Ikiwa ni Ishara tosha kuwa katika uchaguzi mkuu ujao CCM Tabora Mjini itapoteza viti vingi vya Udiwani kama mtendaji wa CCM tabora Mjini na Timu yake hawatawajibishwa! hadi Uchaguzi unafanyika hakuna semina yeyote kwa viongozi wala mawakala hivyo kuingia kwenye uchaguzi kwa kubahatisha. matokeo yameonyesha kuwa viti vingi vya Mitaa vilivyokuwa vikishikiliwa na CCm vimekwenda CUF, TLP na UDP kwa idadi kubwa tofauti na miaka ya nyuma. viongozi wa CCM Mkoa na Taifa fanyeni hima ili kurekebisha hali ya ya kisiasa tabora MJINi vinginevyo hali ni mbaya Mno, Katibu Mwenezi wa CCM mkoa Tabora ambaye pia ni diwani kata yake ina idadi kubwa ya viti vya mitaa vilivyochukuliwa na vyama vya siasa tofauti na CCM kwa maana CCM 5 upinzani 6, Mkiti wa CCM Mkoa wa tabora anaongozwa na CUF aibu!