Uzandiki na usanii wa bank za CRDB na NMB kwa AMCOS

FisadiKuu

JF-Expert Member
Nov 19, 2015
8,108
13,346
Habari wanabodi,

Kwa wasio na ufahamu AMCOS ni vyama vya ushirika ambavyo vinakusanya mazao kwenye vijiji mbalimbali kwa niaba ya chama kikuu cha ushirika. Mfano wa vyama vikuu vya ushirika ni Kilimanjaro Native Cooperative Union (KNCU), Kagera Cooperative Union (KCU), Mtwara Masasi Cooperative Union (MAMCU). Hivyo hivi vyama vikuu vinakuwa na AMCOS ambazo ndio wawakilishi wake kwa kila kijiji. AMCOS hizi zinakuwa na uongozi wake na nguvu ya kukopo na kukopesha kwa utaratibu maalum uliowekwa na Serikali. Pia AMCOS hizi zinakaguliwa mahesabu yake na zinafanya shughuli mbalimbali za maendeleo.

AMCOS zinajiendesha kutokana na ushuru wanaoupata kwenye mauzo ya mazao yao. Mfano, wanamkata kila mwanachama wake shillingi 70 kwa kila kilo ya zao alilouza. Hivyo kama AMCOS imepeleka mnadani Tani 800 ya zao fulani ushuru wake unakuwa ni Tshs. 56,000,000. Na pesa hizi zinatumika kwa shughuli mbalimbali za uendeshaji wa chama kama kulipa wazabuni, kulipa mishahara wafanyakazi, kulipa walinzi na kulipa wachukuzi n.k

Kutokana na msimu wa Korosho 2018/19 kuwa na changamoto kadhaa. AMCOS zilipata ushuru wa shillingi 14 tu ambao kwa uhalisia haukuweza kulipa madeni yote waliyonayo pamoja na mishahara ya wafanyakazi wake. Hivyo iliwalazima Chama kikuu kuongea na Mabenki ili AMCOS ziweze kukopeshwa fedha kwa ajili ya uendeshaji wa mwanzo wa vyama vyao kwa Msimu huu wa 2019/2020. Bank za CRDB na NMB ambao ni wadau pia wanufaika wakubwa sana kwa wakulima wa korosho walikibali kuwakopesha fedha AMCOS kwa ajili ya uendeshaji wa vyama mpaka hapo watakapoanza kupata ushuru wao.

Kwa faida tu ya wasiofahamu, kwa mkoa wa Mtwara pekee korosho inaingiza zaidi ya Billion 800 kwa wakulima. Na asilimia 99 ya hizo billion 800 huwa zinapita kwenye bank hizi kubwa mbili.

Cha kusikitisha mchakato mikopo ulishaisha mapema kabla hata ya kufungua maghala yao ili wapate mikopo hiyo kwa ajili ya marekebisho na maandalizi mbalimbali. Kwa takribani wiki 3 sasa AMCOS zimekuwa zikizungushwa na bank hizi pamoja na kwamba walikamilisha vigezo vyote vya kupata mkopo.

Cha kusikitisha zaidi AMCOS ziliamua kutugeukia wadau wa korosho angalau waweze kupata kiasi cha kuweza kuendesha vyama vyao na ingawa hali zetu pia ni mbaya ila wadau wengi tumefanya kazi bega kwa bega na AMCOS kwa kusaidiana vijisenti tangia wanafungua maghala mpaka sasa ambapo mnada wa kwanza ni Ijumaa ya tarehe 1 mwezi wa 11 na kwakuwa kuna dalili ya wanunuzi wengi kujitokeza ndio Bank zimetuma statement kwa AMCOS kwamba wataanza kuwaingizia fedha walizoomba jumatatu ya wiki ijayo.

Huu ni ubabaishaji mkubwa na Usanii mkubwa wa hizi bank zetu na tunaomba viongozi mnaosoma hapa hili lifike kwa Waziri Mkuu au hata Mheshimiwa Rais na bank zipigwe stop kwa ulaghai wanaotaka kuufanya. Kwanza, riba ambazo wameziweka ni kubwa sana lakini pia hakutakuwa na maana ya kuwapa mkopo wa kuendesha chama wakati tayari walishauza mazao yao kadhaa na vyama vitakuwa vimeshapata ushuru wao mpaka hiyo wiki ijayo.

Inasikitisha mteja wako anayekuingizia mabilioni ya fedha anakuomba million 4 ya kuweza kujiendesha unamfanyia usanii. CRDB na NMB acheni uzandiki, kungekuwa na bank ingine imara lazima tungeshawishi hivi vyama viwahame.
 
Waache uzandiki..hopefully taarifa hii itawafikia viongozi wa juu

Sema paragraph ya mwisho kuna typing error..rekebisha
 
Ndugu, bank tajwa hapo juu usizilaumu bure kwani wao walisubiri kuona kama msimu wa korosho utavurugwa na serikali tena kama mwaka jana, jambo ambalo lingesababisha hizo Amcos kushindwa kurejesha mikopo hio kwa muda waliokubaliana. Sasa banks zimejiridhisha kua msimu utaendehswa kama zamani ndio maana wanataka sasa kutoa hela.
 
Umeongea kitu muhimu ila hio aya ya mwisho waombe @moderators wakufanyie marekebisho haraka mkuu
 
Mkuu serikali ilishasema zaidi ya mara 3 kupitia Waziri Mkuu akijibu maswali ya papo kwa papo na kupitia Waziri wa Kilimo mara mbili tofauti walishasema mwaka huu serikali haitaingilia na itaachia wadau wanunue.

Pili, kama concern yao ilikuwa ni hiyo ni bora wangesema mapema kwamba hatutaweza tafuteni pesa sehemu nyingine kuliko kutaka kuwapa Million 4 sijui 5 wakati vyama vitakuwa zishapata zaidi ya hizo pesa kwenye mnada wa kwanza.
Ndugu, bank tajwa hapo juu usizilaumu bure kwani wao walisubiri kuona kama msimu wa korosho utavurugwa na serikali tena kama mwaka jana, jambo ambalo lingesababisha hizo Amcos kushindwa kurejesha mikopo hio kwa muda waliokubaliana. Sasa banks zimejiridhisha kua msimu utaendehswa kama zamani ndio maana wanataka sasa kutoa hela.
 
Habari wanabodi,

Kwa wasio na ufahamu AMCOS ni vyama vya ushirika ambavyo vinakusanya mazao kwenye vijiji mbalimbali kwa niaba ya chama kikuu cha ushirika. Mfano wa vyama vikuu vya ushirika ni Kilimanjaro Native Cooperative Union (KNCU), Kagera Cooperative Union (KCU), Mtwara Masasi Cooperative Union (MAMCU). Hivyo hivi vyama vikuu vinakuwa na AMCOS ambazo ndio wawakilishi wake kwa kila kijiji. AMCOS hizi zinakuwa na uongozi wake na nguvu ya kukopo na kukopesha kwa utaratibu maalum uliowekwa na Serikali. Pia AMCOS hizi zinakaguliwa mahesabu yake na zinafanya shughuli mbalimbali za maendeleo.

AMCOS zinajiendesha kutokana na ushuru wanaoupata kwenye mauzo ya mazao yao. Mfano, wanamkata kila mwanachama wake shillingi 70 kwa kila kilo ya zao alilouza. Hivyo kama AMCOS imepeleka mnadani Tani 800 ya zao fulani ushuru wake unakuwa ni Tshs. 56,000,000. Na pesa hizi zinatumika kwa shughuli mbalimbali za uendeshaji wa chama kama kulipa wazabuni, kulipa mishahara wafanyakazi, kulipa walinzi na kulipa wachukuzi n.k

Kutokana na msimu wa Korosho 2018/19 kuwa na changamoto kadhaa. AMCOS zilipata ushuru wa shillingi 14 tu ambao kwa uhalisia haukuweza kulipa madeni yote waliyonayo pamoja na mishahara ya wafanyakazi wake. Hivyo iliwalazima Chama kikuu kuongea na Mabenki ili AMCOS ziweze kukopeshwa fedha kwa ajili ya uendeshaji wa mwanzo wa vyama vyao kwa Msimu huu wa 2019/2020. Bank za CRDB na NMB ambao ni wadau pia wanufaika wakubwa sana kwa wakulima wa korosho walikibali kuwakopesha fedha AMCOS kwa ajili ya uendeshaji wa vyama mpaka hapo watakapoanza kupata ushuru wao.

Kwa faida tu ya wasiofahamu, kwa mkoa wa Mtwara pekee korosho inaingiza zaidi ya Billion 800 kwa wakulima. Na asilimia 99 ya hizo billion 800 huwa zinapita kwenye bank hizi kubwa mbili.

Cha kusikitisha mchakato mikopo ulishaisha mapema kabla hata ya kufungua maghala yao ili wapate mikopo hiyo kwa ajili ya marekebisho na maandalizi mbalimbali. Kwa takribani wiki 3 sasa AMCOS zimekuwa zikizungushwa na bank hizi pamoja na kwamba walikamilisha vigezo vyote vya kupata mkopo.

Cha kusikitisha zaidi AMCOS ziliamua kutugeukia wadau wa korosho angalau waweze kupata kiasi cha kuweza kuendesha vyama vyao na ingawa hali zetu pia ni mbaya ila wadau wengi tumefanya kazi bega kwa bega na AMCOS kwa kusaidiana vijisenti tangia wanafungua maghala mpaka sasa ambapo mnada wa kwanza ni Ijumaa ya tarehe 1 mwezi wa 11 na kwakuwa kuna dalili ya wanunuzi wengi kujitokeza ndio Bank zimetuma statement kwa AMCOS kwamba wataanza kuwaingizia fedha walizoomba jumatatu ya wiki ijayo.

Huu ni ubabaishaji mkubwa na Usanii mkubwa wa hizi bank zetu na tunaomba viongozi mnaosoma hapa hili lifike kwa Waziri Mkuu au hata Mheshimiwa Rais na bank zipigwe stop kwa ulaghai wanaotaka kuufanya. Kwanza, riba ambazo wameziweka ni kubwa sana lakini pia hakutakuwa na maana ya kuwapa mkopo wa kuendesha chama wakati tayari walishauza mazao yao kadhaa na vyama vitakuwa vimeshapata ushuru wao mpaka hiyo wiki ijayo.

Inasikitisha mteja wako anayekuingizia mabilioni ya fedha anakuomba million 4 ya kuweza kujiendesha unamfanyia usanii. CRDB na NMB acheni uzandiki, kungekuwa na bank ingine imara lazima tungeshawishi hivi vyama viwahame.

Abdulmarik soma habari hii
 
Korosho ni uwanja wa upigaji.

..............Bank zinapiga, Wadau wanapiga, Viongozi wa AMCOs wanapiga mwisho wa siku mkulima anabaki na maumivu..
 
Korosho ni uwanja wa upigaji.

..............Bank zinapiga, Wadau wanapiga, Viongozi wa AMCOs wanapiga mwisho wa siku mkulima anabaki na maumivu..
Mkuu ingekuwa ni upigaji tu sidhani kama mbuzi wangekunywa soda msimu wa 2017/18..

Na hakuna viongozi wenye changamoto na lawama kama hawa viongozi wa AMCOS. Hawa jamaa wanapata shida sana ingawa pia wamo wapigaji.
 
Mkuu ingekuwa ni upigaji tu sidhani kama wangekunywa soda msimu wa 2017/18..

Na hakuna viongozi wenye changamoto na lawama kama hawa viongozi wa AMCOS. Hawa jamaa wanapata shida sana ingawa pia wamo wapigaji.

Viongozi wa AMCOs wakishirikiana na maafisa Ushirika Mungu anajua wanachowafanya wakulima.
 
Viongozi wa AMCOs wakishirikiana na maafisa Ushirika Mungu anajua wanachowafanya wakulima.
Ni kweli wapo ambao sio waaminifu. Hata sie wadau tunapata usumbufu mkubwa sana na hawa viongozi..

Maafisa ushirika nao nilimsikia Bashe akisema wataangaliwa kwa umakini na wale wenye malalamiko mengi wataondolewa..
 
Mkuu serikali ilishasema zaidi ya mara 3 kupitia Waziri Mkuu akijibu maswali ya papo kwa papo na kupitia Waziri wa Kilimo mara mbili tofauti walishasema mwaka huu serikali haitaingilia na itaachia wadau wanunue.

Pili, kama concern yao ilikuwa ni hiyo ni bora wangesema mapema kwamba hatutaweza tafuteni pesa sehemu nyingine kuliko kutaka kuwapa Million 4 sijui 5 wakati vyama vitakuwa zishapata zaidi ya hizo pesa kwenye mnada wa kwanza.
Ukawaamini hawa watu? Kama mwaka jana Magufuli alimuagiza Majaliwa atafute wafanyabiashara wa kununua korosho ndani ya wiki,

Majaliwa kahangaika akatafuta na kuwapata, siku anampelekea taarifa Magufuli, Magufuli akakataa akasema korosho itanunuliwa na jeshi.
Hadi hapo bado unaamini majibu ya Majaliwa? Magufuli hatabadilisha tena mawazo?

Na utamlaumu mfanyabiashara kama benki kuingiwa wasiwasi na matamko ya serikali?

Achilia mbali hilo, serikali ikasema itanunua korosho za wakulima na ndani ya muda mfupi itawalipa wote, uliona malipo kwa wakulima yalivyokuwa? Hili liliathiri vipi benki? Bado tu unashauri benki kuamini serikali?

Magufuli pia alitoa tamko kuwq mkulima akilipwa fedha zake benki, ni marufuku kuikata hela juu kwa juu hata kama anadaiwa fedha za pembejeo na vyama vya ushirika, hadi mkulima atoe hela yake, akafanye matumizi yake na ikibaki ndio alipe deni, tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo deni lilikatwa juu kwa juu.. Sasa mkuu kama wewe ni mkopeshaji utafanya biashara kwenye mazingira haya?

Bado sijagusia lile tamko la jeshi kubangua korosho na jinsi lilivyofeli
 
Ukawaamini hawa watu? Kama mwaka jana Magufuli alimuagiza Majaliwa atafute wafanyabiashara wa kununua korosho ndani ya wiki,

Majaliwa kahangaika akatafuta na kuwapata, siku anampelekea taarifa Magufuli, Magufuli akakataa akasema korosho itanunuliwa na jeshi.
Hadi hapo bado unaamini majibu ya Majaliwa? Magufuli hatabadilisha tena mawazo?

Na utamlaumu mfanyabiashara kama benki kuingiwa wasiwasi na matamko ya serikali?

Achilia mbali hilo, serikali ikasema itanunua korosho za wakulima na ndani ya muda mfupi itawalipa wote, uliona malipo kwa wakulima yalivyokuwa? Hili liliathiri vipi benki? Bado tu unashauri benki kuamini serikali?

Magufuli pia alitoa tamko kuwq mkulima akilipwa fedha zake benki, ni marufuku kuikata hela juu kwa juu hata kama anadaiwa fedha za pembejeo na vyama vya ushirika, hadi mkulima atoe hela yake, akafanye matumizi yake na ikibaki ndio alipe deni, tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo deni lilikatwa juu kwa juu.. Sasa mkuu kama wewe ni mkopeshaji utafanya biashara kwenye mazingira haya?

Bado sijagusia lile tamko la jeshi kubangua korosho na jinsi lilivyofeli
Boss katika hao wahanga tunaodai AMCOS mimi ni mmoja wao. Nadai fedha nyingi tu na mpaka leo nazungushwa tu..

Lakini hiyo isiwe sababu ya kuacha kusaidiana maana hawa wamekuwa wadau wetu kwa muda mrefu tu.

Mkuu serikali haiwezi kurudia makosa waliyofanya kwenye korosho kamwe. Rais hakufahamu vizuri biashara ya korosho ina mkono mrefu kiasi gani akaingia kichwa kichwa akaingia kichwa kichwa kilichowapata hawatakaa warudie.. Watu walikaa pale Ikulu wakampotosha Rais walifikiri korosho ni mchezo mchezo.

Mkuu mnada wa kwanza ni leo, saa kumi tutajua mbivu na mbichi..
 
Boss katika hao wahanga tunaodai AMCOS mimi ni mmoja wao. Nadai fedha nyingi tu na mpaka leo nazungushwa tu..

Lakini hiyo isiwe sababu ya kuacha kusaidiana maana hawa wamekuwa wadau wetu kwa muda mrefu tu.

Mkuu serikali haiwezi kurudia makosa waliyofanya kwenye korosho kamwe. Rais hakufahamu vizuri biashara ya korosho ina mkono mrefu kiasi gani akaingia kichwa kichwa akaingia kichwa kichwa kilichowapata hawatakaa warudie.. Watu walikaa pale Ikulu wakampotosha Rais walifikiri korosho ni mchezo mchezo.

Mkuu mnada wa kwanza ni leo, saa kumi tutajua mbivu na mbichi..
Wanaweza wasirudia makosa, lakini huwezi kulaumu benki kwa kuwa sceptical mkuu, na kupiga chenga

Haupo kwenye kichwa cha Magufuli hadi utoe guarantee kuwa ata act vip

Pia kuna suala la kangomba ambao walikuwa player wakubwa kwenye hii ishu ya korosho na Serikali imetamka imewapiga marufuku kabisa msimu huu,

Sasa hii nayo itavuruga equilibrium iliyokuwepo kwa muda mrefu, na kuacha uncertainity,
Na pia haifahamiki Serikali ita act vip tena ili kuhakikisha kweli hakuna kangomba aliyegusa korosho za mkulima.
So suala la korosho bado maji hayajatulia vizuri, baada ya kuvurugika mwaka jana

Benki siwezi kuwalaumu kwa kupiga chenga
 
Mkuu kuna msemo unasema "akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki" yes biashara haina urafiki lakini ni bora wangewaambia kabisa kwamba hatuwapi..

Mbona sie wadau tumenyimwa mikopo na hizo taasis na tulielewa tu. Alafu suala la kangomba mkuu serikali haiwezi kusema wazi eti kangomba ni ruksa, haiwezi lakini watu wamenunua na watalipwa.

Mkuu mnada ushapigwa na korosho yote ilioingia mnadani ishauzwa. Tunasubiri mnada wa pili sasa.. Tunajua sasa simu za mabenki kwa AMCOS na sie wadau zitakuwa nyingi sana.
Wanaweza wasirudia makosa, lakini huwezi kulaumu benki kwa kuwa sceptical mkuu, na kupiga chenga

Haupo kwenye kichwa cha Magufuli hadi utoe guarantee kuwa ata act vip

Pia kuna suala la kangomba ambao walikuwa player wakubwa kwenye hii ishu ya korosho na Serikali imetamka imewapiga marufuku kabisa msimu huu,

Sasa hii nayo itavuruga equilibrium iliyokuwepo kwa muda mrefu, na kuacha uncertainity,
Na pia haifahamiki Serikali ita act vip tena ili kuhakikisha kweli hakuna kangomba aliyegusa korosho za mkulima.
So suala la korosho bado maji hayajatulia vizuri, baada ya kuvurugika mwaka jana

Benki siwezi kuwalaumu kwa kupiga chenga
 
Mkuu kuna msemo unasema "akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki" yes biashara haina urafiki lakini ni bora wangewaambia kabisa kwamba hatuwapi..

Mbona sie wadau tumenyimwa mikopo na hizo taasis na tulielewa tu. Alafu suala la kangomba mkuu serikali haiwezi kusema wazi eti kangomba ni ruksa, haiwezi lakini watu wamenunua na watalipwa.

Mkuu mnada ushapigwa na korosho yote ilioingia mnadani ishauzwa. Tunasubiri mnada wa pili sasa.. Tunajua sasa simu za mabenki kwa AMCOS na sie wadau zitakuwa nyingi sana.
Kwa hiyo Kangomba ipo kama kawaida na serikali haina shida nayo?
 
Back
Top Bottom