Uzalendo ni nini?

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
Wana jamvi,

Haya tunahitaji maoni yenu jinsi ya kuweza kutoa elimu ya uzalendo kwa mafisadi na wananchi kwa ujumla

Kwanza naomba mtambue nini maana ya uzalendo:

UZALENDO ni ile hali ya mtu kuipenda na kuithamini nchi yake na kuweka maslahi ya taifa lake mbele. Uzalendo ni neno dogo lakini maana inayobebwa na neno UZALENDO ni kubwa.

Elimu ya uzalendo ni elimu ambayo imekosekana kwenye jamii yetu. Hili linatokana na watu kutofundishwa kuipenda nchi yao. Upungufu huo ndio ambao hupelekea watu mbalimbali katika jamii kutenda mambo ambayo hushangaza watu na kuacha wengi katika mfadhaiko wa kujiuliza kama huyu mtu anaipenda nchi yake ama la.

Vitendo kama vya utoaji rushwa, upokeaji rushwa, upoteaji wa tamaduni (kutothamini kabila lako na chanzo chake), kutojiamini kama Mtanzania kwamba wewe ni bora kama wengine, wivu wa maendeleo uliyojikita kwa Mtanzania mwenzako na sio kwa mtu wa taifa lingine, kutothamini cha kwako na kutukuza cha mwenzako (Bidhaa za Tanzania, lugha ya Kiswahili, timu za mpira wa Ulaya) na kutojua ya kwamba utunzaji wa maslahi ya taifa lako ni jukumu lako na langu pia na sio la serikali pekee..

NAWASILISHA
MAPINDUZIIII DAIMAAAAAA
 
hivi kwa nini sisi watanzania hasa vijana tunakosa uzalendo wa kweli kwa nchi yetu? Tunaishia kutawa liwa na kuwa watumwa wa kuuza kura kwa wanasiasa mafisadi? Hata leo wakifufuka hao tunaowaita mashujaa watajuta kwa kujitolea kwao kwa ajili ya kututafutia maisha mazuri watanzania. Tatusaidiki.
 
kwa kweli wana JF ni mashahidi kwamba hapa tz karibu kila kitu kinakwena mrama.ukiangalia ktk siasa ramani haisomi.kweye uchumi umejaa ubabaishaji mtupu,ktk sekta ya afya migogoro tu bila ya huduma bora nk.ukiwauliza wanazuoni wetu pasi na shaka kabisa utajibiwa"hakuna uzalendo"naomba mnifahamishe hasa kuhusu huo uzalendo.
 
Habari zenu wajamvi wote.

Husika na kichwa cha habari juu,Nini MAANA YA UZALENDO?

NA UZALENDO HUO HUPATIKANA WAPI???

NA ILI UWE MZALENDO UNATAKIWA KUFANYA NINI??

NA UZALENDO HUO HUKAA MOYONI AU AKILINI MWA BINADAMU..?

JE NI KWELI YANAYOTOKEA KATIKA NCHII HII NI YA KIZALENDO AU KIUTUMWA
 
umenikumbusha somo la siasa, ngoja wenye uzalendo waje watakuja kukuijibu. maana si wengine tunaogopa maswali tunajua pepa.
 
Nawasalimia wote;
Hiyo nyimbo ya Uzalendo huwa tunaimba tu.
kwa mtazamo wangu UZALENDO hupatikana deep ndani ya MOYO.
Nyoyo huwa zinatenda haijalishi Rangi, kabila,dini nk. Umuhimu wake ni msukumo wakujituma.
 
Uzalendo = Patriotism,

Uzohali = Nationalism.


===

Quotes about Patriotism



"A patriot must always be ready to defend his country against his government." --― Edward Abbey


"The duty of a patriot is to protect his country from its government." --― Thomas Paine

"The greatest patriotism is to tell your country when it is behaving dishonorably, foolishly, viciously." --― Julian Barnes, Flaubert's Parrot


"The notion that a radical is one who hates his country is naïve and usually idiotic. He is, more likely, one who likes his country more than the rest of us, and is thus more disturbed than the rest of us when he sees it debauched. He is not a bad citizen turning to crime; he is a good citizen driven to despair." --― H.L. Mencken

zubedayo_mchuzi
Kijana leo
life is Short
thumbs_patriotism_means_to_stand_by_the_country_not_by_the_president_or_any_other_public_official_theodore_roosevelt.jpg


 
Kwa Bahati Mbaya Mtu Ukiwa CCM Ndio Unaonekana MZALENDO.
Uzalendo Sio Kuvaa Skafu Ya Bendera Ya Taifa.
Uzalendo Sio Kuisifia Serikali Pale Inapotimiza Wajibu Wake.
Uzalendo Sio Kwenda JKT.
Uzalendo Sio Kuimba Nyimbo Za Kusifu.
UZALENDO NI HISIA Za Mtu ZIZOKUJA KWA WAKATI FULANI. NA WALA UZALENDO HAUFUNDISHWI HAKUNA SHULE INAYOFUNDISHA UZALENDO DUNIANI.
 
Back
Top Bottom