Uchunjuba Punjubi
JF-Expert Member
- Jul 1, 2017
- 799
- 619
Huu ni Uzi maalumu kwa ajili ya watu waliowahi au wanaofanya kazi kama Bank Teller au Cashiers katika mabenki mbali mbali. Tuweze kupeana vituko, uzoefu au changamoto ...n.k katika kazi hii ambayo inataka umakini sana, pia tuutumie Uzi huu kwa ajili ya kuwaelimisha watu wanaotulaumu kwamba sisi ni wezi (japo wapo baadhi) wakati kuna tupo ambao ni waaminifu 100%. Binafsi nina uzoefu wa miaka mitatu (3) katika kazi hii na nimeajiriwa na Bank fulani kongwe hapa nchini.
CHANGAMOTO
Changamoto zipo nyingi katika kazi hii lakini kwa upande wangu ni hizi
-Mwanzo wakati unajifunza kazi unashindwa kupangilia pesa vizuri, hazikai sawa kabisa
-Kuingiza loss kwa kumzidishia mteja
-Mteja anaiamini mashine ya kuhesabu pesa ikiwa utamwambia pesa yake imezidi lakini mashine hiyo hiyo mkihesabu na ukamwambia pesa imepungua anaona unamdanganya
VITUKO
Pia kuna vituko vingi lakini kwa upande wangu ni pale mtu anakuja kazificha pesa zake ndani ndani huko kisha akizitoa ili umhesabie zinakuwa mbichi mbichi hivi
Pia kuna wale wateja ambao wameizoea bank kwahiyo akija hata kama kuna foleni vipi ye anataka ahudumiwe na kuondoka. ...n.k
Karibuni Tellers wenzangu tushee ujuzi na changamoto katika kazi yetu hii ngumu, pia tujibu maswali ya wateja wanao tutuhumu vibaya(japo kiukweli wapo Tellers wenye tabia mbovu) Karibuni.
CHANGAMOTO
Changamoto zipo nyingi katika kazi hii lakini kwa upande wangu ni hizi
-Mwanzo wakati unajifunza kazi unashindwa kupangilia pesa vizuri, hazikai sawa kabisa
-Kuingiza loss kwa kumzidishia mteja
-Mteja anaiamini mashine ya kuhesabu pesa ikiwa utamwambia pesa yake imezidi lakini mashine hiyo hiyo mkihesabu na ukamwambia pesa imepungua anaona unamdanganya
VITUKO
Pia kuna vituko vingi lakini kwa upande wangu ni pale mtu anakuja kazificha pesa zake ndani ndani huko kisha akizitoa ili umhesabie zinakuwa mbichi mbichi hivi
Pia kuna wale wateja ambao wameizoea bank kwahiyo akija hata kama kuna foleni vipi ye anataka ahudumiwe na kuondoka. ...n.k
Karibuni Tellers wenzangu tushee ujuzi na changamoto katika kazi yetu hii ngumu, pia tujibu maswali ya wateja wanao tutuhumu vibaya(japo kiukweli wapo Tellers wenye tabia mbovu) Karibuni.