Uzi huu ni maalumu kwa ajili ya pedejee Yanga Omary rais wa Tanga

donlucchese

JF-Expert Member
Mar 23, 2011
17,031
21,499
YANGA OMARY RAIS WA TANGA

Kuanzia mwaka 2016, Watu maarufu kama MAPEDEJEE walikuwa na wakati mgumu sana.

Watu hawa ambao walikuwa wakiimbwa na kusifiwa na wanamziki wa dansi Walianza “kusomeshwa namba”

Nani asiyekumbuka kesi za kina Ndama mtoto wa ng’ombe na Papaa Msofe Chuma Cha Reli Laini ya Mwisho?

Watu hawa walikuwa wakinong’onwa kuwa wanajihusisha na dili za gizani zinazowapa ukwasi wa kumwaga pesa hovyo kwa wanamziki na pisi kali. Minong’ono hii haikuwahi kuthibitishwa nami sitaki kuwahukumu.

Uzi huu ni maalumu kwa ajili ya PEDEJEE YANGA OMARY RAIS WA TANGA

Tukio lilianza kwa “kichomi” kuwauma sikio watu wa Idara ya Drugs Control Enforcement Agency(DCEA) kuwa kuna “mzigo” unatarajia kuingia kupitia katika bandari bubu ya Tanga iliyo katika ufukwe wa bahari ya Hindi.

DCEA ni Idara inayohusika kupambana na dawa za kulevya.

Taarifa hiyo, Inamfanya afisa mmoja wa juu Inspector HASSAN MSANGI kusafiri kutoka Dar hadi Tanga tarehe 27 Sept 2018

Nia ya safari hii ni kwenda kuchukuza hobbies, shughuri na mali za mtu wanayemshuku kutokana na taarifa ile.

Hapa naomba niwaibie taarifa flani hivi, baada ya siku moja kuwa kupiga michapo miwili mitatu na kachero mmoja mbobevu wa polisi.

Namnukuu

“Kachero hata akiwa bar, muda wote huwa anakuwa kazini... Tabia za watu kuweka “bia msitu” mezani huwa zinamvutia sana kachero”

Anaendelea,

“Sio kwa sababu kwamba sie makachero tunakuwa na wivu dhidi ya aagizaye “bia msitu”, bali matumizi ya pesa bila mpangilio huwa yanatuwashia taa kutaka kujua shughuri halisi za mtanuaji”

Hapa “bia msitu” namaanisha kuweka vinjwaji vingi mezani na ukute vya gharama

Turudi kwenye story yetu,

Inamaana jamaa wa DCEA alikuwa anafatilia lifestyle ya mtu wanayemfatilia, wakahamia pia kuchunguza shughuri zake binafsi.

Uchunguzi wa afisa yule ulimpa “kisukununu” cha kuanza kuamini taarifa za “kichomi” wao.

“Kichomi” hakuchoka, akatoa tena info kuwa “target” yuko mbioni kuhamishia mzigo kwenye nyumba fulani iliyoko Bombo mkoani Tanga.

Taarifa ilisema “target” atakuwa anatumia gari ya Land Cruiser V8 yenye usajili T325 DJX

Idara ya DCEA ikampa jukumu Inspector wa polisi DANIEL MTEWELE kwenda kuongoza Operation ile ya kumkamata “target”

Kuna msemo unasema, Ukijua A wengine watajua U.

Saa 7 na Dk 30 usiku, Informer akampigia simu Inspector MTELEWE na kusema “Target” anaelekea kwenye nyuma ile.

Sasa naomba ninukuu

“Kaka Mwanamke aliyekuwa akiishi na “Target” kama mkewe alikuwa ni Afisa Usalama na ndio alivujisha mchongo mzima”

Dakika 30 tangu itolewe taarifa ile, hapa namaanisha saa 8 usiku,Inspector MTEWELE aliisogelea nyumba ya “target” akiwa ameambatana na wenzake kina BEATUS TUNYAWE na WP CHRISTIAN pia alikuwa na Mwenyekiti wa mtaa MIRIAM KIWAMBO.

Walipofika pale, wakajitambulisha kwa mlinzi kuwa wao ni maafisa wa DCEA na mlinzi akaenda ndani kuwaitia mwenye nyumba ile ambapo alitoka akiwa ameshika bastora mkononi.

Jamaa akanywea baada ya kujitambulisha kuwa wao ni watu kutoka DCEA na kwamba wapo pale kwa sababu wanamshuku yeye kuhusika na biashara ya “ngada”

Akafika Inspector wa polisi aitwaye WAMBA kisha maafisa wale wakaanza kupekua sehemu mbali mbali za nyumba ile huku wakiongozwa na “target” mwenyewe.

Wakiendelea na msako, maafisa wale wakagundua chini ya uvungu wa kitanda alichokuwa amelalia RAHMA ALLY mke wa “target”, kulikuwa na mkoba wa pink huku ndani yake kukiwa na mfuko wa nylon wenye unga uliosadikiwa kuwa madawa ya kulevya.

Pia kwenye Wardrobe ukakutwa unga mwingine ambao nao ulihisiwa kuwa “narcotic drugs”

Kama haitoshi kwenye katika chumba kingine kilichokuwa kinalaliwa na mtumishi wao wa ndani HALIMA MOHAMED ANUARY, ndani ya ile nyumba, kulikutwa kabati la mbao ukutani likiwa na vyombo vya kunyweshea kuku maji pamoja na kiroba kilichokuwa na chakuka cha kuku. Hapo napo baada ya kutoa kitu kimoja kimoja wakakuta soksi nyeusi ikiwa na unga uliohisiwa kuwa madawa.

Baadae upekuzi ukahamia nje kwenye gari Toyota Land Cruiser V8 T325 DJX. Kwenye gari ile kukakutwa pesa Cash Tshs 5,340,000/= na hundi za benki za AMANA,CRDB,EXIM, na NMB.

Ikatolewa hati ya ukamataji mali(Certificate of Seizure) ambapo gari na vitu vingine vilishikiliwa kwa uchunguzi. Mke wa “target”, mwenyekiti wa mtaa na target mwenyewe walitia sahii hati ya ukamataji mali.

RAHMA ALLY JUMA mke wa “target” pamoja na target mwenyewe YANGA OMARY na mfanyakazi wao wa ndani HALIMA MOHAMED ANUARY,wakapelekwa mpaka kituo cha polisi CHUMBAGENI ambako walichukuliwa maelezo.

Alfajiri yake wakasafirishwa toka Tanga hadi Dar Es Salaam pamoja na vitu vilivyoshikiliwa wakiwa wameambatana na Inspector DANIEL MTELEWELE

Nanukuu chanzo;

“ Siku jamaa alivokamatwa alisafirishwa mpaka kwa Commander In Chief Ikulu. Alipofikishwa Mzee akasema “ok kumbe wewe ndiye yanga Omary… haya nendeni mkaendelee naye… nilitaka tu kumuona”. Jamaa baada ya hapo ndo akarudishwa Tanga.”

“ Hii ni Top secret kabisa nakupa… ni kwamba capital ya kuuza dawa huyu Jamaa alipewa na aliyekuwa mwenyekiti wa Simba yule billionaire kijana Mr Chopli Chopli”

Tuendelee,

Walipofika Dar,vizibiti vile vikakabidhiwa kwa mtunza vizibiti Inspector JOHARI ISSA MSIRIKALE

Inspector JOHARI akavipa namba vizibiti vile na tarehe 2 October 2018 akavipakia kwa ajiri ya kuvipeleka kwa mkemia mkuu wa serikali.

Vizibiti vile akakabidhiwa Detective Constable MASSAWE

Pale ofisi ya Mkemia mkuu wa Serikali, vizibiti vile vilipokelewa na ELIAS ZAKARIA MULIMA ambaye baada ya kufanya “Preliminary test” akabaini kwamba vizibiti vilivyokuwa vimepewa namba D1 na D3 havikuwa madawa ya kulevya.

Lakini,

Vizibiti vilivyopewa namba D2 na D4 vilikuwa ni madawa ya kulevya aina ya Heroine Hydrocloride vyenye uzito wa gram 1053.62 (zaidi ya kilo moja)

Baada ya uchunguzi ule, Detective Constable MASSAWE akapewa majibu yake ambapo naye siku ile ile aliyarudisha kwa Inspector JOHARI.

Tarehe 3 October 2018 washtakiwa wale walirudishwa Tanga na kesho yake tarehe 4 Oct 2018 walipandishwa kizimbani mkoani Tanga ambapo Omary Yanga,Rahma Ally Juma na Halima Mohamed Anuary walishitakiwa kwa kosa la kusafirisha madawa ya kulevya kinyume cha sheria ya kupambana na kuzuia madawa ya kulevya sura ya 15 (1) (a) (3) (1) (i) [CAP 95 R.E. 2019] ikisomwa pamoja na sheria ya uhujumu uchumi sura ya 57 (i) and 60 (2) [CAP 95 R.E. 2019]

Hii ilikuwa ni kesi ya uhujumu uchumi namba 1 ya mwaka 2020

Washitakiwa walikana mashtaka yao yote na kudai kilichokutwa ndani ya nyumba yao ni madawa na chakula cha kuku kwani walikuwa na mradi wa ufugaji kuku.

Hata hivyo jaji wa kesi ile IMAKULATA BANZI alilidhika na ushaidi wa upande wa mashtaka na tarehe 20 November Mwaka 2020 alimtia hatiani mshtakiwa YANGA OMARY na washtakiwa wenzake wakaachiwa huru kwa kuwa hawakukutwa na hatia yoyote.

Kutokana na hili, YANGA OMARY akahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela pia ikaamuliwa gari na bastora yake vilivyokuwa vinashikiliwa na polisi virudishe kwa ndugu wa Yanga Omary. Pia mahakama ikaamuru madawa yaliyokamatwa yateketezwe.

Wakati OMARY YANGA anahukumiwa alikuwa ameshasota gereza la MAWENI karibu miaka miwili na alikuwa tayari ana umri wa miaka 60 huku akiandamwa na maradhi ya Moyo.

Nanukuu tena chanzo;

“Brother Usalama wa Taifa wanabalaa huyo Manzi Yanga Omari alikuwa nae kwenye mahusiano kwa takriban 5 years jamaa haku detect chochote kumbe demu Yuko kwenye mission na ilikuwa mi Pisi Kali kinoma Mkuu bro dk ya mwisho demu kaja kutoa ramani nzima ya mzigo Yani ukiwa bado mbichi haujashushwa ata kwenye gari”

Kulingana na taarifa za kipelelezi na uchunguzi wangu binafsi, nimebaini kuna taarifa mbili zinazokinzana
Informer alitoa taarifa kuwa OMARY YANGA atakuwa amebeba “mzigo” ndani ya gari lake.
Polisi hawakukuta mzigo ndani ya gari lake bali walikuta mzigo ndani ya nyumba yake.

Ndugu msomaji, unabaini nini?

Inaonekana kikosi cha DCEA kilichelewa kumuwahi OMARY YANGA akiwa na mzigo ndani ya gari, au taarifa ya kichomi ilichelewa kuwafikia kwani Omary Yanga alidai kuwa alirudi nyumbani kwake tangu saa 1 jioni siku ya tukio, na hakutoka tena.

Je, bahada ya polisi kuukosa mzigo ndani ya gari,walifosi kupata ushaidi “kimeno meno” ndani ya nyumba ya Omary Yanga? Mimi na wewe hatujui. Kwani kama ulivyosikia kesi hii ilikuwa ikifatiliwa na CIC mwenyewe kwa hiyo ilikuwa ni lazima matokeo yawe positive by hooks and crooks.

Pia “kichomi” katika story hii anaonekana ni aliyekuwa mkewe kumbe alikuwa ni “kitengo”. Hapa utaona ni kwa nini kesi hii imechukua record ya kesi zilizoendeshwa kwa haraka sana

Tarehe 27 sept 2018 mpelelezi anatumwa Tanga.
Tarehe 1 oct 2018 nyumba ya Omary Yanga inavamiwa na polisi na anakamatwa.
Tarehe 2 October 2018 anapelekwa Dar es salaam na vizibiti vinapelekwa kwa Mkemia mkuu wa serikali na majibu yanatoka siku hiyo hiyo.
Tarehe 3 October 2018 mshtakiwa anarudishwa Tanga.
Tarehe 5 Oct 2018 anapandishwa kizimbani Tanga.
Tarehe 9 Nov 2020 vizibiti vikapelekwa mahakamani Tanga.
Tarehe 20 Nov 2020 yaani siku 11 tu baada ya vizibiti kupokelewa, Hukumu inatolewa.

Lakini kijana huyu wa Kidigo Omary Yanga alikuwa na shughuri zisizoeleweka pia pale kwenye nyumba yake iliyokuwa kwenye ufukwe wa Mwambani jijini Tanga. Unaambiwa ujenzi ulikuwa hauishi pale nyumbani kwake. Mara anang’oa tiles na kuweka mpya n.k yaani aliajiri kabisa mafundi non stop pale kwake. Je haiwezekani hii biashara aliyotuhumiwa nayo alikuwa akiificha kwa mgongo wa ujenzi usiokwisha? Mimi na wewe hatujui.

Hata hivyo Omary Yanga alikatia rufaa hukumu hii kwa vigezo vifuatavyo;

Sehemu yalipokutwa madawa iliweza kufikiwa na mtu yeyote ndani ya nyumba yake hivyo ni makosa kumuhusisha yeye binasfi na madawa hayo. Madai haya yalitokewa na wakili wa mrufani Mr. RWEYONGEZA na akamtaka Jaji arejee kesi ua huko Scotland katika shauri la MARY HUTTEN MARTIN OR LEES VS HER MAJESTY'S ADVOCATE [2012]
Pia muda ambao umetajwa kuwa Omary Yanga alienda nyumbani kwake una utata. Yeye alidai kufika kwake saa 1 jioni huku watu wa DCEA wakidai alienda usiku wa manane. Ni mlinzi wa nyumba yake ndio angemaliza utata ule kwani ndiye aliyewapokea maafisa wa DCEA lakini hakuitwa mahakamani kutoa ushaidi.
Pia alipinga mahakama kupokea ushaidi wa Mkemia mkuu kwani kwake wanadai walikuta Unga lakini tipoti yake ilisema kilichopelekwa kwake ni chengachenga. Hivi ni vitu viwili tofauti.
Pia shaidi wa tano wa jamuhuri ambaye ni Detective Constable MASSAWE alipokea vizibiti saa 8 kamili mchana lakini Mkemia alidai kuvipokea saa 8 na dk 44, huu muda wa dk 44 ulitakiwa kuelezewa alikuwa akifanya nini lakini hakufanya hivyo kama sura ya 48(2)(3) ya sheria ya kupambana na madawa ya kulevya inavyotaka. Wakili wa mrufani Mr. Magafu alidai inawezekana kabisa muda huu ulitumika kubadili vielelezo.
Pia wakili Magafu akadai mtunza vidhibiti ambaye alikuwa ni shaidi wa tatu wa Jamuhuri hakuieleza mahakama muda ambao alipokea vielelezo kutoka kwa shaidi wa tano Detective Constable William Massawe kutoka kwa mkemia mkuu hivyo makabidhiano ya vielelezo yalikiukwa. Akamtaka Jaji amfutie makosa mteja wake kwa kurejea kesi mbili za rufaa za ZAINAB D/O NASSOR Zena VS REPUBLIC, No. 348 ya mwaka 2015 na kesi ya rufaa ya PAULO MADUKA AND 4 OTHERS VS REPUBLIC, No. 110 ya mwaka 2007.

Swala la rufaa ya kesi hii kiundani nitaliandalia uzi wake maalumu kwenu nyie wasomaji kwa nia ya kujifunza vifungu vya sheria.

Lakini kwa ufupi tu ni kuwa rufaa hii iliaangukia pua na hukumu ya mwanzo ikaendelea kukaziwa.

Sasa turudi kujua kidogo maisha wanayoishi watu kwa kikosi cha kupambana na madawa ya kulevya ndani na nje ya ofisi.

Watu hawa wana ulinzi wa hali ya juu.

Hapa nitakinukuu chanzo changu ambacho kilienda kumtembelea ofisini mshikaji wake wa siku nyingi ambaye ni afisa wa DCEA;

“Hicho kitengo Cha madawa nimewahi kufika headoffice zao ziko hapo Utumishi house Kama unaenda feri kupanda panton mle ndani Kuna Kuna ofisi za cosota pia hawa wanaodhibiti hakimiliki.”

Anaendelea,

“Sasa nyuma ndani ya uzio huo huo nyuma hizo ofisi za COSOTA ndo kuna jengo la DCEA Mwanangu mmoja ndo amekula shavu hapo Kama director of operations nadhani ni second in command baada ya yule kamishna wa madawa. Mshikaji tulikuwa nae intake Moja …..”

“Sasa hivi jamaa ni Lt Col anaitwa Fredrick Milanzi Mkuu siku hiyo nimeenda kupay visit ofisini kwake aise jamaa Yuko protected mpaka nilishtuka ndo nikajua ishu za madawa ni ishu ambazo ni very sensitive brother”.

“Simu na vitu vyote vyenye asili ya chuma niliacha counter ambapo palikuwa na ma officer watatu mmoja ni Askari polisi amevaa uniform ya polisi wawili wamevaa kiraia ila yule mmoja kwa Ile kauda suit aliyokuwa amevaa nikajua direct ni Afsa Usalama basi wakaniadikisha kisha wakanihoji unakuja kumuona nani? nikawaeleza Afande fulani. Una appointment? nikajibu ndio basi ikapigwa simu ofisini nikaambiwa Mkuu anakula so nikapelekwa waiting room palepale pembeni ya reception”

“Baada ya muda nikafatwa na bwana mdogo mmoja nae kwa Ile suit nadhani alikuwa ni Usalama pia basi tukapandisha lift mpka floor ya tatu ambapo ndo ofisini kwa mshikaji lift ilivofunguka jamaa akanikabidhi kwa vijana wengine wawili Kisha ye akashuka kurudi ground wale jamaa wakaniuliza nina simu nikasema hapana iko counter wakasema sawa nikawekwa Tena ofisi ndogo Yani nje ya ofisi ya mwamba Kuna ofisi ndogo Ambayo ndo wanakaa hao walinzi wake wawili pamoja na secretary after muda secretary akaenda kumuona Afande then akaniambia ingia”.

“Bro aise nilitamani nami nirudi job kaka … hiyo ofisi ni five star nadhani umenielewa…!”

“ Basi tukapiga soga kidogo japo simu za hapa na pale zilikuwa zinakatisha maongezi yetu”.

FARAGHA ZA WATUMIA SIMU MASHAKANI

“ brother nawashangaa watu wanaolalamika maongezi ya Mbowe Kuwa hacked...”

“wakati niko mle ofisini zilikuwa zinatolewa order na jamaa kwenye simu kuwa anahitaji maongezi ya mtu fulani kuanzia siku fulani mpk siku fulani na especially nyakati za usiku…”! so hivi vitu ni normal kabisa linapokuja Swala la Ulinzi wa nchi.

MSANII MKUBWA NI MUUZA NGADA

Nanukuu,


“So by the end of the day nilikuwa na jambo langu jamaa aka ni assist vizur tu…

“but story alizonipa ndo nikapata picha kamili za mtandao wa madawa ya kulevya bongo.

“Bro Kuna wasanii wakubwa kabisa nchi hii mmoja ana radio na TV na ana magari sijui yalikuja kwenye container wako kwenye hiyo chain sema system inawalinda.”

“so usiwaone wanavaa zile nguo za kijani kupanda kwenye kampeni ukajua wanapenda wapo ambao file zao ziko pale kwa mshkaji tena with evidence so nikama wamebinywa Kuwa “if u don't support us you are finished tutaku expose”

Jamaa akamalizia,

“ Ndio hivyo yaani so ndo Tanzania yetu kaka mambo ni mengi muda ni mchache wacha mi nipumzike see u when u see me bro”


MWISHO
 
Umenikumbusha mbali kuhusu yanga daaah,wadigo wa pale mwambani huwaambii kitu kwa omary yanga...ishu ya yanga ilikuwa inajulikana muda mrefu sanaaa na hata wananchi wachache walikuwa wanafahamu sema kilichokuwa kimebaki ni 'timing' nzuri tu,unafikiri kwa nini alinaswa kipindi Cha alcohol gufuri?,network ya poda ni kubwa sana...walikuwa wanashangilia Sana zile hammer zilivyokuwa zinapita pale wanapaita njia panda ya mwambani Yani mwakidila sijui pale,long time...
 
Umenikumbusha mbali kuhusu yanga daaah,wadigo wa pale mwambani huwaambii kitu kwa omary yanga...ishu ya yanga ilikuwa inajulikana muda mrefu sanaaa na hata wananchi wachache walikuwa wanafahamu sema kilichokuwa kimebaki ni 'timing' nzuri tu,unafikiri kwa nini alinaswa kipindi Cha alcohol gufuri?,network ya poda ni kubwa sana...walikuwa wanashangilia Sana zile hammer zilivyokuwa zinapita pale wanapaita njia panda ya mwambani Yani mwakidila sijui pale,long time...
Yanga Omari alionywa sana aache hizo mambo baada ya awamu ya tano kuingia madarakani lakini akapuuza! Yeye kama Chonji wa Magomeni walijisahau kiasi hata watoto wadogo walikua wanajua biashara yao

Pia walikua wanajiamini kupita kiasi kwasababu walikua "wanawatoa" mapolisi.

Nyumba ya Yanga Omari pale Mwambani ipo karibu kabisa na bahari akiwa amepakana na marehemu Mzee Makalo Athuman. Nashangaa mzee huyu sijui kwanini hakua amemuonya jirani yake asome alama za nyakati na aachane na hiyo biashara maana Mzee Makalo alikua na connection na watu wa system
 
Kwa hyo wenye mamlaka yao ndo wanawafuga wauza ngada au nao wapo kwenye chain hyohyo??
Hili mbona si la kuuliza.

Wanajulikana vizuri tu.

Kwa wabongo walivyo wambea labda ukauzie mbinguni ndo usijulikane.

Asikudanganye mtu hakuna muuza ngada yoyote asiejulikana.

Issue ni ushaihidi usioacha shaka sababu ma drug lords nao sio wanyonge wana mbinu elfu moja kidogo.
 
19 Reactions
Reply
Back
Top Bottom