 25% na kusahau kabisa swal zima la wale wafanyakazi wa migodini au wale woote wenye mikataba mifupi mifupi kama kwenye mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) ambao wengi wao wamekuwa wakipewa mikataba mifupi mifupi kati ya miaka minne hadi mitano na baada ya hapo kwa uzoefu inakuchukua mtu si chini ya miaka minne au mitatu kupata kazi nyingine au kukosa kabisa kazi jambo ambalo limepelekea wengi wao kuamua kufanya shughuli nyingine za kujitegemea. Nia na madhumuni hasa ya kuanzisha uzi huu ni kujaribu kuhamasisha au kutafuta uungwaji mkono hasa hasa kutoka kwa wafanyakazi woote walio kwenye sekta binafsi hasa wenye mikataba mifupi mifupi kama NGOs,wale wa Migodini na hata wale ambao mikataba yao ya ajira imekwisha ili tuweze kuungana kwa pomooja kudai haki zeetu ..Nakaribisha mawazo ya ni jinsi gani tujadili na kufikia muafaka …UMOJA NI NGUVU ...tunaweza kukubaliana hata kuanzisha group la telegram kuhusu ni jinsi gani ya kurahisisha hii ajenda...Nawasiilisha....

HONGERA MR. PRESIDENT KWA HILO NAFIKIRI HUWA UNASOMA THREAD ZANGU...
 
MKUBWA KAMALIZA KAZI, KASEMA WAPENI CHAO WAKAFE NACHO MBELE MAANA BAADA YA MIAKA 60 PENGINE MTAKUWA MMEWASAHAU HATAKAMA WLIKUWA WANACHAMA WENU. NANI ATAWAKUMBUKA WALIKUWA NA MIKATABA YA MIAKA MIWILI MITATU AU MINNE ,? WAPENI CHAO . HII INAMAANISHA FAO HILO LINATOKA BILA KIGUGUMIZI
 
Naamini Mheshimiwa kakusikia. Subiri santuri ya kikokotoo ichuje, atakuja na fao la kujitoa.

Andikeni mabango kabisa ikibidi yabatizeni ile zaburi ya 23,
"JIWE NDIYE MCHUNGAJI WETU HATUTAPUNGUKIWA NA KITU..."
 
Back
Top Bottom