Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Nilikuwa natafuta namna moja ya kuelezea mgogoro ambao ninao na Idara hii nyeti ya Ikulu kwa muda mrefu. Mgogoro ambao tayari umeshawahi kujadiliwa hapa mara kwa mara lakini itoshe leo niuweke kwa maneno machache ili maana yake isije kupotea katika maneno mengi. NI mgogoro wa maono, uongozi, utendaji, uwajibikaji na zaidi ya yote ni mgogoro wa ukweli.
Kuna uzembe uliokubuhu ambao unaakisi tu matatizo ambayo tunayo kwenye idara nyingine mbalimbali za seriklali.
1. Tumelalamika miaka nenda miaka rudi sasa kwanini Ikulu haina mtandao mzuri kiintaneti wenye kusheheni taarifa mbalimbali za shughuli za Rais na hivyo kufanya kuwa chanzo cha kuaminika cha habari kwa vyombo vingine vya habari. Ninaamini wao ndio walipaswa kusimamia mambo hayo ya TEKINOHAMA hapo Ikulu ili kuhakikisha Ikulu ya Tanzania ina mtandao wa kisasa wa habari.
Tovuti ya http://www.statehouse.go.tz haipo kwa muda mrefu sasa na ukienda Ikulu.go.tz utashangaa kuambiwa ni "Tanzania Building Agency"! na tumelalamikia hili kwa muda mrefu. Ili kuweza kuelewa ninachozungumzia angalia tovuti za Kenya - statehousekenya.go.tz, Uganda-statehouse.go.ug, au Rwanda (wanayo ya Paul Kagame, na ya Serikali).
Kwanini vitu hivi ni muhimu? sababu moja ni kwamba vinakuwa ni kiungio cha haraka na cha uhakika katika ya wananchi na Rais wao na Ikulu yao. Badala ya wananchi kusubiri kila siku magazeti yaeleze nini Rais kafanya au nini kimetokea Ikulu leo au kitatokea kesho, Ikulu ingeweza kabisa kuwa na habari hizi kila siku na kwenye tovuti ambayo ni rahisi pia kukisiwa.
Lakini kinachouudhi ni kuwa Idara hii inadaiwa kuwa imetengewa karibu dola laki mbili! kwa ajili ya kuendeleza tovuti ya Ikulu! Sasa miaka minne na hawa watu wameshindwa kufanya jambo dogo linalochukua masaa 24 tu?
2. Tovuti ya Tanzania.go.tz; sasa baada ya hilo la hapo juu tatizo jingine ni ni tovuti rasmi ya serikali yetu, yaani ile ya anuani hiyo hapo juu. Japo tovuti hii imekuwa ikiwekewa taarifa mpya mara kwa mara lakini ni mojawapo ya tovuti zenye sura mbaya, mpangilio mbaya na inatumia teknolojia ya karibu miaka 15 ya nyuma katika mambo ya internet.
NI sawasawa na watu wanaoisimamia wamefungwa katika kile kinachoitwa na rafiki yangu Kiranga kuwa ni time warp na hawawezi kutoka humo na matokeo yake wanatuzungusha mle mle. Lakini kinachoudhi zaidi ni kuwa tovuti hii ndio imegeuka kuwa ni tovuti ya Ikulu! NI kama hawa kina Salva, Premi (huyu mdada tena nina kesi naye nyingine.. na atajibu siku moja) wanaishi katika sayari nyingine hivi. Tovuti hii ya serikali ingekuwa inasimamiwa na Wizara ya Habari na utamaduni badala ya Ikulu! Ingekuwa ni mahali ambapo mtu akitaka kujua kuhusu Tanzania au mahali pa kuanzia kuhusu utendaji wa serikali ya Tanzania au vyombo vyake mbalimbali angeweza kwenda hapo.
Halafu cha kukera zaidi badala ya kuwa na tovuti mbili zenye lugha mbili tofauti (Kiswahili na Kiingereza) basi wameamua kuchanganya tu mumo kwa mumo; kuna nyaraka za Kiingereza, zipo za kiswahili zote zimesambazwa ukurasa mzima bila kufuata mpangilio wowote wa kimantiki au maudhui. Wenyewe wanaita "Online Gateway"! my foot!
3. Katika tovuti zao zote na habari zote zilizopo inaonekana hawa jamaa wa Ikulu (Mawasiliano) hawajawahi kukaa chini na kusema waanze kuweka kumbukumbu za taarifa mbali mbali za serikali yetu kwenye mtandao hasa taarifa ambazo zimekuwa declassified na ni haki ya wananchi kuzijua (nyingi zimepita tayari miaka 30 ya kawaida ya kuzizuia). Kuna mambo mengi ambayo wasomi wetu wangeweza kuyapata kwa kupata taarifa hizo mbalimbali za mwanzo wa jamhuri yetu, kwanini Ikulu isiziweke hadharani kwa mtandao ili kila mtanzania aweze kuzipitia?
Inaonekana katika fikra zao historia ya Tanzania imeanza wakati wa Mkapa! Hebu angalia:
- Picha zilizopo kwenye tovuti hiyo ya tanzania.go.tz kuhusu Rais ni za mwaka 2007!
- Press Release waliyonayo (as of leo) ni ya Aprili 8, 2010. Ina maana kwa haraka haraka hawa jamaa hawajatoa press release kwa mwezi mzima. Kwa taifa kama la kwetu idara inatakiwa kutoa press release kila siku iendayo kwa Mungu ya nini Rais kafanya au nini kimetokea Ikulu.
-Ukienda kwenye hotuba za marais wanazo kuanzia awamu ya tatu tu! Kwa maneno mengine awamu ya pili au ya kwanza haina nafasi katika Tanzania yao hii mpya. Hivi hawaoni kuwa historia yetu ni ya moja kwa moja tangu Nyerere hadi leo hii? Hata kama hawampendi Nyerere au kutaka kumkumbuka na hata kama wanaona Mwinyi hakuwafaa hawawezi kamwe kufuta historia zao. Tunahitaji watu pale ambao wataweza kuunganisha historia nzima kwa manufaa ya watanzania. Ingesaidia sana wanafunzi katika shule na vyuo vyetu wanaofanya utafiti mbalimbali au hata kwa waandishi na watafiti wa mambo mbalimbali.
4. Kilichonitibua hata hivyo zaidi ni upotoshaji wa wazi unaofanywa na idara hiyo linapokuja suala la hotuba za Rais. Nimefuatilia kwa muda mrefu (tangu hotuba ile ya Kikwete kuhusu Muungano Bungeni) hadi sasa na nimegundua kuwa kina Salva, Premi, na wenzao wanaamini kabisa kuwa hotuba ya Rais ni ile iliyoandaliwa na siyo iliyotolewa!
Katika mawazo yao potofu, ile hotuba iliyoandikwa ndiyo rasmi na ile iliyotolewa siyo rasmi na hivyo utaona kuwa katika tovuti ya Tanzania hotuba za Rais zilizowekwa siyo zote ndizo zilizotolewa na Rais. Wamekuwa wakiweka mtandaoni hotuba zilizopangwa kutolewa lakini SIYO zilizotolewa.
Mfano mzuri ni hotuba ya mwaka jana ambapo Rais alizungumzia suala la asilimia 30 za bajeti kutafunwa na mafisadi wakati akifungua jengo la PCCB. Japo alizungumza hadharani hilo kwenye hotuba yao kina Salva hilo hakuna!
Mfano mwingine ni hii hotuba ya juzi kwa Mbayuwayu, Watanzania wengi wanakumbuka mfano huu wa Kikwete na porojo nyingine alizozitoa. Ile ndiyo ilikuwa hotuba rasmi. Lakini kina Salva katika hekima yao ya milele wameamua kuweka hotuba ambayo Kikwete alikuwa aitoe!
Ukweli ni kuwa hapa wanapotosha watu kwa sababu wanatuweka hotuba ambayo Kikwete mwenyewe hakuitoa. Wakati umefika waache hili, kama Rais wao hawezi kukaa makini na kusoma alichoandikiwa kama Obama basi ni watoe hotuba zake kama zilivyo, kama walivyokuwa wakimfanyia George Bush kwani hizo ndizo hotuba rasmi! Nakumbuka vizuri hili kwa sababu katika ile hotuba ya kutetea Muungano Kikwte alisema mengi sana na mengi yaliyokuwa yakushagaza zaidi lakini ndugu zetu hawa katika hekima yao isiyo na mwisho wakaonelea wasitoe hotuba ile bali watoe kile "alichopaswa" kusema.
Ndugu zangu, kuna mgogoro wa mawasiliano na wakati umefika Salva na Premi waachie ngazi wawape watu wengine nafasi ya kufanya kazi ya mawasiliano ya Ikulu kwa uhakika, ufanisi na ukweli.
Kuna uzembe uliokubuhu ambao unaakisi tu matatizo ambayo tunayo kwenye idara nyingine mbalimbali za seriklali.
1. Tumelalamika miaka nenda miaka rudi sasa kwanini Ikulu haina mtandao mzuri kiintaneti wenye kusheheni taarifa mbalimbali za shughuli za Rais na hivyo kufanya kuwa chanzo cha kuaminika cha habari kwa vyombo vingine vya habari. Ninaamini wao ndio walipaswa kusimamia mambo hayo ya TEKINOHAMA hapo Ikulu ili kuhakikisha Ikulu ya Tanzania ina mtandao wa kisasa wa habari.
Tovuti ya http://www.statehouse.go.tz haipo kwa muda mrefu sasa na ukienda Ikulu.go.tz utashangaa kuambiwa ni "Tanzania Building Agency"! na tumelalamikia hili kwa muda mrefu. Ili kuweza kuelewa ninachozungumzia angalia tovuti za Kenya - statehousekenya.go.tz, Uganda-statehouse.go.ug, au Rwanda (wanayo ya Paul Kagame, na ya Serikali).
Kwanini vitu hivi ni muhimu? sababu moja ni kwamba vinakuwa ni kiungio cha haraka na cha uhakika katika ya wananchi na Rais wao na Ikulu yao. Badala ya wananchi kusubiri kila siku magazeti yaeleze nini Rais kafanya au nini kimetokea Ikulu leo au kitatokea kesho, Ikulu ingeweza kabisa kuwa na habari hizi kila siku na kwenye tovuti ambayo ni rahisi pia kukisiwa.
Lakini kinachouudhi ni kuwa Idara hii inadaiwa kuwa imetengewa karibu dola laki mbili! kwa ajili ya kuendeleza tovuti ya Ikulu! Sasa miaka minne na hawa watu wameshindwa kufanya jambo dogo linalochukua masaa 24 tu?
2. Tovuti ya Tanzania.go.tz; sasa baada ya hilo la hapo juu tatizo jingine ni ni tovuti rasmi ya serikali yetu, yaani ile ya anuani hiyo hapo juu. Japo tovuti hii imekuwa ikiwekewa taarifa mpya mara kwa mara lakini ni mojawapo ya tovuti zenye sura mbaya, mpangilio mbaya na inatumia teknolojia ya karibu miaka 15 ya nyuma katika mambo ya internet.
NI sawasawa na watu wanaoisimamia wamefungwa katika kile kinachoitwa na rafiki yangu Kiranga kuwa ni time warp na hawawezi kutoka humo na matokeo yake wanatuzungusha mle mle. Lakini kinachoudhi zaidi ni kuwa tovuti hii ndio imegeuka kuwa ni tovuti ya Ikulu! NI kama hawa kina Salva, Premi (huyu mdada tena nina kesi naye nyingine.. na atajibu siku moja) wanaishi katika sayari nyingine hivi. Tovuti hii ya serikali ingekuwa inasimamiwa na Wizara ya Habari na utamaduni badala ya Ikulu! Ingekuwa ni mahali ambapo mtu akitaka kujua kuhusu Tanzania au mahali pa kuanzia kuhusu utendaji wa serikali ya Tanzania au vyombo vyake mbalimbali angeweza kwenda hapo.
Halafu cha kukera zaidi badala ya kuwa na tovuti mbili zenye lugha mbili tofauti (Kiswahili na Kiingereza) basi wameamua kuchanganya tu mumo kwa mumo; kuna nyaraka za Kiingereza, zipo za kiswahili zote zimesambazwa ukurasa mzima bila kufuata mpangilio wowote wa kimantiki au maudhui. Wenyewe wanaita "Online Gateway"! my foot!
3. Katika tovuti zao zote na habari zote zilizopo inaonekana hawa jamaa wa Ikulu (Mawasiliano) hawajawahi kukaa chini na kusema waanze kuweka kumbukumbu za taarifa mbali mbali za serikali yetu kwenye mtandao hasa taarifa ambazo zimekuwa declassified na ni haki ya wananchi kuzijua (nyingi zimepita tayari miaka 30 ya kawaida ya kuzizuia). Kuna mambo mengi ambayo wasomi wetu wangeweza kuyapata kwa kupata taarifa hizo mbalimbali za mwanzo wa jamhuri yetu, kwanini Ikulu isiziweke hadharani kwa mtandao ili kila mtanzania aweze kuzipitia?
Inaonekana katika fikra zao historia ya Tanzania imeanza wakati wa Mkapa! Hebu angalia:
- Picha zilizopo kwenye tovuti hiyo ya tanzania.go.tz kuhusu Rais ni za mwaka 2007!
- Press Release waliyonayo (as of leo) ni ya Aprili 8, 2010. Ina maana kwa haraka haraka hawa jamaa hawajatoa press release kwa mwezi mzima. Kwa taifa kama la kwetu idara inatakiwa kutoa press release kila siku iendayo kwa Mungu ya nini Rais kafanya au nini kimetokea Ikulu.
-Ukienda kwenye hotuba za marais wanazo kuanzia awamu ya tatu tu! Kwa maneno mengine awamu ya pili au ya kwanza haina nafasi katika Tanzania yao hii mpya. Hivi hawaoni kuwa historia yetu ni ya moja kwa moja tangu Nyerere hadi leo hii? Hata kama hawampendi Nyerere au kutaka kumkumbuka na hata kama wanaona Mwinyi hakuwafaa hawawezi kamwe kufuta historia zao. Tunahitaji watu pale ambao wataweza kuunganisha historia nzima kwa manufaa ya watanzania. Ingesaidia sana wanafunzi katika shule na vyuo vyetu wanaofanya utafiti mbalimbali au hata kwa waandishi na watafiti wa mambo mbalimbali.
4. Kilichonitibua hata hivyo zaidi ni upotoshaji wa wazi unaofanywa na idara hiyo linapokuja suala la hotuba za Rais. Nimefuatilia kwa muda mrefu (tangu hotuba ile ya Kikwete kuhusu Muungano Bungeni) hadi sasa na nimegundua kuwa kina Salva, Premi, na wenzao wanaamini kabisa kuwa hotuba ya Rais ni ile iliyoandaliwa na siyo iliyotolewa!
Katika mawazo yao potofu, ile hotuba iliyoandikwa ndiyo rasmi na ile iliyotolewa siyo rasmi na hivyo utaona kuwa katika tovuti ya Tanzania hotuba za Rais zilizowekwa siyo zote ndizo zilizotolewa na Rais. Wamekuwa wakiweka mtandaoni hotuba zilizopangwa kutolewa lakini SIYO zilizotolewa.
Mfano mzuri ni hotuba ya mwaka jana ambapo Rais alizungumzia suala la asilimia 30 za bajeti kutafunwa na mafisadi wakati akifungua jengo la PCCB. Japo alizungumza hadharani hilo kwenye hotuba yao kina Salva hilo hakuna!
Mfano mwingine ni hii hotuba ya juzi kwa Mbayuwayu, Watanzania wengi wanakumbuka mfano huu wa Kikwete na porojo nyingine alizozitoa. Ile ndiyo ilikuwa hotuba rasmi. Lakini kina Salva katika hekima yao ya milele wameamua kuweka hotuba ambayo Kikwete alikuwa aitoe!
Ukweli ni kuwa hapa wanapotosha watu kwa sababu wanatuweka hotuba ambayo Kikwete mwenyewe hakuitoa. Wakati umefika waache hili, kama Rais wao hawezi kukaa makini na kusoma alichoandikiwa kama Obama basi ni watoe hotuba zake kama zilivyo, kama walivyokuwa wakimfanyia George Bush kwani hizo ndizo hotuba rasmi! Nakumbuka vizuri hili kwa sababu katika ile hotuba ya kutetea Muungano Kikwte alisema mengi sana na mengi yaliyokuwa yakushagaza zaidi lakini ndugu zetu hawa katika hekima yao isiyo na mwisho wakaonelea wasitoe hotuba ile bali watoe kile "alichopaswa" kusema.
Ndugu zangu, kuna mgogoro wa mawasiliano na wakati umefika Salva na Premi waachie ngazi wawape watu wengine nafasi ya kufanya kazi ya mawasiliano ya Ikulu kwa uhakika, ufanisi na ukweli.