Uzawa ni dhana ya kishenzi inayotumiwa na wanasiasa janja janja na wenye Akili ndogo kabisa

William Mshumbusi

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
1,656
2,250
Ukifatilia tawala kubwa zilizopitA kale, za Sasa na matAifa yaliyoendelea kiuchumi Kuna mchango mkubwa Sana wa wageni kutoka nje.
Ukiangalia asili ya Trump na Obama wote walitoka nje ya marekani. Ukizungumzia nguvu ya kivita Basi zungumzia nguvu za waisraeli waishio Marekani na Russia ndio msingi wake. Ukizungumzia Ujerumani yenye nguvu NI Akili za waisraeli waliotekwa na kutumikishwa na Adolf hitra.

Wanahistoria wanaweza wasinielewe kabisa nikiwaambia Taifa kubwa kutokea duniani la utawala wa uturuki (otuman empire) ulitumia wataalamu wa hesabu, philosophy na madaktari Bingwa kutokea Ugiriki. Tusome historia jamani. Uongozi, utaalamu wowote kinachotangulia NI talent Mambo ya ELIMU huja tu kuing'arisha talent aliyonayo mtu.

Watu wa Mpira hupima kwa macho ndio maana Leo Simba na yanga zinajaza wachezaji kutoka nje, kocha kutoka nje na wazawa wakitaka kuhoji wanakosa nguvu kwa kuona matokeo. Kama ulivyo Mpira uongozi ( manajement) NI kipawa sio kila mtu anaweza kumenaji ata awe na madegree mangapi. Watu walikimbia shule wakaenda kuunda kampuni zinazoongoza duniani kwa mafanikio. William Henry Gets(Bill gets) hakumaliza degree akarudi muanzisha kampuni kubwa Sana duniani.

Tukumbuke pia mafanikia ya Nmb Sasa yanatokana na UBUNIFU wa top management nett group kutoka south Afrika baada ya kufeli na kujiendesha kwa hasara ya miaka nenda Rudi kwa wazawa wa iliyokuwa NBC.

Nakumbuka jinsi serikali ilivyowawekea ngumu voda kupata kibari Cha kuajili top management ya yule mkenya ikitakA mzawa. Sijui iliwaza mzawa yupi?!! Kwa mafanikio gani aliyoyapata ya uongozi katika kampuni ipi au waliangalia na PhD tu.

Juzi Tena Baada ya mfumo wa ruku kusumbua nilisikia waziri akiingizwa kingi na kuanza kulaumu wageni wanaoendesha mfumo husika. Bila tafiti iliyokamilika ya kujua chanzo chA tatizo ukweli na Nini kilitokea. Hapo mtu yoyote anaweza kuujumu mfumo Fulani ili apate njia ya kumtoa mgeni na kuweka watu wake.

Kama unawaza maendeleo ya kweli NI ujinga na ujanja ujanja kuanza kufikilia uzawa kwanza.
NI dhana ya kishamba Sana na kizamani mno kufikiri watu wako au taifA lako NI Bora kuliko watu wengine wote. Kama tunatAkA maendeleo tuangalie uwezo sio uzawa au mzungu yeyote anaweza kufanya vizuri.
 
Ukifatilia tawala kubwa zilizopitA kale, za Sasa na matAifa yaliyoendelea kiuchumi Kuna mchango mkubwa Sana wa wageni kutoka nje....
Umeonaee madhulumati ndiyo yanaenda hilo neno.Na wanao pambana kutetea empty legacyhawana plan B,nikamtu aliyejiachia mbio kwenye mteremko Mali ukamsimamisha ghafla hawezi mpaka afike chini,subiri kukuche kunawatu wataanza kuulizia blanket
 
Ukifatilia tawala kubwa zilizopitA kale, za Sasa na matAifa yaliyoendelea kiuchumi Kuna mchango mkubwa Sana wa wageni kutoka nje..
Mbona China, Japan, India na Singapore hawana hao watenda miujiza yako? Ni suala la kutumia akili. Siyo kila taifa lililoendelea limefanya hivyo kwa kutegemea wageni.

Kwani huyo Trump na Obama wameongeza nini kwa Marekani? Kwa nchi ambazo wageni huja na kuendelea kung'ang'ania uraia wa hata nchi wasizokuwa na uraia kama wahindi wakiiba na kutoroshea India na Ulaya, dhana hii inafaa. Ubunifu wa nchi hautegemei wageni vinginevyo Japan na Korea ya Kusini wasingewini
 
Hakuna taifa lenye akili timamu linalokabidhi mgeni sehemu zake nyeti au Kazi zake ovyo ovyo.
Kama ikulu ya marekani iliongozwa na mtoto wa mkenya Mzee Obama aliyeenda Marekani kusoma tu lakini akazaa uko. Sasa unataka utuaminishe unachokiamini kwa mfano upi!?
Ulinzi wa Marekani umetawaliwa na raia wenye asili ya Israeli.
Uwezo kwanza vingine baadae
 
Mbona China, Japan, India na Singapore hawana hao watenda miujiza yako? Ni suala la kutumia akili. Siyo kila taifa lililoendelea limefanya hivyo kwa kutegemea wageni.

Kwani huyo Trump na Obama wameongeza nini kwa Marekani? Kwa nchi ambazo wageni huja na kuendelea kung'ang'ania uraia wa hata nchi wasizokuwa na uraia kama wahindi wakiiba na kutoroshea India na Ulaya, dhana hii inafaa. Ubunifu wa nchi hautegemei wageni vinginevyo Japan na Korea ya Kusini wasingewini
Ukizungumzia uwezo wa Korea kiuchumi usisubutu kutoitaja Marekani na uingereza. Wamewekeza kwenye karibu kila sekta. Sumsung, Lg na vitu vingi Zina ubia na wazungu
 
Kama ikulu ya marekani iliongozwa na mtoto wa mkenya Mzee Obama aliyeenda Marekani kusoma tu lakini akazaa uko. Sasa unataka utuaminishe unachokiamini kwa mfano upi!?
Ulinzi wa Marekani umetawaliwa na raia wenye asili ya Israeli.
Uwezo kwanza vingine baadae
Tafuta houseboy kama una mke mzr na watoto wakali uondoke nyumban miez mitatu halafu utuletee majibu. Pu...b..f
 
Uzawa ni dhana uchwara inatumiwa na watawala wa kiafrika. Asilimia kubwa ya nchi nyingi zilizoendelea ni kwa mchango mkubwa wa wageni
 
Ukizungumzia uwezo wa Korea kiuchumi usisubutu kutoitaja Marekani na uingereza. Wamewekeza kwenye karibu kila sekta. Sumsung, Lg na vitu vingi Zina ubia na wazungu
Lakini hawajawatawala bali wameshirikiana katika biashara tofauti na hawa wetu walioletwa na wakoloni nao wakageuka kuwa mzigo mkubwa tu huku wakiendelea kutubagua kwa kila eneo isipokuwa vyakula na fedha zetu tuendapo kununua kwenye uchuuzi wao.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom